Showing posts with label UFALME WA MUNGU UMEKARIBIA. Show all posts
Showing posts with label UFALME WA MUNGU UMEKARIBIA. Show all posts

Mtu mmoja(1) akiingia mbinguni, watu elfu moja(1000) wanaingia kuzimu-.Ushuhuda na Mchungaji Park Yong Gyu.


Ushuhuda wa Mbingu na Kuzimu, 1-1000, na Mchungaji Park Yong GyuMchungaji Park alikuwa amefariki kutokana na shinikizo la damu. Lakini kwa neema ya Mungu, maisha yake yaliongezwa kwa miaka 20 nyingine.
Hata hivyo, kwa miaka minne ya kwanza, hakuweza kuzungumza kutokana na hali yake. Alikuwa na umri wa miaka 50 hivi alipofufuliwa. Wakati wa kifo chake, Bwana alimpeleka mbinguni na kuzimu.Nataka ujue ukiwa na kiburi na majivuno utajiletea laana.
Nilikuwa na kanisa kubwa la washiriki 5000 lakini nilipigwa na Mungu kutokana na kiburi changu. Sasa namcha Mungu. Nilikuwa nikimiliki mali nyingi sana zenye kufikia thamani ya dola za kimarekani milioni 150, ambazo ni sawa na bilioni 349.86 za kitanzania.
Nilikuwa na magari matano(5) ya kifahari, Lakini baada ya haya niliyoyaona kwa neema ya MUNGU, niliyatoa yote na kuyagawa. Wokovu hauwezi kupatikana kwa mali zako bali kwa imani. Tafadhali, ninawasihi mashemasi, wazee, na viongozi wengine katika makanisa yao kumtumikia MUNGU chini ya wachungaji wenu kwa mioyo yenu yote.

Mnamo Desemba 19, baada ya kumaliza chakula changu cha mchana na nilipokuwa nikipumzika, nilianza kuhisi maumivu makali. Nilihisi kana kwamba nitakufa. Maumivu hayakuvumilika. Kisha nikapoteza fahamu. Nilipozinduka, watu waliokuwa karibu nami walisema miezi minne imepita.
Nilikuwa katika hali tete na nikiwa katika hali hiyo, daktari alikuwa amesema kwamba ningekufa.Kweli mara tu baada ya kufa, mara nikaona watu wawili wakiingia chumbani kwangu.
Lakini watu hawa walikuwa wameingia kwenye chumba changu kupitia ukuta. Nilipiga kelele, “Nani, wewe ni nani!! Nyumba yangu itabomoka ukifanya hivyo!!” Kisha malaika wakasema, “Sisi ni malaika tulioshuka kutoka mbinguni. Sisi tunatoka katika ufalme wa Mungu.” Nuru angavu ilimulika kutoka kwa malaika. Malaika waliniweka kati yao.
Nikauliza, “Mlikujaje ?”Walinijibu “Umekufa, familia yako inalia kwa huzuni nyingi huko,Baba MUNGU amependezwa kukupa muda zaidi wa kuishi. Ila kwa sasa, anataka kukuonyesha mbingu na kuzimu.
Atakuonyesha nawe utakwenda shuhudia kwa watu wa duniani. Kupitia ushuhuda wako idadi ya watu wanaoishia kuzimu ipunguzwe na idadi ya wanaokwenda mbinguni iongezeke. Hii itakuwa shabaha yako. Mungu alituagiza tukuambie usichelewe. Ukichelewa, hutaweza kuzuru mbinguni na kuzimu.” Malaika wa kulia kwangu alijitambulisha. “Ninafanya kazi kwa ajili ya Yesu katika ufalme wake. Yesu aliniita na kuniamuru nishuke duniani, akaniamuru nikupeleke mbinguni.
Kisha malaika aliyesimama upande wangu wa kushoto akajitambulisha. Alisema, "Wakati ulipozaliwa na hadi ulipokufa, nilikuwa pamoja nawe." Wakati huo, sikuelewa malaika alikuwa anamaanisha nini. Sasa najua. Yeye ni malaika wangu mlezi. Mimi nikasema, “Siwezi kwenda! Sitakwenda! Mimi ni mchungaji! Siwezi kukutana na Bwana katika hali hii ya kimwili. 
 
Ninataka kumwona nikiwa mtu mwenye afya njema. Pengine naenda kupokea karipio zaidi kuliko pongezi kutoka kwa Bwana. Nina kiburi mimi na majivuno, sasa nimelaaniwa na ni mgonjwa. Je, ninawezaje kuingia mbinguni? Ninaogopa sana. Tafadhali rudi mbinguni na umwombe Bwana aniponye. Kisha urudi na kunipeleka mbinguni kupitia ndoto yangu.
Tafadhali malaika omba rehema kwa niaba yangu.” Lakini malaika hawakusikiliza hoja yangu. Walinivua nguo zangu na kusema kwamba zilikuwa chafu sana kuvaliwa mbinguni. Kisha wakanivalisha gauni jeupe. Walishika mikono yangu na tukaruka moja kwa moja hadi mbinguni. Tuliruka kupitia mawingu na nilipotazama chini, niliona dunia ikizidi kuwa ndogo. Waliponiruhusu niende, ndani ya futi 3 kutoka kwangu, niliona Barabara ya Dhahabu isiyo na mwisho.
Tulikuwa bado tunaruka na kwa kasi kubwa. Kuangalia mbele, niliona mwanga mkali unaowaka. Sikuweza kutazama moja kwa moja kwenye mwanga.
 
 Nikawauliza wale malaika, Nuru inatoka wapi? Malaika akajibu, "Inatoka mbinguni." Nilipotazama mbele, nilijiwazia, “Lo! Ni kubwa!” Mbele yangu niliona makundi ya watu waliovalia mavazi meupe wakiruka mbele.
Niliwauliza wale malaika, “Ni nani hao?” Malaika akajibu, “Hao ndio waliokuwa wamemtumikia Mungu kwa uaminifu na kumtumaini Yesu kwa kutii na kufuata mwongozo wa Roho Mtakatifu kwa moyo wao wote. Miili yao imekufa duniani. Sasa ni nafsi zinazoelekea mbinguni.”Malaika mwingine akaendelea, “Kuna milango kumi na miwili(12) mbinguni. Wakati nafsi iliyookolewa inapokuja mbinguni, lazima iingie kupitia mojawapo ya milango hiyo.” Tulikuwa tumesimama kwenye lango la kusini lakini lilikuwa limefungwa.
Tulipokuwa tukingoja, nilimuuliza malaika, “Malaika, kwa nini lango hili halifunguki?” Malaika akajibu, "Ni kwa sababu huimbi wimbo wa kuabudu wa mbinguni." Niliuliza, “Malaika, mimi nilikuwa na kiburi na majivuno sana na matokeo yake nimelaaniwa na ugonjwa. Siko vizuri kuimba nyimbo za kuabudu za duniani. Je, ninawezaje kuimba nyimbo za kuabudu za mbinguni wakati sijawahi kuzisikia kabla?” Malaika akajibu, “Umesema kweli. Lakini bado unapaswa kujitayarisha kuabudu.
Wewe ni mtu wa kujivunia lakini jiandae kuimba.” Malaika walianza kuimba. Walipokuwa wakiimba, nilianza kuimba pamoja nao. Ikawa asili kwangu! Lakini basi, waliacha kuimba baada ya muda mfupi. Niliuliza, “Kwa nini umeacha kuimba? Nilikuwa nikifurahia.” Kisha nikagundua tayari tumeingia kwenye geti.
 
 Kwa jinsi mbingu ilivyo nzuri ,sitaweza kamwe kuelezea matukio ya mbinguni kwa maneno yangu ya kidunia. Nikasema, “Bwana! Asante sana! Ingawa, nilikuwa na kiburi na majivuno sana na kulaaniwa kwa ugonjwa, bado umenileta mbinguni ili kunionyesha pande zote. Tukio la mbinguni lililojitokeza mbele ya macho yangu lilikuwa lisiloelezeka. Kisha nikasikia sauti ya Mungu, “Mchungaji wangu mpendwa Park, Yong Gyu, ninakukaribisha.
Umefunga safari ndefu hapa.” Sauti ya Bwana ilijaa upendo na huruma. Nilijibu huku nikilia kwa machozi, “Bwana,….” Malaika walinisimamisha kulia mara moja, huku akisema “Umekuwa mchungaji kwa miaka 20. Je, hujui maandiko ya MUNGU?,kuwa mbinguni hakuna machozi. 
 
