SIRI ZA MBINGUNI NA KUZIMU-sehemu ya kwanza na Emmanueli Senayon

Jina langu ninaitwa Emmanueli Senayon;Nina umri wa miaka 18, kutokea nchini Naijeria.

NIMEKUTANA NA YESUKRISTO.
Mwaka 2012 mwezi Novemba, Nilikuwa mgonjwa sana na wazazi wangu wakanichukua na kunipeleka hospitalini.Daktari akasema damu yangu i chini sana na nilikuwa na kifua kikuu{TB}(tuberculosis).
Ilikuwa taarifa mbaya sana hasa kwa wazazi wangu  kwa kuwa hawakuweza kumudu gharama za kunihudumia pale hospitalini, hivyo wakanichukua na kunirudisha nyumbani bila matumaini yeyote.
Nilipokuwa kwenye kitanda nikipumzika, Nikaanza kuhisi kitu cha ajabu na mwili wangu wote ukazidi kuwa dhaifu isiyokuwa kawaida.Nikajikuta mwenyewe niko nje ya mwili katika chumba cheupe haswaa.YESUKRISTO akanitokea, Sura yake ilikuwa inang`aa na alikuwa mzuri sana lakini nikagundua hakuwa na furaha.Akanishika mkono wangu na kunichukua mimi hadi nje ya chumba hicho na nikajikuta nimesimama mbele ya enzi kubwa.

Nikamwona Baba MUNGU katika enzi yake.Sikuweza kuona sura yake ,mwili wake ulikuwa kama moto uwakao, amejaa nguvu na utukufu.Nikaona makundi ya malaika wakiwa na mavazi meupe mbele ya enzi, na walijaa utukufu.Wale malaika wamebeba vitabu kwenye mikono yao.Nikaona watu wasiohesabika mbele ya enzi[UFUNUO 20:11] nao walikuwa wakienda mmoja baada ya mwingine kupokea hukumu yao na kila mtu alipofika mbele ya enzi, malaika walifungua vitabu mikononi mwao na MUNGU ndiye anayehukumu huyo mtu.

Watu wengi waliosimama wakisikia MUNGU akiwaambia “ONDOKA KWANGU”.
MUNGU aliwahukumu na hasira kali na sauti yake ikasikika kwa mlio mkuu [EZEKIELI 43:8].Pale MUNGU anaposema “ONDOKA KWANGU”,Kulikuwa na kimbunga kikubwa kinachomzoa mtu huyo na kumtoa hapo.[MATHAYO 25:41].Watu wote waliokuwa mbele ya enzi walikuwa wakiogopa sana kusimama mbele za MUNGU.Wao malaika hawaiti jina la mtu yeyote lakini kila mtu anajua inapofikia zamu yake ya kupokea hukumu[2 wakorintho 5:10].Yeyote aliyefanya uovu alitwaliwa na kimbunga kwenda kwenye adhabu isiyo isha[Mathayo 25:46].

Kwa kuwa uko hai ,Bado una neema ya dhahabu kutubu kutoka kwenye dhambi zake na kuaha uovu wako.Hasira ya MUNGU ni kama moto uwakao[SEFANIA 2:1-3] na dunia ni bonde  la kufanya maamuzi[YOELI 3:14].Uamuzi wako uache uwe KRISTO;kabidhi maisha yako kwa YESUKRISTO na kuipuka hasira ya MUNGU.Haijalishi dhambi gani ulioifanya, YESU atakusamehe yote yote[HOSEA 14:4], [HABAKKUKI 2:13].

YESUKRISTO AKANIPELEKA KUZIMU YA MOTO
Ndipo YESUKRISTO akanitoa hapo na kunipeleka kuzimu iwakayo moto.Kuelekea kuzimu tulipitia handaki ambapo tulipotoka tuu kwenye hilo handaki tukawa tumefika sehemu ambayo ina giza kweli kweli.Ilikuwa ni sehemu yenye giza kubwa na sauti za kutisha za vilio na kutisha.

