Uchumba/Ndoa


Somo:Hatujijui kama yeye MUNGU anavyotujua!-part 1

Walengwa: couple/single

Neno:  “Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, . . . .  .” Mwanzo 1:26

Theme:Sababu kuu ya kuoa au kuolewa

“Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi MUNGU atawahukumia adhabu” Waebrania 13:4

MUNGU ndiye aliyetuumba sisi sote,yaani watu wote wale wanao mjua MUNGU na wasio mjua.Imeandikwa “Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini,
na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.” Mwanzo 1:26

Hivyo hatujijui kama yeye MUNGU aliotutengeneza, aliyetuumba anavyotujua!.Hatujui hata siku za maisha yetu kwa nguvu zetu bali ni kwa unabii utokao kwake MUNGU tena kwa mapenzi yake.

Imeandikwa “(Kwani sisi tu wa jana tu, wala hatujui neno, Kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli tu;)” Ayubu 8:9.
Yeye MUNGU anajua kila kitu juu yetu, anajua uwezo tulionao,anajua tuishi namna gani ndio itakuwa vyema zaidi,anajua kitu gani tusifanye kisije kikaharibu uumbaji wake juu yetu kwa namna yoyote ile.
MUNGU aliyetuumba anasema sii vyema mtu aishi pekee yake na akamfanyia msaidizi.
Imeandikwa“BWANA MUNGU akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.” Mwanzo 2:18
Ni nani  wakumpinga MUNGU yeye aliyetuumba  kwa kuwa yeye amesema sii vyema mtu kuishi pekee yake.
Hakuna mtu aliyejiumba ,hakuna hata mtu mmoja aliye jitengeneza.Na yule aliyetuumba anajua ni jinsi gani tunatakiwa tuwe mke na mume.

Katika maisha ya kawaida tuu,Mtu anayefinyanga (mfinyanzi) akitengeneza chungu cha udongo ,hata kile chungu kiende wapi yeye mfinyanzi akikiona tuu anakijua, tena kwa undani sana.
Atakijua na kukumbuka alitumia udongo gani ?,anajua  uwezo wa chungu hicho,kinaweza kufa ukikigonga na kitu kigumu,anajua aliweka mapambo gani ? na vyote katika chungu hicho yeye mfinyanzi anajua kwa sababu yeye ndiye aliyekifinyanga.

Je ? kama sisi wanadamu tunajua mambo yote hayo juu ya kile kitu tunacho kitengeneza,Si zaidi ajuavyo MUNGU juu yetu kwa kuwa YEYE ndio aliyotuumba.
Yeye anayetujua zaidi anatuambia si vyema mtu aishi pekee yake.Kwa hiyo kuna haja ya mtu kooa au kuolewa kwa kuwa yeye MUNGU anayetujua zaidi anatuambia kuwa sii vyema mtu kuishi pekee yake.
Hivyo BWANA asema mwanamke kuishi pasipo kuolewa sii vyema na mwanaume aishiye bila kuoa sii vyema.
Sababu ya mtu kuoa au kuolewa ni moja tuu kuwa yeye hajajiumba na aliyemuumba ambaye ni MUNGU anasema sii vyema mtu kuishi pekee yake.
“Kwa sababu hiyo ........................................................” Waefeso 5:31.
Andiko limeanza kwa kusema kwa sababu hiyo,sababu yenyewe ni “Kwasababu hatujijui sana na kiundani kama MUNGU aliyetuumba anavyotujua,na kwa agizo lake si vyema mtu aishi pekee yake..”

No comments :

Post a Comment

Andika maoni yako hapa !! ... You may comment here !!!

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...