Tafadhali acha!” Sikuweza hata kulia.
Kisha Bwana akaniuliza maswali matano(5).
1. “Ulitumia muda gani kusoma Neno (biblia)? 2. Ulitoa kiasi gani cha sadaka?
3. Je, umehubiria watu mara ngapi?
4. Je, ulitoa zaka ipasavyo?
5. Ulitumia muda gani katika maombi?” Sikuweza kujibu swali la tano.
Bwana alinikemea kwa swali la tano. BWANA akaniambia “Baada ya kuwa mchungaji mkuu wa kanisa, umekuwa mvivu sana katika maombi. Na umekuwa na shughuli nyingi sana yakupasa ujue kuwa si kisingizio Kwangu!” Ilinibidi nitubu baadaye. Bwana aliendelea na kuniambia, “Malaika watakuonyesha sehemu nyingi mbinguni na kuzimu. Angalia kote kama unavyotaka. 
 
Utaondoka baada ya kushuhudia sehemu nyingi tofauti mbinguni na kuzimu.” Lakini Bwana hakuni ruhusu nione sura yake.Malaika walinipeleka kwanza sehemu tatu tofauti mbinguni. Sehemu ya kwanza, niliona watoto wadogo wakiishi pamoja. Sehemu ya pili ilikuwa mahali ambapo watu wazima waliishi. Sehemu ya tatu ilikuwa ni ya wale waliofika mbinguni kana kwamba kwa bahati bahati. Ingawa walifika mbinguni, walikuwa wameifika kwa aibu.
 
Watu wengi sana walikuwa wameniuliza watoto wadogo walikuwa na umri gani. Nadhani wanaonekana kufikia umri wa kusoma chekechea. Sikuweza tambua kuhusu jinsia ila kila mtoto alikuwa na malaika wake mtoto wa kuongozana nao. Mbinguni, roho nyingi zitakuwa na makao yao binafsi (Yohana 14:22). Hata hivyo, kulikuwa na wengine ambao hawakuwa na nyumba.
Nitalieleza hili baadaye. Isitoshe, watoto hawakuwa na nyumba zao binafsi pia. Niliuliza, “Watoto pia ni nafsi, kwa nini hawana nyumba zao wenyewe?”Malaika akajibu, “Kama vile watu duniani wanahitaji vifaa vya kujenga nyumba zao, sisi mbinguni pia tunahitaji vifaa vya kujenga hapa. Wakati mtu anatumikia kanisa na wengine kwa uaminifu kwa Bwana, matendo hayo yatakuwa nyenzo kwa ajili ya nyumba ya mtu mbinguni. 
 
Vifaa vinapotolewa, malaika waliopewa kazi ya kujenga nyumba ya mtakatifu wataenda kufanya kazi ya kuijenga. Watoto walio chini ya umri wa uwajibikaji hawajajenga nyenzo zozote za kujenga nyumba. Kwa maneno mengine, hawakuwa na wakati au nafasi ya kupata tuzo/nyenzo zao. Ndiyo maana hawana nyumba.”Niliendelea na maswali yangu, Na kuuliza “Nitafanya nini duniani ili kutoa nyenzo(materials) zaidi kwa ajili ya kujengea nyumba yangu?”
 
Malaika wakajibu, “Kuna mambo saba(7) ambayo mtu lazima afanye yatayosababisha mbinguni kupata vifaa/nyezo(materials) vitakavyo wezesha kujenga nyumba yake mbinguni.
1. La kwanza ni mkusanyiko wako wa ibada na sifa kwa Mungu.
2. Pili ni muda wako binafsi wa kusoma biblia.
3. Tatu, muda wako binafsi wa kusali.
4. Nne, muda wako ulioutumia kuhubiri injili kwa watu.
5. Tano, sadaka ya uaminifu ya mtu kwa Bwana.
6. Sita, zaka zao za utii kwa Mungu.
7. Mwisho, muda wao walioutumia kutumikia kanisa kwa njia yoyote ile.
 
Haya ni matendo au kazi za utii ambazo ndani yake mtu hukusanya nyenzo/vifaa kwa ajili ya kujengewa makao yao ya mbinguni. Ikiwa moja itakosekana katika maeneo haya, hawatakuwa na vifaa vya kujenga nyumba yao.Kulikuwa na watu wengi mbinguni na wasio na nyumba.
Wengi ambao hawakuwa na nyumba walikuwa wachungaji, mashemasi, wazee, n.k. Niliuliza kwa udadisi, “Watoto wanaishi wapi wakati huo?” Malaika wakajibu, "Wanaishi hapa." Nilipotazama pande zote, walikuwa wamekusanyika katika bustani yote ya maua. Bustani ya maua ilikuwa nzuri sana na harufu nzuri. Tukio hilo lilikuwa zaidi ya vile ningeweza kuelezea kwa maneno yangu. Sehemu ya pili ilikuwa kwa watu wazima waaminifu.
 
Kuna tofauti kati ya wokovu na thawabu. Mahali hapa palikuwa na nyumba nyingi sana. Nyumba zilijengwa kwa vito vya kupendeza na mawe adimu. Baadhi ya nyumba zilikuwa juu kama maghorofa ya juu zaidi duniani. Watu hao ambao walikuwa wamemtumikia Bwana kwa uaminifu walipokuwa wakiishi duniani walijenga nyumba zao kwa vito vya kupendeza na mawe adimu. Katika mahali hapa, watu wote walionekana wana wastani wa umri wa miaka 20 hadi 30.
 
  Hakuna wagonjwa, wazee, au vilema.Nilimuulizia mzee niliyemjua akiwa duniani, mzee anayeitwa, Oh, Im Myung. Alikufa akiwa na umri wa miaka 65. Alikuwa mtu mfupi sana, yaani mrefu kama mtoto wa darasa la 2 katika shule ya msingi. Alikuwa ameugua ugonjwa adimu unaoitwa rickets. Hata hivyo kwenye biblia, alikuwa amesoma hadi uzamivi(PHD). Alikuwa ameandika maoni mengi. Nilikutana naye Mbinguni, na hapo alikuwa mrefu na mzuri. Hakuwa mgonjwa tena bali mzima wa afya.
 
 Mbinguni ni mahali pazuri sana!! Mimi nimejawa na shauku kamili ya matarajio ya mbingu! Tafadhali amini ninachosema wapendwa!Sehemu ya tatu ni mahali ambapo waliookolewa kwa aibu wamekusanyika. Kijiji hiki ni kikubwa sana kwa ukubwa. Mahali hapa ni kubwa mara kadhaa kuliko mahali ambapo roho zilikaa mahali pa pili ambapo nyumba zimetengenezwa kwa vito na mawe adimu. Nilifika mahali hapa nikiendesha gari la dhahabu. Nilikuwa nimefika kwa kasi kubwa. Mahali hapa palikuwa mbali sana na sehemu nzuri za mbinguni. Niliwauliza malaika, “Naona nyika kubwa na mashamba. Kwa nini sioni nyumba?"Malaika akajibu, "Unachoona ni nyumba."
 
 Niliona nyumba kubwa pana za gorofa. Umbo la nyumba hizo lilinikumbusha banda kubwa la kuku au aina fulani ya ghala. Nyumba hizi zilikuwa chakavu sana. Kijiji hiki na nyumba zilikuwa kwa ajili ya roho zilizookolewa kwa aibu. Kulikuwa na nyumba nyingi kubwa zenye sura mbovu. Kijiji hiki ni kikubwa mara kadhaa kuliko mahali ambapo roho zilizotuzwa hukaa. Malaika akasema, “Je, unaziona nyumba mbili kubwa, moja kulia kwako na nyingine kushoto kwako?Nikajibu, “Ndiyo, ninaona.”Malaika alisema kwamba alitaka kunionyesha nyumba hizo mbili haswa. Alisema, “Nyumba za upande wa kulia ni kwa wale waliokuwa wachungaji duniani. Makao ya kushoto ni ya wale waliokuwa wazee wa kanisa duniani.”
 
 Tulipofika mbele ya nyumba hizo mbili, nikawaona wakiwa wacheshi.. Tulipofungua mlango na kuingia, Taya langu lilishuka mawazo yangu ya kwanza yalikuwa, ‘banda la kuku.’ Badala ya maelfu ya kuku wanaoishi kwenye banda lao, niliona nafsi. Malaika walinishauri niangalie kwa makini sana kwa sababu ningewatambua baadhi ya wachungaji waliokuwa maarufu huku duniani. Kweli nilitambua wachungaji wengi kutoka kwa historia.
 