Nikauliza, ‘Bwana tuko wapi ?’ naye akasema, “huu ni ufalme wa shetani, kuzimu ya moto”.Kuzimu inatisha sana kuna giza zito.Niliona mapepo wengi ;walikuwa wakubwa na wabaya sana.Mapepo hayo yalikuwa yanafanya kazi kwa kasi sana bila ya kuchoka.[1 PETRO 5:8].Bwana akaniambia mimi , “wanapanga jinsi ya kuleta watu sehemu hii”.

Kuzimu ya moto iko kama ziwa, na kila mmoja ana sehemu yake katika kitengo tofauti tofauti.Kuna watu wengi kuzimu wako kwenye moto wanaomba nafasi ya sekunde, lakini hakuna kibali na haiwezekani.[MIKA 3:4].

Kitengo cha kwanza Bwana alichonionyesha nisehemu ambayo ni ya wachungaji walioikosa mbingu.Niliona wachungaji wengi wako kuzimu katika mashimo yao kuna kitu kamaubao watangazo ambako umeandikwa jina la huyo mchungaji,jina la hilo kanisa alilokuwa akilichunga jumuisha na sababu iliyopeleka kuzimu.Kila mchungaji alikuwa ana mapepo yaliyokuwa yanamtesa.Walikuwa wakilia na kuomba rehema kwa YESU, lakini YESU alilia na kuwaambia “nilipokuwa nikiwaonya ninyi hamkunisikiliza na sasa mpo katika sehemu hii.siwajui ninyi !”.[Mithali 1:24-31].
Ndipo Bwana akaniambia, “kuzimu imejiongeza na hakuna ajaye huku atayeweza kurudi tena”.[Mithali 2:19],[ Isaya 4:14].
Niliona kitu kikubwa na cha kushangaza sana ! “Watu wangu,tutawezaje kuikwepa kuzimu kama tukidharau wokovu mkuu?” [Waebrania 2:3].

MCHUNGAJI OSHOFFA
Nilimuona mtu akiwaka moto kuzimu, mapepo walikuwa wakimtesa kwa silaha zao na vifaa vyao.Mtu huyo alikuwa akiomba rehema na alilia kwa uchungu sana.

Nikamuuliza Bwana, “Huyu ni nani?”.Bwana akaniambia, “ni mchungaji oshoffa, muanzilishi wa makanisa ya ‘CELESTIA KANISA LA KRISTO’,KANISA LA VAZI JEUPE”.Bwana akaniambia siri ya mtu huyu; “alijiwekea agano na shetani kuwavuta watu kwa mafundisho ya giza, uponyaji kutumia mishushumaa, marashi na sabuni.Huwaambia watu watumie hivyo vitu na waende kuoga kwenye mito, na kuwadanganya kwa nguvu ya shetani”.

Bwana aliongeza “yeye alifundisha mafundisho ya uongo ili tuu ajulikane kama mtu mkubwa wa Mungu”.[Efeso 4:14] Bwana alisema, “NILIMUONYA YEYE LAKINI ALIKATAA”.
Bwana YESU alimwambia mtu huyu “SIKUJUI WEWE”,YESU alilia kama mtoto; huyu mtu alikataa msalaba wa KRISTO tuu kwa sababu ya umaarufu.Sasa yupo kuzimu akiomba rehema kwa Bwana kutokana na uovu aliokuwa nao.[ 2 Timotheo 2:12,19].
Nataka nikueleweshe kuwa haijalishi hali yeyote usiamini au mafundisho tofauti na kwa hayo “Hutaweza kujitetea mbele za Bwana”.[Tito 1:16],[Yeremia 23:24].Watu wengi wapo kuzimu kutokana na mafundisho yao.[Wafilipi 2:5].

YUDA ISKARIOTE.
Nikamuona mtu mwingine akiwa kuzimu;,mapepo yamemfanya alale juu ya kitu kama chuma ambayo ni mfano wa meza,Walikuwa wakimuumiza na aina za vifaa mbali mbali.Nikaona chuma kikubwa ambacho pepo anakitumia kumtesea na kukitumbukiza kupitia kwenye tumbo la huyo mtu.Kilikuwa kinapita kwenye tumbo na huyo mtu alikuwa akilia kwa uchungu sana.