 Nilimchagua mchungaji mmoja na kumuuliza malaika, “Ninamfahamu yule kasisi wa Korea! Ninajua jinsi alivyokuwa maarufu na kazi aliyokuwa amemfanyia Bwana. Kwa nini yuko hapa? Sielewi." Malaika wakajibu, “Hakuwahi kutoa vifaa vyovyote vya ujenzi kwa ajili ya nyumba yake.” Hii ndiyo sababu anaishi katika nyumba ya jamii.” Niliuliza kwa udadisi, “Hii ilifanyikaje? Kwa nini hakuwa na nyenzo yoyote? Malaika akajibu, “Alipokuwa mchungaji akitekeleza majukumu yake kama mchungaji, alipenda kusifiwa na watu. Alipenda kuheshimiwa. Alipenda kuhudumiwa. 
 

Hakukuwa na dhabihu na utumwa kwa upande wake.” Mchungaji huyu aliheshimiwa sana huko Korea na ni nguli(icon) kwenye historia ya Kikristo ya Kikorea. Lakini hakuwa na thawabu kubwa mbinguni !!. Mchungaji, tafadhali sikiliza! Inabidi uwaongoze watu kwa zaidi ya ibada za jumapili asubuhi. Lazima uwatembelee majumbani mwao. Lazima uwatunze maskini, viwete na wazee. Wachungaji ambao wametumikia bila kutoa maisha yao na kupenda kuheshimiwa hawana thawabu mbinguni. Baada ya kushuhudia tukio hili mbinguni na baada ya kurudi duniani, mara moja nilitoa mali yangu yote ikiwa ni pamoja na magari yangu matano ya kifahari. Maisha yetu ni ya kitambo tu. Katika Biblia, maisha ya wastani ni takriban miaka 70 hadi 80.Mungu pekee ndiye anayejua ni lini mtu atakufa. Mtu yeyote anaweza kufa kabla ya umri wa miaka 70 au 80. Nilikuwa nimeamua kutoa kila kitu hata nguo zangu.
 
 Watu niliowaona wamepokea wokovu kwa aibu walikuwa wachungaji, wazee, mashemasi, na waamini walei. Kulikuwa na umati wa wazee na mashemasi katika nyumba ile tambarare iliyochakaa. Lakini bila shaka, bado ni bora kuliko kuzimu. Hata hivyo, kwa nini mtu yeyote bado angependa kuingia mbinguni kwa njia hiyo? Sitaishia mahali pa aibu. Hata nguo zao zilikuwa chakavu. Ikiwa mtu anasema hawezi kufika kanisani kwa sababu hawana nguo nzuri, basi lazima umpatie baadhi. Ikiwa mtu huyo anasema hana Biblia, lazima umtolee.
 
 Ikiwa mtu anasema hana miwani ya kusoma, lazima umpatie. Ni lazima utoe chochote unachoweza pia ili mtu huyu aweze kuongozwa kwa Bwana. Wale wanaoishi katika nyumba bora zaidi ni wale ambao walikuwa wamehubiri mara nyingi.” Ni matakwa gani ili Wakristo wapokee makao hayo mazuri mbinguni? Hebu tuijadili. Kwanza, tunapaswa kuinjilisha kwa watu wengi zaidi kadri iwezekanavyo.Niliuliza swali muhimu. Je, tunapaswa kueneza injili jinsi gani? Malaika akajibu na kusema, “Fikiria kwamba kuna mtu asiyeamini ambaye hamjui Bwana. Mara tu unapoamua kuinjilisha mtu huyo, vifaa vya ujenzi vya nyumba zako vitatolewa. 
 
Unapowaombea wokovu bila kukoma, vifaa vingi vya ujenzi vinatolewa. Lazima uendelee kuwachunguza, kuwatembelea na kuendelea na uinjilisti wako. Kisha malaika akanisindikiza hadi mahali ambapo watakatifu waliishi katika nyumba nzuri. Hapa ndipo walipoishi watakatifu waliohubiri sana. Mahali nilipochukuliwa nilihisi kama mbinguni katikati mwa jiji. Katika historia ya Kikristo, kuna watu wanne ambao wana nyumba kubwa na nzuri zaidi.
 
 Malaika alinionyesha nyumba ya mwinjilisti wa Marekani D.L. Moody. Nyumba ya pili niliyoiona ilikuwa nyumba ya Mchungaji wa Uingereza John Wesley na ya tatu ilikuwa mwinjilisti wa Kiitaliano. Nyumba ya nne ilikuwa nyumbani kwa Mwinjilisti wa Kikorea Mchungaji Choi, Gun Nung. Watu hawa wanne wana nyumba kubwa zaidi mbinguni. Malaika waliniambia kwamba hawa wanne walikuwa wametumia maisha yao yote kuhubiri injili kwa watu hata hadi wakati wa kufa kwao. Ndani ya waumini wa Korea, kulikuwa na mwamini mlei ambaye alikuwa na nyumba kubwa. Muumini huyu mlei alikuwa amejenga majengo mengi ya kanisa pamoja na mali zake zote alikuwa amewapa maskini magunia elfu tatu ya mchele. 
 
Alisaidia kwa siri maelfu ya wachungaji na viongozi kwa kutumia fedha zake. Alisaidia wanafunzi wanaosoma theolojia au shule ya biblia na masomo yao. Pia alikuwa amemchukua mchungaji (umri wa miaka 65) nyumbani kwake na kumtunza vizuri. Kanisa lake mwenyewe lilikuwa limemfukuza. Kisha ghafla, nikasikia malaika akipaza sauti, “Nyenzo/vifaa vinakuja!” Nilimuuliza malaika aliye kulia kwangu kuhusu nyenzo hizo. Alijibu, “Vifaa hivi ni vya shemasi kutoka kanisa dogo ambaye anatoka nchini. Kwa kweli, yeye hupokea vifaa kila siku. Ingawa yeye ni maskini, yeye huja kwenye ibada ya asubuhi kila siku, anawaombea washiriki 87 wa kanisa kila siku.
 
 Anapomaliza kusali, anasafisha kanisa.” Nilimsikia malaika mwingine akipiga kelele, “Utoaji maalum! Binti wa shemasi amempa mama yake pesa kidogo aliyokuwa nayo. Hata hivyo, shemasi hakuitumia yeye mwenyewe. Alinunua mayai matano na jozi mbili za soksi kwa mchungaji wa kanisa. Ingawa inaweza kuonekana kuwa sadaka ndogo, alikuwa ametoa vyote alivyokuwa navyo kwa siku hiyo. Hiki kilikuwa nyenzo maalum kwa ajili ya nyumba yake mbinguni.” Pili, wale ambao pia wana nyumba kubwa ni wale ambao wamejenga majengo ya kanisa au majengo mengine kwa ajili ya Ufalme wa MUNGU kwa mali zao.
 
 Mbinguni nilikutana pia na mzee anayeitwa Choi. Miongoni mwa wazee wote wa Korea na mashemasi walio mbinguni, alikuwa na nyumba nzuri zaidi. Nyumba yake ilikuwa juu sana kuliko jengo refu zaidi nchini Korea. Choi alikuwa amejenga makanisa mengi nchini Korea kwa utajiri wake. Nilimuuliza malaika, “Vipi kuhusu nyumba yangu? Je, iko katika mchakato wa kujengwa? Malaika akasema, Ndiyo.
Niliomba kuona nyumba yangu, Lakini waliniambia hairuhusiwi. Niliendelea kuomba. Baada ya kuomba kwa bidii, malaika walisema kwamba sasa Bwana ameruhusu. Tuliingia kwenye gari na kusafiri mbali sana hadi sehemu nyingine. Tulipokuwa tukiondoka, nilimuuliza malaika, “Hii itatuchukua muda gani?” Wakawawanasema kwamba ninazungumza sana. Hatimaye, baada ya muda fulani, malaika walinijulisha kwamba tumefika. Nilijawa na shauku kubwa. 
 
Nikauliza, “Nyumba yangu iko wapi?” Malaika akajibu, “Iko pale!” Lakini ilionekana kana kwamba mahali hapo palikuwa pazuri kwa bado haijakamilika kujengwa. Nililia, Nikieleza“Mngewezaje kunifanyia hivi? Hii inawezaje kutokea? Nyumba yangu inawezaje kuwa katika kutokamilika ?. Niliuza nyumba yangu pekee ili kujenga kanisa. Kanisa hili hatimaye lilikua na washiriki elfu tano. Niliandika vitabu vingi vilivyoongozwa na Roho Mtakatifu.
 