Mara akatokea pepo ambaye alikuwa ana kisu kikubwa cha chuma mkononi mwake, akakata katikati ya kichwa cha mtu huyo, mapepo kumi walikusanyika ,kulikuwa na funza wengi na n`nge.Walikuwa wakiingilia kichwa cha mtu huyu na baadae kurejea tena.Mtu huyo alikuwa akilia zaidi kama upepo wa ziwa.Iliniuma mimi sana kuona hayo.Bwana akaniambia, “HUYO NI MMOJA WA WANAFUNZI WANGU, YUDA ISKARIOTE”.

Nikauliza mapepo sababu ya kumtesa  yeye kiasi hicho,na pepo akaniambia “Kama asinge mfichua mtu huyu wa Nuru(YESUKRISTO) kwa watu ili wamuue , basi kazi ya wokovu isingedhihirika”.Mapepo yalikuwa yakipiga kelele yakimwambia, “Kwa nini umemsaliti?”,aliendelea kumtesa.[Mathayo 10:4],[Mathayo 20:18].

Unatakiwa uwe makini kwa kile unachokifanya usimsaliti YESUKRISTO ! “Ole wake mtu yule ambaye amsaliti Mwana wa Adamu !”.[Mathayo 26:24].Wale ambao wamejifunza kutoka kwa Bwana na kuelewa Neno la MUNGU wanatakiwa waruhusu “neno la KRISTO kukaa ndani yao”.[Wakolosai 3:16-17].Kwa yule ambaye anarudi nyuma,Bwana anasema “ROHO YANGU HAINA FURAHA NAYE.”.[Waebrania 10:38].Kama wewe ni mtumishi wa MUNGU jichunguze mwenyewe na utoe kikwazo katika maisha yako.---MOTO WA KUZIMU UNATISHA KWELI.

MFALME AHABU NA YEZEBELI.
Bwana alinionyesha mtu aliyekuwa amekaa amefungwa kwenye kiti cha chuma.Hicho kiti kilikuwa cha moto sana na chekundu kama kaa.Ingawa alikuwa akipiga yowe kwa uchungu sana badomapepo yaliendelea kumtesa na mikuki wakiwa na hasira kali.Mtu huyo akaanza kumuomba YESU nafasi yakutoka kwenye moto.Nikajiuliza huyu anaweza kuwa nani, Bwana alijua mawazo yangu na kuniambia mimi “NI MFALME AHABU”.
Ghafla nikamuona mwanamke ambae mapepo yalikuwa yakimtesa sana.Walikuwa wakimpiga na kwa mikuki alipokuwa akilia na kupiga  kelele.Bwana akaniambia, “HUYO NI YEZEBELI,NABII WA UONGO AMBAO ALIKUWA AKIWASHAWISHI WATU KUMTENDA DHAMBI MUNGU”.[Ufunuo 2:20].
Unabidi uwe makini kwa sababu kuna manabii wengi wa uongo,  wanaofundisha mafundisho potofu ambao kwa hayo mafundisho wajiwekea utajiri wao wenyewe.Waanajiita wenyewe waokozi na kudanganya watu kwa uongo wa shetani.KAMA WAKIKATAA KUTUBU,WATAKUWA NA NAFASI YAO KUZIMU YA MOTO.[ 2Wathesalonike 1:8]

MTOTO WA MIAKA SITA(6).
Nilimuona mtoto mdogo akiwa kuzimu,mapepo yalikuwa yakimtesa huyo mtoto kwa mikuki,Huyo mtoto alipotuona sisi alilia na kuomba msaada ili atolewe motoni, lakini Bwana akasema “MIMI SIO MUNGU WA WASIOTII”.Huyo mtoto alikuwa jeuri sana alipokuwa duniani, alikuwa akisumbua wazazi wake kipindi mchungaji anapotoa Neno.Wazazi wake walipomsahihisha aliwafokea.Aliumwana na alipokufa ,sasa yupo kuzimu milele.Bwana akasema,”HAMNA MTOTO ASIYETII ATAKAYERITHI UFALME WA MUNGU”.[Waefeso 6:1-2].

REVEREND PATRICK R. COONEY
Bwana alinionyesha mimi mtu mmoja aliyekuwa kuzimu,alikuwa akifahamika kama PATRICK COONEY alipokuwa hapa duniani.Mapepo yalikuwa yanakata kata mwili wake kwa misumeno, mateso yalikuwa makali sana.Walikuwa wakimkejeli na kumcheka na kusa pekee alilokuwa nalo ni kutokana na mafundisho yake.Alipelekwa kuzimu kwa sababu ya kuinamia mara kwa mara [inayosemekana] SURA YA MTAKATIFU MARIA.[Kutoka 20:3-4].

Ni huzuni sana watu wengi wanaishia milele kuzimu kutokana na mambo kama haya.Nilikuwa na huzuni kubwa na Bwana akaniambia “KAMA KWELI UNAHUZUNI, UTAWAAMBIA ULICHOKIONA”.
Unatakiwa ufungue moyo wako na kusema “hapana” juu ya uongo wa shetani.Tunatakiwa tutoke kwenye mafundisho yenye kumfanya KRISTO atukatae sisi.[2 Wakorintho 6:14-18], USIINAMIE KUABUDU  MTAKATIFU MARIA TENA.

KITENGO CHA WENYE KUJIWEKA KIKAHABA.
Niliwaona watu wengi katika hiki kitengo,Bwana akanionyesha picha zo walivyokuwa duniani nao kwa sura walikuwa wazuri lakini sasa wapo kuzimu ni wabaya sana.Mapepo yalikuwa yakiwatesa kwa kutumia mikuki kuwapiga na kuwabana sehemu zao za siri, walikuwa wakilia na kutafuta wafe lakini ilishindikana.[Ufunuo 9:6]
YESU alilia, nao watu walikuwa wanamuomba BWANA awatoe, nao walikuwa wakiapa katika maisha yao watafanya mapenzi YAKE kama wakitolewa kwenye moto, Lakini Bwana hachezi au kutania na NENO lililotoka kwenye kinywa chake[Wakolosai 3:5-6].Imeshaandikwa kwenye NENO kuwa yeyote anayetenda uovu hata urithi ufalme wa MUNGU[1Wakorintho 6:9-10].

KITENGO CHA WALIOSIKIA KUHUSU KRISTO NA WAKAKATAA KUTUBU.
Kuna watu wengi kuzimu ambao walisikia habari za wokovu,lakini walikataa kutubu dhambi zao.Nao walidhani watakuja mbinguni kwa kazi za mili na damu yao, Tofauti na hayo sasa wameishia kuzimu inayowaka milele[ 1Wakorintho 15:50].

Walikuwa wakilia, lakini Bwana alisema “walipewa neema kubwa ya kutubu dhambi zao pindi walipokuwa duniani lakini walisema ‘kesho’ na kuzidi kesema kesho!,kesho!.b aadhi walisema ‘hakuna moto wa kuzimu’.baadhi yao waliwapiga watumishi wangu niliowatuma kwao, na sasa wapo kuzimu wakiomba nafasi ya pili.....siwajui ninyi”.[Mithali 1:24-28].
Bwana YESU akaniambia, “niliwaonyesha njia ya kuepuka moto wa kuzimu lakini walinichukia mimi na njia yangu na kuchagua maisha ya kufurahia dunia.hata niliwapa ofa  ya neema walipokuwa wakitaka kufa lakini lakini waliiharibu”.
Bwana akasema tena, “walinichukia mimi na kupenda kifo .........sio kifo tuu cha duniani bali pia adhabu ya milele ndani ya kuzimu”.[Mithali 8:35-36]
Tubu kutoka kwenye dhambi yako kwa kuwa kuzimu hakuna kutubu.Wale wote wanaokataa kutubu wanatupwa kwenye adhabu ya milele.[Ufunuo 21:8].
KITENGO CHA WAKRISTO WALIORUDI NYUMA.
Kulikuwa kuna mateso makali sana kwa wale waliorudi nyuma na kumwacha YESU, Mapepo yalikuwa yakikata ndimi zao, wakikata miili yao na kuwapiga kwa silaha zenye ncha kali.Walilia kwa uchungu sana, walikuwa wakijilaumu wao wenyewe wakisema “oh,kwa nini niligeuka nyuma?,Alinionya lakini sikusikia !”.Mapepo huwaambia “kaeni kimya!,Aliwapa ninyi neema lakini mkaichezea.Hutaweza kutoka huku,tutawatesa mpaka hukumu itapowekwa!” .......na wakaendelea kuwatesa[Ezekieli 18:24].Mapepo yalikuwa yakiwaambia “u wangu milele”.