Kitabu kimoja kikawa kinauzwa zaidi. Kwa mapato ya vitabu, nilijenga shule za Kikristo. Shule hiyo ilizaa wachungaji 240. Wakati wa utumishi kama mkuu, nilikuwa nimetoa zaidi ya ufadhili wa masomo 400 kwa zaidi ya watoto 400 maskini. Nimewajengea wajane nyumba za kuishi. Hii yote iligharimu kiasi kikubwa cha pesa. Kwa hivyo hii inawezaje kuwa? Kwa nini nyumba yangu iko katika hali ya kuendelezwa ? Nimekasirika sana!” Malaika akajibu kwa ukali, “Hustahili kuishi katika makao mazuri kama haya mbinguni kwa sababu umeheshimiwa na watu mara nyingi. Kila wakati ulikuwa umejenga au umefanya kitu kizuri, ulisifiwa na watu. 
 
Uliheshimiwa hata na habari za kilimwengu. Kwa hiyo, kazi zenu zote ni bure.” Nilimuuliza malaika, “Kwa nini nina vyumba vidogo hivyo?” Hata hivyo, kwa kuwa tayari nilikuwa hapa, niliamua kuangalia nyumba yangu katika eneo la maendelezo. Nyumba yangu ilikuwa katikati ya nyumba zingine tatu. Nyumba yangu ilikuwa na safu tatu(3).
Nyumba hiyo ilikuwa na vyumba vingi vidogo kwenye orofa mbili za kwanza. Malaika akajibu, "Vyumba hivi ni vya wana wako na binti zako." "Nina watoto wanne tu" Hapana, si kwa ajili ya watoto wako wa udongo(yaani wa uzazi) bali ni kwa ajili ya wale uliowahubiria na kuokolewa.” Malaika alisema kwamba ilikuwa juu ya paa. 
 
Sikuipenda. Chumba changu hata hakijaisha. Kwa sauti ya hasira nilisema, “Ni ndogo sana! Kwa nini ni vigumu kumaliza?” Niliipenda! Nikauliza, “Chumba changu kikuu kiko wapi?” Malaika akajibu, “Hata wewe hujafa. Hatuwezi kumaliza nyumba au chumba chako kwa sababu hatujui ikiwa nyenzo zaidi zitatolewa. Unaelewa?" Tuliingia chumbani kwangu.
 
Niliona vyeti viwili vikining'inia ukutani. Nilikwenda kusoma kile kilichosema. Cheti cha kwanza kilichoelezwa nilipokuwa na umri wa miaka 18 nikiishi katika kituo cha watoto yatima. Siku ya Krismasi, nilikuwa nikirudi kwenye ibada ya asubuhi ya asubuhi. Nilikuwa nimemwona mzee mmoja akitetemeka barabarani. Nikavua koti langu na kumpa. Tendo hilo lilikuwa limenipa thawabu mbinguni. Cheti cha pili kilieleza tukio lilelile lakini kilikuwa cha kununua mkate kwa pesa kidogo niliyokuwa nayo kwa yule mzee. Kiasi sio suala. Tendo lazima liambatane na imani ya kweli.
 
** *NILITEMBELEA KUZIMU***
Malaika wawili(2) walinisindikiza hadi kuzimu. Wakasema, "Sasa utatembelea kuzimu." Hujui ukubwa wa kuzimu. Nilivyoiona nilipiga kelele, “Ni kubwa sana! Ni kubwa sana!” Hapa ndipo mahali ambapo roho zilizolaaniwa na kupokea laana ya milele zinawekwa.
Nilihisi kana kwamba mahali hapa palikuwa pakubwa mara elfu moja kuliko dunia. Nusu ya kuzimu ilikuwa na rangi nyekundu na nusu nyingine ilikuwa nyeusi sana. Niliwauliza malaika, “Kwa nini sehemu hii ni nyekundu?” Malaika wakajibu, “Je, hujui? Inawaka kiberiti.
 
 Nusu nyingine ni giza. Watu wakitenda dhambi na kuishia hapa, watateswa kutoka pande zote mbili.” “Mahali hapa ni pakubwa sana! Ni roho ngapi zilizo humu ndani?" Malaika akajibu, "Je, unaamini kuna mbingu na kuzimu?" “Ndiyo, ninaamini!” “Kuna wingi wa makanisa duniani na makanisa mengi yamejaa watu wengi.
Hata hivyo, wengi wao si wakristo wa kweli. Ni wahudumu wa kanisa tu. Makanisa ya kweli yataamini kabisa mbinguni na kuzimu. Maisha ya wakristo wengi yako katika machafuko kwa sababu hawaamini kabisa mbinguni na kuzimu. Nafsi moja(1) inapoingia mbinguni, roho elfu moja(1000) zilizolaaniwa huingia kuzimu. Kiwango cha uwiano wa mbinguni na kuzimu ni 1 kwa 1000." 
 
Chuo cha theolojia nilichokuwa nimesoma ni mojawapo ya shule kubwa zaidi za theolojia za kihafidhina nchini. Sikuamini katika mbingu na hadithi za kuzimu. Lakini sasa, mimi ndiye ninayeandika matukio kama haya ili kuwashuhudia wengine. Ingawa unaweza kuamini na kuwa Mkristo, ukiishi maisha yako kulingana na mapenzi ya mapepo, utaishia kuzimu.Mimi ni mchungaji wa Presbyterian. Mimi ni mzungumzaji maarufu.
 
Nimehitimu kutoka shule moja kubwa zaidi ya theolojia nchini Korea. Mahali pa kwanza waliponipeleka ni mahali pa salfa. Je, unaweza hata kufikiria jinsi moto wa kuzimu unavyoweza kuwa mkali? Hakuna mtu atakayeweza kuhimili joto kali. Kuzimu utasikia kauli tatu tu. Kwanza, ni joto sana na wanahisi kama kufa. Pili, wana kiu sana na wanahisi kufa. Tatu, utasikia wengi wakiomba maji. Ni ya milele! Watu wengi husema tuko huru katika Kristo na wanaishi maisha yao jinsi wanavyotamani.
Nikamwuliza yule malaika, “Wale waliomo humu ndani, wamefanya nini?” Malaika akajibu, "Kundi la kwanza ni la wasioamini." Wale ambao hawakuwa wamehubiria familia zao wenyewe lazima watubu! Malaika akaendelea, “Kundi la pili ni wale waliomwamini Yesu lakini hawakutubu dhambi zao.” Tunapaswa kutubu dhambi zetu na kukiri kwa Bwana.
 
Hatupaswi kutenda dhambi. Kuomba msamaha kwa midomo tu sio kutubu. Kwa moyo wa toba na wa dhati, lazima tutubu! Kisha niliwaona wachungaji, wazee, na mashemasi wengi kuzimu. Nilimuuliza malaika, “Ninawajua. Walikuwa wamemtumikia Mungu kwa uaminifu walipokuwa duniani. Walikuwa wamekufa wakati fulani uliopita. Sote tulifikiri walikuwa mbinguni pamoja na Mungu. Lakini sasa, ninawaona wote kuzimu na wanalia kwamba kuna joto sana! Sababu yao ni nini humu ndani?” Kulikuwa na idadi kubwa ya wachungaji, wazee, mashemasi na waamini walei wote. 
 
Wakiwa kwenye vitanda vyao vya kifo, walifikiri wamefanya kazi nzuri kwa hiyo hawakutubu mambo hayo. Hii ndiyo sababu walitupwa katika moto wa kuzimu.” Malaika akajibu, “Mchungaji Park Yong Gyu, mtu anaweza kuonekana kuwa mfuasi wa kweli wa Kristo kwa nje lakini Mungu anaujua moyo. Hawakuweka Jumapili Takatifu. Kwa kweli walipenda kupata pesa siku za Jumapili. Mashemasi na wazee wengi walikuwa wamekosoa mahubiri ya wachungaji wao. Hawakutoa zaka ipasavyo. Hawakuomba. 
 
Hawakuwa wamehubiri injili kwa watu hata kidogo. Wengi wa wazee hawa na mashemasi walikuwa wamewasumbua wachungaji wao na wangekuja kinyume na mamlaka yao. Walikuwa wameingilia kazi na shughuli za wachungaji wao. Kisha nikaona mfalme na mwana mfalme ambao walikuwa wamewatesa wakristo huko Korea kwanza. Mfalme na mkuu huyu aliwakata vichwa waumini wengi wa kwanza huko Korea. 
 
Waliwekwa katikati ambayo ilikuwa mahali pa moto zaidi kuliko zote. Pia nilimwona Hitler, Stalin, Mao Zedong, na mchungaji maarufu kutoka Korea kaskazini aitwaye Mchungaji Kang, na shujaa maarufu wa Kijapani, na mengi zaidi. Kisha tukafika mahali pa giza sana. Sikuweza kuona mahali ningekanyaga. Nilipaza sauti, “Malaika! Malaika! Ni giza sana! Ninawezaje kuona chochote?" Malaika walinipigapiga bega na kusema, “Subiri kidogo tu.” Ndani ya dakika chache, niliweza kuona. Niliona idadi isiyohesabika ya watu uchi.
 
 Wote walikuwa na wadudu wanaotambaa kwenye miili yao.
Hakuna hata inchi moja iliyosalia kwani miili yao yote ilikuwa imefunikwa kabisa na wadudu. Watu waliokuwa uchi walijaribu kuwafukuza wadudu hao huku wakisaga meno yao. Niliuliza, “Watu hawa walifanya nini walipokuwa wakiishi duniani?” “Ni wale ambao wamekosoa na kupinga mambo ya MUNGU. Hawakuwa waangalifu kwa yale waliyoambiana.”
Niliona mapepo yakitoboa na kuchoma matumbo ya watu kwa mundu. Vilio vyao vilikuwa havivumiliki kwangu.
 
 Nilimuuliza msindikizaji wangu, “Malaika, watu hawa walifanya nini walipokuwa wakiishi duniani? “Watu hawa walikuwa na kazi, nyumba, na familia lakini hawakuwa na cha kumtolea Mungu.
Hawakuwasaidia maskini, makanisa yao, au makusudi mengine ya kimungu. Walikuwa wabahili sana na wachoyo. Hata walipokutana na maskini, waliwapuuza na hawakujali. Walijijali wenyewe na familia zao tu. Walivaa vizuri, walilishwa, na walikuwa na maisha ya starehe.
 
Ndio maana matumbo yao yamechomwa kwa sababu matumbo yao yalijaa uchoyo. Lilikuwa ni tukio la kuogofya sana. Baada ya kushuhudia tukio kama hilo, niliporudi duniani, nilitoa pesa na mali zangu zote kwa wengine. Wokovu hauwezi kupatikana kwa pesa au mali. Ni kwa imani. Kuzimu ni mahali pabaya na pabaya. Ni mateso ya milele! Kisha nikaona vichwa vyao vimekatwa na msumeno mkali sana.
Nilimuuliza malaika kwa mara nyingine tena, “Watu hawa walifanya nini ili kustahili mateso ya kutisha namna hii?” Malaika akajibu, “Akili zao zilitolewa na Mungu kufikiria mema na yenye manufaa. Lakini watu hawa walikuwa wamefikiria mambo machafu. Walifikiria mambo ya ashiki(tamaa za ngono).”
 
Kilichofuata nikaona watu wakichomwa visu na kukatwa vipande vipande. Mtazamo huo ulikuwa wa kutisha. Nikauliza, “Vipi kuhusu watu hawa?” Walifanya nini hata kuteswa namna hiyo?” “Hawa walikuwa wazee na mashemasi ambao hawakutumikia makanisa yao. Kwa kweli, hawakutaka hata kufanya kazi au kutumikia! Mambo pekee ambayo walikuwa wamependa yalikuwa kupokea na kupokea kutoka kwa kundi.” 
 
Niliwaona wazee, mashemasi, na waamini walei wengine wakiteswa na mapepo. Mashetani walitoboa tundu kwenye ndimi zao na kuweka waya kupitia ndimi za wao kwa wao. Kisha mapepo yakawakokota watu kwa sime. Nikauliza tena, “Walifanya nini duniani?” Malaika akajibu, “Walikuwa wametenda aina nne tofauti za dhambi.
Kwanza, walikuwa wamewakosoa wachungaji wao. Wangezungumza mambo mabaya kuhusu wachungaji wao. Walikuwa nyuma wakiuma na kuwadhihaki wachungaji wao. " Nawasihi waliofanya vitendo hivyo WATUBU, WATUBU!! Malaika aliendelea, “Pili, walitukana kanisa kwa maneno yao. Walikuwa wamewasumbua Wakristo wengine hadi kufikia hatua ambayo hata waamini waliathiriwa na wakaacha kwenda kanisani na hata kuwafanya wengine waache kuamini. 
 
Walifanya yote waliyoweza ili kuwazuia Wakristo waaminifu wasifanye kazi ya Mungu. Waovu hao waliwafanya wengi waaminifu wajikwae. Mwisho, kuna wanandoa ambao walikunywa pombe na kuwatusi watu wa familia zao. Niliona mapepo yakiwatoboa wanaume na wanawake kwenye matumbo yao kwa msumari mkubwa sana wenye ncha kali. Nikauliza, “Walifanya nini?” Hawakuwa wametubu kamwe. “Hawa ni wanaume na wanawake ambao walikuwa wameishi pamoja lakini hawakuwa wameoana. 
 
Hawa wana hatia ya kutoa mimba kwani pia walipata ujauzito. Niliona kundi lingine la watu. Mashetani hao walikuwa wakipasua midomo yao kana kwamba mtu anapasua nyama au mboga. Niliuliza, “Kwa nini watu hawa wanateswa namna hiyo?” Malaika akasema, “Hawa ni wana, mabinti, wakwe zao na wakwe zao ambao walikuwa wamewajibu vibaya wazazi wao.
 
Walichopaswa kufanya ni kusema, ‘samahani’ badala ya kufanya mambo kuwa mabaya zaidi. Wengi wao walikuwa wametumia lugha ya matusi. Walikuwa wamewashambulia wazazi wao kwa lugha kali. Walikuwa waasi. Ndiyo maana midomo yao inakatwakatwa.”Ndugu, sisi sote tutakufa siku moja. Hatujui siku tutakufa.
Tafadhali jitayarishe. Kuwa tayari kwenda mbinguni. Tafadhali sameheaneni mara kwa mara kadri inavyohitajika.Tubu kwa toba ya kweli na ufanye hivyo siku zote.Ndugu zangu wapendwa, nilikuwa napuuza shuhuda hizo. Nilikuwa mchungaji wa Kipresbiteri ambaye alipuuza mambo kama hayo. Lakini sasa, lazima nishuhudie na nishuhudie kwako kile nilichoona.Tafadhali usisite kuishi maisha matakatifu. 
 
Tafadhali epuka adhabu na hukumu mbaya. Okoka! Msiishi kwa ajili ya miili yenu bali mtiini Ufalme wa Mungu. Tafadhali ombea wale wasiomjua Yesu. Kuinjilisha na kuzaa matunda. Tafadhali omba mapema asubuhi na uitakase Jumapili kuwa Takatifu. Tafadhali toa zaka kwa Bwana ipasavyo. Jikusanyieni thawabu zenu mbinguni na sio duniani. Nakuombea na kukubariki katika Jina la YESU!Kumbuka KUSHIRIKISHA wengine ujumbe huu : ubarikiwe!.

USHUHUDA WA MTOTO WA MIAKA 12 ALIVYOCHUKULIWA NA YESUKRISTO NA KUPELEKWA KUONYESHWA MBINGUNI NA KUZIMU.

Laura wamna(lala) ni mtoto wa miaka kumi na miwili (12), kutoka nchini indonesia.Tangu akiwa mtoto mdogo sana alikuwa anatamani sana akutane naye YESUKRISTO ana kwa ana.

Laura wamna anafahamika kwa jina lingine ambalo ni LALA sehemu moja akishuhudia alisema “ROHO wa MUNGU alinijia akanichukua mimi katika roho kukutana na YESUKRISTO”.Anaeleza jinsi ilivyokuwa  mpaka alivyochukuliwa na YESUKRISTO, alichokiona ni ukweli hakuna kilichopungua au kuongezwa.Tafadhali unaposoma ushuhuda huu omba ROHO mtakatifu akupe hekima yake na uelewa hata kabla hujasoma ushuhuda huu.

YESUKRISTO  ALIVYONICHUKUA  KUNINIONYESHA  MBINGUNI
·        YESUKRISTO alivyomtembelea LALA siku ya kwanza:Ilikuwa ni kipindi cha kusifu na kuabudu mikono yangu illikuwa imeinuliwa juu yenyewe, na nikamwambia mama yangu: “Mama, siwezi kushusha mikono yangu chini,na ilikuwa imeendelea kuinuliwa juu.Nikawaona malaika wengi ndani ya kile chumba, na ghafla nikaona mwanga mkali sana na unapotoka mwanga ule, kulikuwa na sauti ya BWANA ikisema nami.

Bwana YESUKRISTO aeleza juu ya kifo cha kaka wa LALA:BWANA akasema kutakuwa na kifo cha ndugu yangu wa karibu sana akazidi kusema akaniambia “Nenda kamwambie kaka yako wa karibu, mwambie anatakiwa anirudie MIMI , Kwa kuwa bado nina REHEMA kwa ajili yake, Kwa sababu maisha yake aliyokuwa akiyaishi yalikuwa mbali NAMI.” Kaka yangu alikuwa ana matatizo na alikuwa mzigomkubwa katika familia yetu.