Tafadhali sana kama umeokoka usijerudi ulimwengu, wote ambao ni waKristo kuna hatari kubwa ya kurudi nyuma na kumuacha Bwana.[2 Petro 2:20-22].

SHIMO LANGU MWENYEWE
Bwana alinionyesha shimo langu kuzimu.Nilipatwa na huzuni , lakin Bwana akaniambia, “KILA MTU DUNIANI ANA SHIMO LAKE HUKU MOTONI(kuzimu), NA KAZI YA MAPEPO NI KUHAKIKISHA ANAKULETA HUKU KUZIMU”.Unatakiwa uwe na uhakika kuwa hutaenda kwenye shimo hilo kwa sababu ni la moto sana, moto wake ni kama asidi.
ENZI YA SHETANI
Tukatoka hapo na Bwana akanichukua mpaka kwenye enzi ya shetani.Nikaona mapepo katika enzi hiyo wakubwa,warefu,wanene na wapana.shetani alikuwa amejificha na ghafla akaniangalia mimi.Akaniita jina langu ,“’Senayon, umekuja hapa kuona siri zetu.Sitakuruhusu umshirikishe yeyote siri zetu! ,Nita kuuwa wewe, naapa”.Na Bwana YESU akaniambia, “USIOGOPE,  MIMI NI MAISHA YAKO”.[Isaya 41:10-11].
Ndipo mda mwingine tukawa hatuonekani kwa shetani, na Bwana akaniambia mimi “VITU VYOTE HAVIONEKANI KWA SHETANI,SHETANI HAJUI VITU VYOTE LAKINI VITU VYOTE VIKOWAZI KWA MUNGU”.

Kwa mara ya kwanza siku amini hiki kwa sababu duniani wote tulikuaga tunajua shetani ni mwenye nguvu sana.Bwana naye akajua mawazo yangu na akanichukua nyuma kwenye enzi ya shetani.Nikagundua shetani hakujua kuwa tuko pale nyuma.Bwana akaniambia “ITA JINA LANGU” na nikaita kimya kimya “YESU!” na nguvu isiyokuwa ya kawaida ikatikisa kuzimu na shetani akaanguka chini kutoka kwenye enzi yake.Ndipo shetani alipogeuka nyuma na tukawa tumeonekana, shetani aliita jina langu kwa sauti “SENAYON” na Bwana akaniambia, “IJARIBU NGUVU ILIYO KATIKA JINA LANGU”.na nikaamuru shetani kufa kwa dakika tatu(3) kwa jina la YESU,Nguvu iliyotoka katika jina la YESU ikatoboa roho kama kitu kama ukuta na mwili wake wote aliouficha ukaanguka chini.[Wafilipi 2:9-11].Na mara baada ya dakika tatu(3),Bwana akaiachia roho yake naye shetani akarudi tena na ule mwili wake uliojificha.Alipoinuka tuu alitoa sauti akiwa na hasira kubwa sana na gadhabu.Nikaona mapepo mengi yakimkimbilia na kukusanyika wakiwa na mishale mikononi mwao.Na wote wakaja kinyume chetu, ndipo nikaona mbingu imefunguka na nikaona mshale haswaa,kiasi kwamba kwa mshale mmoja unaweza kuja kuharibu mishale yote ya shetani.
Nataka niwaambie kuna nguvu katika jina la YESU kwa jina lake kila goti litapigwa.[Wafilipi 2:9-11],[Marko 16:17-19], [Yohana 14:14], [Yohana 16:23].Kuna nguvu katika jina la YESU,liite kwa imani na mapepo watakimbia kutoka kwako; lakini utapoita jina la YESU bila kutubu utakuwa kwenye hatari.