·        YESUKRISTO alivyonitembelea siku ya pili:
Siku ya pili BWANA YESU aliniambia “utafaulu mitihani yako tena kwa daraja zuri”.Kipindi ambacho mimi na mama tulikuwa tunaabudu MUNGU, Ghafla malaika akaja akaitwa roho yangu tukaenda naye juu mpaka juu ya mbwamba naye malaika kanionyesha baadhi ya miji nayo ni Nabire, Serui, Biak, Manokwari.Malaika akaongea nami akisema “MUNGU kakwambia uende usimame katika hiyo miji na uhubiri ujumbe wa BWANA  ,wanatakiwa WATUBU kwa sababu “HAKUNA  MUDA  YESUKRISTO AKUJA HARAKA SANA””.Nilimuuliza yule malaika wewe ni nani ?,Malaika akanijibu “mimi naitwa  Gabriel”, Malaika wa BWANA .Ndipo aliponirudisha roho yangu kwenye mwili wangu.

·        Mauti ilivyozunguka watu:Tarehe 2o machi ,Nilipokuwa katika safari ya kutoka mji wa Abe to Entrop, Nikafikamji wa  Kotaraja nilikuwa kwemye taxi ambapo malaika akanichukua tukaenda juu ya jiji la Jayapura.

Malaika akaniambia “angalia”, Nilipotazama nikaona watu wengi wamesimama, Wamezaa nguo nyeusi zilizo wafunika kutoka kichwani mpaka miguuni na macho yao ni meusi na kuna moto ndani yao.
Niliwaona kila mahali hospitalini ,pembezoni mwa barabara,katikati mwa mitaa, masokoni, majumbani walikuwa kila sehemu.Niliona mikononi wameshika rato kubwa,Nikamuuliza malaika “hawa ni wakina nani?”, Akanijibu hao ni “malaika wa mauti”.

Tulipokuwa tunaruka kiroho juu ya mji wa Entrope, “Niliona makundi ya vijana wadogo wakinywa pombe mitaani, nilijawa na huzuni kwa sababu mauti ilikuwa imewazunguka kila sehemu”.
Malaika akaniambia “Lala, kama kuna kitu kimetokea na hauwi huru nacho., unaweza itia majina mawili nayo ni damu ya YESUKRISTO na kwa jina la YESUKRISTO kwa sababu jina hili lina nguvu sana.”.

Malaika kanichukua tukapaa juu ya mawingu nami nikazidi kuona dunia chini ikiwa ndogo na ndogo sana.Tulivyokuwa tunazidi kwenda  juu kuna sehemu tulipita ilikuwa nyembamba yenye giza na yakutisha.

Niliogopa lakini malaika alinishikilia tukafika nikaona mwanga na ilikuwa mbinguni, Mimi na malaika tulifika getini kulikuwa na malaika walinzi wawili mbele ya geti la mbinguni, Geti la mbinguni limepambwa kwa lulu nzuri za kung`aa ndipo lilipofunguka na wote wawili tukaingia tukawa tunatembea katika bustani.

Kulikuwa kuna mlango uliofunguka na ndani nikaona meza ndefu imepangwa vizuri inaonyesha kwamba si muda kutakuwa na sherehe(Ushirika mtakatifu/Holy communion), Kuna malaika waliosimama nyuma ya kila kiti, kila malaika ana tarumbeta mkononi mwake.Inaonekana kama vile wanaenda kupiga tarumbeta mapema.

Nikaendelea kutembea na katika bustani niliona miti mizuri sana,matunda mbali mbali mazuri, nikaona maua mazuri sana, Malaika Gabriel akaja akaniambaia “muda wako wakukaa hapa umeisha unabidi urudi” nami nikamjibu “ninafuraha na amani kukaa hapa sipendi kurudi”.Ghafla sauti ikatoka kutoka kwenye kiti cha Enzi ambako kulikuwa na mwanga na utukufu ikisikika “Lala ,unatakiwa urudi sasa”.Malaika Gabriel kanisindikiza akanirudisha.

Kutoka juu naliangalia na kuiona ile taxi nyekundu niliyekuwa nimeipanda mwanzo ,ilikuwa ikienda ofisi ya serikali ya mji wa Entrope.Malaika akairudisha roho yangu kwenye mwili wangu nikaamka nikasema “Halleluya!”.

Abiria ambao walikuwa pamoja nami kwenye hiyo taxi walishangaa na kupigwa na butwaa, Wakiniuliza “Dada, je ni mzima ?”.Nilishangazwa sana kwa sababu nilijikuta nikining`inia kwenye bega la abiria mmoja, naye alikinichuwa na mafuta kwenye pua kwa kuwa walidhania nimezimia.Nalisimamisha taxi pale nilipofika nyumbani.

Ilipofika saa11 usiku nilipokuwa nimelala, Malaika akanijia kunipeleka kwa Bwana, Tukaingia katika geti la mbinguni, Na nikaona mtu amesimama naye amevaa kamba ndefu nyeupe.Akanionyesha mikono yake kwangu, Nami nikatembea kufika karibu naye, nikajua kuwa ni YESUKRISTO akanichukua tukatembea wote mbinguni.Mbinguni ni pazuri sana na kuna kila aina ya maua ambayo sijawahi yaona duniani.

Kila kitu kipo pale , moyo wangu ulifarijika sana na kuwa na amani isiyokuwa ya kawaida,kuna miti ya vivuli,itoayo matunda na kwa uwazi kabisa kulikuwa kuna mto.Bwana YESUKRISTO akaniambia “Lala, utajaribu kuweka miguu yako kwenye maji ?,”Nami nikaichovya kwenye maji.YESUKRISTO kaniambia tena “unaweza kunywa maji haya”.

Nilipokunywa yale maji nikajisikia amani katika moyo isiyokuwa ya kawaida.YESUKRISTO aniambia “waweza kuzamisha hata kichwa chako humu kwenye maji na bado ukawa unauwezo wa kuhema ndani mwa maji haya”.
Alichokisema YESUKRISTO  kilikuwa ni kweli kabisa.Kulikuwa na samaki wengi wakiogelea karibu yangu, Nikamwambia YESUKRISTO “Nilipokuwa duniani sikuweza kukamata samaki kwa kuwa kule samaki wanakimbia ukitaka kuwakamata ”.YESUKRISTO akaniambia “Samaki wa huku wanaweza kuongea na wewe, Lala !”.

Baada ya muda nikamuuliza YESUKRISTO “Wawezaje kuona dhambi wanazozitenda  watu dunia nzima na huku dunia ni kubwa sana, waona je?”.YESUKRISTO kaniambia “njoo pamoja nami huku.”nikaenda akanionyesha kuna kioo kikubwa na nikaona dunia kuwa ni ndogo.

Nikaweza kuona watu wanaofanya dhambi nilishangazwa kuomuona mtu ninayemjua nikamwambia YESUKRISTO , “Bwana, naweza kuona yote chini” mama na baba walikuwa wamelala kitandani.Naye YESUKRISTO akanijibu “Ndio, na kuna malaika amesimama katika chumba chako.”
Mimi na Bwana YESUKRISTO tukatembea tena, kulikuwa na chumba ambacho malaika wawili(2) walikuwa wamesimama hapo nje.Kulikuwa na kitabu kikubwa mezani, na nikamuuliza Bwana, “MUNGU, kitabu cha aina gani hiki ?”, YESUKRISTO akanijibu, “Hiki ni kitabu cha uzima”,Nikamuuliza tena “naweza kuona ndani yake ?”, Bwana YESUKRISTO kaniambia “Ndio, unaweza”.

Na hao malaika wawili (2) walikuwa wako tayari kufungua kile kitabu kurasa baada ya kurasa, Kwenye ukurasa wa kwanza nikaona  moja ya majina ya familia ninayoijua, Nikaona tena kuna jina la kaka yangu nikamwambia YESUKRISTO  “Bwana, hili ni jina la kaka yangu” na Bwana akajibu “Ndio, ninayajua maisha yake na sasa yupo humu akimsifu Bwana”.

Malaika akanifungulia ukurasa unaofuata nikaona jina la mtu ninayemjua tena nikamwambia YESUKRISTO “Huyu ni mjomba wangu”.Naye Bwana akanijibu “Ndio , yuko hapa ” .Nikamkumbatia YESUKRISTO huku nikilia.
Tukaendelea kutembea na YESUKRISTO kwenye bustani nikaona watu wawili(2) wakinijia mmoja anaonekana kama anamiaka 18 au 19 hivii,na mwingine kama ana miaka miwili(2) akanikimbilia akanikumbatia nikaona kama amenipita kwa kuwa tulikuwa wote katika roho.