MALAIKA WALIO ANGUKA
Bwana alinichukua mpaka kwenye ukumbi mkubwa kuzimu, niliona mapepo waliofungwa chini kwenye siti.Bwana akaniambia hao ni malaika walioanguka,nika muuliza sababu kwa nini wamefungwa.Bwana akaniambia, “WANANGUVU SANA NA KAMA WAKIACHILIWA, WATALETA ROHO NYINGI KUZIMU, WANANGUVU SANA”. Bwana akaniambia “WATA ACHILIWA BAADA YA UNYAKUO KUSUMBUA DUNIA NA KUTESA WATU KWA AJILI YA ALAMA YA MNYAMA”.[ 2Petro 2:4].
Mmoja wa mapepo hayo akaniambia “Senayon, Bwana amekuonyesha ushuhuda mzuri lakini kama nikikukuta wewe duniani, nitakuuwa”.
Tulipotoka mahali pale nikagundua kunakitu kimeshika nguo yangu.Nilipotazama nyuma, nikaona pepo ndiyo aliye nishika nguo yangu na alitokea chini.Kwa sababu ya Nuru ya Kristo hakuweza kuja karibu yangu zaidi.

Bwana akaniambia “NI KUHANI MKUU WA SHETANI[Beelzebuli][Mathayo 12:24].Pepo aliniambia “hatuta kuruhusu kushuhudia na kushirikisha wengine na hutafichua siri zetu, tutaku ua”.
Bwana akaniambia “MWAMURU !”.Kwa hiyo nikamuamuru kwa jina la YESU kuanguka ndipo upepo mkali ukaja ukampiga mpaka chini na akarudi sehemu yake.Bwana pia akanionyesha roho za usumbufu, na jinsi wanavyonitumia silaha zao ovu za kishetani, lakini Bwana akarudisha zaidi kwao, na wakakimbia.[Zaburi 91:1].Kwa kadiri ya muda Bwana alivyokuwa akinishika mkono wangu, Uwepo wake ulifukuza hofu yangu, na sikuwa na huzuni kuhusu nikionacho.

SHANGAZI YANGU
Nikaona mwanamke kwa mbali akiwa motoni , mapepo yalikuwa yakimtesa sana [Nahumu 2:10].Alikuwa akilia  kwa kadiri alivyoniangalia mimi na nikamuuliza Bwana, “Huyu ni nani?”.Bwana akaniambia, “NI RUTI, SHANGAZI YAKO”[mzaliwa wetu wa kwanza].Alikufa miaka mingi iliyopita ,huzuni kubwa kiasi gani;alikuwa pale kwa sababu hakumjua Bwana.Sikuwa na furaha na nilikuwa nafikiri nami pia naweza nisiingie mbinguni.Bwana alijua mawazo yangu yote na kuniambia , “MIMI NI MAISHA YAKO”.Nilitaka aniahidi kwamba sitaishia kuzimu naye YESU akasema “....KAMA UNALIJUA JINA LANGU !”.Mara zote ameniambia “USIOGOPE,MIMI NI MAISHA YAKO !”.

KANISA
Kanisa linatakiwa liamke na livae silaha zote za MUNGU.Niliona kundi la mapepo, wamekusanyika na nikaona kitabu kikubwa mbele yao.Wakaanza kufungua na mara wakafungua kurasa na wakasema “Ndio,tunakwenda kupambana na kanisa”,wakafunga kitabu.Ghafla ,mapepo yasiyoweza kuhesabika wakatokea wakiwa na mishale mikononi mwao kuirushia kanisa.Nilishangaa , ndipo Bwana akaniambia, “HIYO NI MISHALE YA USINGIZI NA UDHAIFU, WANAITUMIA HIYO ILI WATU WANGU WASIOMBE, WASIFUNGE NA KUZAA KWENYE UFALME WANGU”.Mapepo yote yana lengo moja na lengo lao ni kupeleka watu kuzimu.Kanisa linatakiwa liamke, tunatakiwa tuombe kinyume na nguvu zisizo onekana zilizo panga kinyume na kanisa[Efeso 5:14].