Huyu aliye mkubwa wa kama miaka 18 au 19 alikuwa anafanana na mama yangu yaani walikuwa kama mapacha na mama yangu kwa jinsi alivyofanana naye,  Ndipo nikakumbuka kuwa mama aliwahi niambia ana kaka yake ambaye alikufa nilivyokuwa mdogo sana,Nikwa nimemjua atakua ndiye nao wote wakaenda katika vyumba vyao.

Nikaona maua mazuri nikawa namuuliza Bwana , “Je naweza kuchuma ua hili ?,ningependa kumpa mama yangu kwa kuwa mama yangu anapenda maua” .YESUKRISTO akanijibu “Muda haujafika bado wa wewe kuchukua maua na matunda kutoka sehemu hii mwanangu !”.

Tukawa tunaendelea kutembea na YESUKRISTO nikaona nyumba ambayo mlango wake uko wazi, nikamuuliza YESUKRISTO kama naweza ingia humo,Bwana akanijibu “ndio ,waweza kuingia”.
Nilipofika mbele ya mlango wa nyumba, sikuingia ndani kwa sababu nilikuwa nashangaa sakafu ya dhahabu.Nikamwambia Bwana “MUNGU waooh !!!, ..chini pazuri sana hivi, duniani dhahabu ni ghali sana”. Naye YESUKRISTO alikuwa akibasamu na akasema “Hii ni nyumba yako ,na kuna baadhi ya nyumba zinazofanana na hii.”

Nikamuuliza YESUKRISTO “Bwana ninaweza kwenda nyumba ingine ?”.Bwana akanijibu “ nyumba ambazo milango imefungwa , ni za watu wengine”.YESUKRISTO akaniambia “Nifuate mimi”.

YESUKRISTO ALIVYONIPELEKA KOUNA KUZIMU.
Bwana YESUKRISTO alinishika wote tukaenda njia pana.Nikaanza kuhisi harufu mbaya kwa kadiri tunavyozidi kwenda nikajisikia hewa inakuwa ya moto.Kwa mbali nikaona pepo lenye miguu mitatu amebeba mikuki mitatu iliyoshikana na alipo muona YESUKRISTO akampigia magoti.

Tukaendelea kwenda mimi na Bwana YESUKRISTO huku akiniruhusu niangalie kwa undani zaidi ambako kuna watu walikuwa wakiteswa na shetani.Shetani alikuwa akiwatesa mpaka miili yao inabaki kuwa vipande vipande lakini hawafi.

·        WAZINZI:
Nikaona kitabu juu yake kimeandikwa “uzinzi”.Nikaona watu uchi wakiwa kwenye moto.Walipomuona YESUKRISTO wakaanza kumuita “Baba, Baba” lakini YESUKRISTO hakuwatazama.

·        Watumishi wa MUNGU:
Nilivyozidi  kuangalia nikagundua kuna watumishi wa MUNGU.Ndipo nikamuuliza YESUKRISTO, “Bwana !, Kwa nini kuna mtumishi wa MUNGU hapa kuzimu ?”.YESUKRISTO kanijibu kuniambia “Nilimchagua yeye lakini haku utoa ujumbe wangu”.

Ndipo yule mtumishi alipomuona YESUKRISTO akamwambia “Baba Baba, tafadhali niondoe hapa japo kwa dakika moja, nataka kutubu”.Bwana akamjibu “umechelewa ,akasema sasa namtumia binti huyu akinionyeshea kidole “mimi(lala)” kama mmoja wa watumishi wangu”.

Nikaona watu wengi wakiteswa, YESUKRISTO akaniambia mimi “hawa watu hawakuwa waaminifu kutoa fungu la kumi(zaka)”.
Nikaona kundi kubwa la vijana wadogo ambao walikuwa wanacheza muziki kwenye misumari, Kama muziki huo wa rock ukisikika basi wao wanatakiwa kuruka kwa haraka zaidi na hawakuruhusiwa kusimama hata muda kidogo.Kama wakisimama, shetani anakuja kuwatesa sana.

Ndipo tukarudi tukatoka kwenye njia pana na kuingia mbinguni.Tulivyofika mbinguni , Bwana YESUKRISTO kaniambia, “Lala, Yote uliyoyaona ukawaambie watu wangu”.Bwana YESUKRISTO akanichukua na akasema, “Lala, umesalimisha maisha yako Kwangu, unatakiwa ubatizwe mwezi machi 25 na mtumishi wangu Ronald, naweka amana kwake ili uweze kuandika kitabu chako”.

YESUKRISTO kamuangalia malaika Gabrieli na Gabrieli kapiga magoti kuabdu chini ya miguu ya Bwana YESUKRISTO.YESUKRISTO kamwambia malaika Gabrieli “Mrudishe mnangu.”

Gabrieli akanichukua na akatembea nami nje ya geti nikamwuona malaika mwingine akawa anaongea na Gabrieli kwa lugha ambayo nilikuwa siielewi, lakini Gabrieli alinionyeshea mimi na kuangalia kweye kiti cha enzi cha Baba MUNGU ,alikuwa malaika maiko naye YESUKRISTO akatutazama ,malaika maiko akapiga magoti na kumruhusu Gabrieli na mimi tuendelee na safari yetu.

Tulipokuwa niani tunarudi ,Gabrieli alniuliza “Ulikuwa unaongea nini na Baba?” .Na nikamjibu , “Kuna vitu vingi ambavyo YESUKRISTO ameongea nami”.Nikamuuliza malaika Gabrieli “Unafanya nini mbinguni ?”.Malaika akanijibu “Ni mlinzi wa Bwana YESUKRISTO, Chochote ambacho Bwana YESUKRISTO ananiagiza kukifanya ndipo nakifanya chote”.

Tulipokuwa tumefika karibu na nyumbani takatembea nikaona malaika wa vifo wamesimama pembezoni mwa barabara kushoto na kulia.Nilipofika nikaona mbele ya nyumba kuna malaika wa mlinzi wa BWANA.
Malaika wa kifo alikuwa anatamani sana kuingia nyumbani lakini hakuweza kwa sababu kulikuwa na malaika wawili(2) walinzi wa Bwana walikuwa nyumbani kwetu.Malaika wa mauti alitaka kuingia mara ya pili akatupwa nje ,akaanguka na kupotea kama vumbi.

Gabrieli kanisindikiza mpaka kwenye chumbani kwangu ndipo roho yangu ikarejea na kuingia katika mwili wangu nami nikarejea katika shughuli zangu za kawaida.
Alhamisi ,Machi 22.Tulikuwa na ibada nyumbani na baadhi ya watu wakanisani kwetu, Ndipo malaika Gabrieli alipokuja kunichukua kunipeleka kwa YESUKRISTO.YESUKRISTO alinionyesha mji ninaotakiwa kwenda.Aliniambia nikatoe ujumbe wake kwenye kanisa la Katoliki lililopo Wamena.

Ijumaa.machi 23.Malaika akaja kunichukua kunipeleka kwa Bwana.YESUKRISTO katoa ujumbe maalumu kwa kanisa lililopo kijijini “Harapan” na akasema “Kaliambie kanisa ,wasiwewanachelewa sana ibada.Kwa wale ambao mara zote wanachelewa hao hawatakuwa sehemu ya ufalme wa MUNGU.

Ibada inapoanza hatakiwi yeyote kubakia nje  ya kanisa akazidi kuniambaia waambie wamama wenye watoto ambao bado ni wachanga wanatakiwa kukaa ndani ya kanisa ili kusikiliza NENO la MUNGU.Asiwepo wakukaa nje hata kama kanisa limejaa wanaweza kukaa chini wasikilize NENO LANGU sio shida, kila mtu aheshimu NENO LANGU.

Siku hiyo hiyo tuliomaliza “maombi ya kufunga”,Nikatoa ujumbe wa Bwana YESUKRISTO kwa walimu wa shule ya jumapili(Sunday school) ,nikaanza kurudi nyumbani kutoka kanisani.

Malaika wa Bwana akanijia njiani na kuniambia “asante lala umeutoa ujumbe wa Bwana kwa walimu wa shule ya jumapili”.Akaongea nami “Jumaili utoe ujumbe kwa waumini kanisani.Utatakiwa kutoa ujumbe si kwa kanisa tuu na familia, lakini pia unatakiwa utoe ujumbe kwa dini zingine pia wadudha,uisilam, uhindizim na kadhaliaka.

Wao pia wanatakiwa kupokea wokovu, toa ujumbe mapema kwa kadiri uwezavyo kwa sababu nitakuchukua kukupeleka katika miji mingine.”(yohana 14,6).
Ilivyofika saa moja jioni ,Malaika wa Bwana akaja kunichukua na kunipeleka kwa Bwana, Bwana YESUKRISTO akasema nami “Lala ,haraka, haraka ,haraka kimbia na uwaambie watu wangu ,Muda wangu umekaribia kuisha!” .
Na Bwana YESUKRISTO akanionyesha ,muda wa mbinguni .Nikaona mkono mfupi umeonyeshea kwenye namba na mkono mrefu uko karibu nao sana ingawa sikuweza kuona namba katika saa.
Bwana YESUKRISTO kaniambia, “Lala, kimbia karaka nautume ujumbe kwa watu wangu,Muda wangu umekaribia kuisha”.YESUKRISTO kaniambia tena “Lala, hakuna malaika aliwahi kuona muda mbinguni.Nakuruhusu wewe kuona muda wa mbinguni ili uende kutoa kwa haraka ujumbe wangu”.

Majira ya saa 2:30:-Malaika kanijia na kunichukua kwenda kwa Bwana ,Bwana YESUKRISTO tena akanionyesha jinsi muda wa mbinguni ulivyobaki mfupi sana.Bwana YESUKRISTO kaniambia “Waambie watu wa darasani kwako, walimu wako, majirani zako na yeyote yule unatekutana naye.Waambie watubu na kunirudia mimi.”

Jumamosi, mach 24-saa 7;-Nilikuwa na mama na shangazi yangu.Tulikuwa katika nyumba ya familia ya Wilson Sentani.Kipindi shangazi yangu alipokuwa akiomba kwa ajili ya familia ya Wilson, na nilipolala chumbani nikamuona malaika kaja, Niliweza kumuona malaika kwa sababu roho yangu ilikuwa nje ya mwili na kukaa kwenye kitanda.

Nikamwita malaika kuingia katika chumba lakini malaika alikuwa amesimama nje ya chumba na nikamwita tena ,na malaika akanijibu “siwezi kuingia chumbani, (akamnyooshea kidole shangazi yangu),mtumishi anapoongea na Baba ,hivyo nimi nasubiri mpakaamalize kusoma aseme ameni”.Shangazi yangu alivyo maliza kuomba naye akaja.

Alinichukua na kunipeleka kwa YESUKRISTO naye Bwana akanipa ujumbe wakuja kuwaambia watu, siku ingine mnamo saa 6 usiku ,Nilikuwa nikijiona mwili wangu mzito sana , kwa sababu malaika alitaka kuja kunichukua , lakini mama yangu alizidi kuniambia niandae nguo zangu tayari kwa ajili ya ibada ya kesho.

Nilipokuwa nimelala, malaika akaja na kunichukua kwenda kwa Bwana.Bwana  YESUKRISTO akaniambia “Lala, mwambie mama yako awe anakuruhusu ulale pindi unapojisikia mwili wako mzito sana, kwa sababu kuna jambo muhimu sana ambalo nataka kusema nawe.”

Akanihakikisha mara ya pili,YESUKRISTO akasema “Lala, kwa nini ?umesahau kutoa ujumbe niliokuambia uutoe,Unatakiwa ukumbuke kila nilichokwambia na uwaambie watu”.Nikasema “Bwana, tafadhali nisamehe mimi” naye Bwana YESUKRISTO akajibu “Nitarejesha kila kitu utavyoshuhudia”.

Jumapili, Machi 25, wakati wa asubuhi.-Kwa rehema za Bwana YESUKRISTO, Nilisimama na kutoa ushuhuda wote wa ujumbe wa Bwana YESUKRISTO kwenye kanisa la Barachiel.Baada ya kumaliza kuutoa ushuhuda,Nilijikuta nimebatizwa (kufa na kufufuka na YESKRISTO) na baada ya ibada kulikuwa kuna kikao cha kufanya uamsho.

Nami nilitakiwa kushiriki katika huduma hiyo ya uamsho nikamuona malaika kaja kunichukua kunipelaka kwake YESUKRISTO ,Bwana akaniambia “Waambie watumishi wangu waende katika huduma hiyo ya uamsho nami nitashuka na kuingilia kati kuleta usuluhisho”.

Kipindi bado nipo katika nyumba ya mchungaji ,Bwana alinionyesha shimo kubwa ambalo lilikuwa refu na lenye giza.Nikaona watu wengi wakivutwa kwenda kwenye hilo shimo,Nao walikuwa wakijitahidi kujizuia lakini wakishindwa na kuanguka mpaka kwenye shimo hilo.

Machi 26;Malaika kaja kunichukua tukaenda mpaka kwa Bwana YESUKRISTO naye Bwana kaniambia “Nitakutumia wewe kama mtumishi wangu mpaka nitakapo kuja, Kazi zote na majukumu yote nakupa wewe, hayajaisha bado, lakini nitazidi kukutumia wewe mpaka nitakapo kuja.”

Saa sita malaika kaja kunichukua kunipeleka kwa Bwana,Tena Bwana YESUKRISTO akanionyesha shimo kubwa lenye giza.YESUKRISTO akaongea nami “Shimo unaloliona  ni sehemu kwa ajili ya wasio waaminifu nao wataenda kwa mika mitatu na nusu( mika 3.5) miaka ya dhiki kuu(Ufunuo 13), Na huku kwa walio waamoinifu kwangu nitawachukua mpaka sehemu niliyo waandalia, mbali na macho ya joka.”

YESUKRISTO kaniambia “Lala, usipingane na mama yako, tena usiende kinyume na amri yangu ya 5,unatakiwa uwaheshimu mama yako na baba yako.”
Nilipomsikia akisema hivyo Bwana nilijisikia mwenye hatia na nikalia.Nikamuona YESUKRISTO akilia na akionekana mwenye huzuni. Niliona machozi yakitoka kwenye macho Yake.Bwana YESUKRISTO kaniambia “Lala usilie , ninataka unisikie na utii amri yangu ya tano(5)(uheshimu wazazi wako) hivyo uweze kuishi maisha marefu na yenye baraka.

Nataka nikutumie wewe kiajabu na kwa kushangaza futa miziki ya kidunia kutoka kwenye simu yako” .(yakobo 4:4).Akaniambia unatakiwa uwe mtaratibu na mkimya hata ukiwa shuleni,YESUKRISTO akaniambia “nitawezaje kukupa ujumbe kama wewe haujatulia mwenyewe.”

Nami nikamjibu “Bwana , siwezi kwa kuwa marafiki wanakuja na kunisumbua na hata kutakua nikacheze nao,Vipi kama nisipo enda shule si ndio itakua vyema ?”,Naye akajibu “Hapana, unatakiwa uende shule”.
Machi 27-04:30,Siku niliyokuwa na mtihani shuleni, Malaika alinichukua mpaka kwa Bwana YESUKRISTO naye akaniambia “ HAKUNA MUDA ZAIDI, unatakiwa uwape watu ujumbe wangu haraka sana”.

Katika ibada ya kuabudu jumapili  , kama kawaida malaika alinichukua mpaka kwa Bwana YESUKRISTO. Niliona YESU amesimama mbele ya geti akinisubiri mimi na nilipofika,YESUKRISTO kaniambia “Unatakiwa uende kule ile sehemu ya wamena mara moja na uwape ujumbe wangu, kuwa wanatakiwa WATUBU kwa sababu muda umekwisha.Unatakiwa uende Wamena”.

Bwana alikuwa akiongea huku uso wake ukiwa wenye huzuni na wenye kusinyaa huku akilia, Machozi yake yakidondoka pale kwenye meza ya kioo ambayo anaweza kuona kila kitu ambacho watu wanakifanya.

Nikamuuliza “ Bwana kwanini walia ?” .Hakunijibu swali langu na huku machozi yakizidi kumtoka nakudondoka kwenye meza nami nikayafuta machozi na kamba nyeupe nilioivaa, kila nilivyokuwa mbinguni nilikuwa mara zote navaa kamba nyeupe ambayo sijawi ivaa popote duniani.

Ndipo Bwana akaniambia huku machozi yakimtoka “Lala, waambie watu wangu haraka ,wanatakiwa warudi kwangu haraka, Muda umekwisha kabisa .”Bwana YESUKRISTO kasema tena, “Sitamani mtu yeyote apotee, lakini wote wakae katika ufalme wangu”.

MUNGU unaposoma ujumbe huu pia mshirikishe na mwingine (share),
Badilika na uanze kuishi kama MUNGU atakavyo hapo ndipo utakapo okoa maisha yako.
Ushuhuda wa Laura Wamna(LALA), dada wa miaka kumi na mbili (12) kutuka Indonesia.





Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...