Niliona pepo lenye nguvu sana,nalo lilijigeuza na kuonekena kama mwanamke mzuri ambaye alionekana mtaratibu na kama mkristo mzuri.Aliingia kanisa moja kumvamia kaka ambaye si muda amempokea YESUKRISTO.Alikuja tuu ili amtongoze huyo kaka ili apoteze wokovu wake.[Yoeli 1:14] “ Tuitishe kutano kwa kudhamiria kabisa na kulia kwa Bwana ili aamshe kanisa, kwa sababu wale walio lala wanapotea”[1 Wakorintho 15:18].
Kanisa linahitaji uamsho wa kiMUNGU, tujijengee maisha ya maombi na kuharibu kila mbegu ambayo Bwana hakuipanda katika kanisa.[ 2Wakorintho 10:4-5].Kuna mapepo wengi sana siku hizi wanaotenda kama watu.Wanataka kutongoza kanisa[2 wakorintho 10:13-15].Ili sisi tuweze kuwashinda ni lazima tuvae silaha zote za MUNGU[Efeso 6:10-18].Kumbuka hizi ni nyakati za hatari[2 Timotheo 3:1-7].

WAKRISTO WANAOMLINDA SHETANI.
Bwana alinifundisha somo na kuniambia, “WAKRISTO WENGI NI WALINZI WA SHETANI”.Nikajiwazia mwenyewe, “Inawezekana vipi kwa mKristo anayeomba kinyume na shetani amlinde shetani?”.

Bwana akaniambia “kuna vitu kwenye maandiko ambavyo nimeviwekea hatia.shetani anajua kila kitu nilichokiwekea hatia na anatendea kazi hivyo.Baadhi ya waKristo huwaambia wenzao ‘si dhambi’ huku ni dhambi.shetani anatafuta njia kuhakikisha kufanya dhambi  kama sio dhambi”.Kwa Mkristo pia anayesema “si dhambi” na huku ni dhambi, huyo hujiweka mwenyewe kuwa mlinzi wa shetani[1 Petro 3:3].

YESU akasema “nimeonya kuhusu mavazi ya kidunia, lakini baadhi husema ‘sio mungu alichomaanisha, ni imani yetu’.....baadhi husema kuvaa hereni sio dhambi,mwanangu sijasema tuu hereni lakini hata kuvaa dhahabu au siliva.wanaovaa ili kuupendeza kumwili”.[yakobo 5:3]. “Usihusike na muonekano wa nje unaotegemea vito(jewelry), au uzuri wa nguo, au mpangilio wa nywele”.Tuna uzuri wa aina mbili ,uzuri wetu wa nje na uzuri wa ndani.

Na usiwe muonekano wa kupaka rangi nywele, kuvaa dhahabu au kuvaa nguo ya mapambo[1 Petro 3:3].Bwana alisema “kama mKristo yeyote akisema ‘si dhambi’ wao ni walinzi wa shetani” na anayekuwa mlinzi wa shetani hawezi kuingia katika ufalme wangu”.
Bwana akasema “mwanangu, soma nilichokisema katika kitabu [Kumbukumbu la torati 22:5],nawaonya watu wanitii mimi, kwasababu mwanamke anapovaa mavazi ya mwanaume au mwanaume anapovaa mavazi ya mwanamke ,wanamlaani mungu wa mbinguni na dunia, akisema hayuko sahihi katika kazi yake”.
Bwana alilia na kusema “mwanangu,mtu anamlaani muumba wake, na bado nawapa neema ya kutubu.lakini kama mtumishi wangu yeyote akikataa kutubu, na kuendelea kumlinda shetani ,nitawatapika nje ya mdomo wangu” [Ufunuo 3:15-16].

SHABAHA YA SHETANI
Bwana aliniambia shabaha ya shetani maisha ya maombi ya mtu,Mara maisha ya maombi yakifungwa basi uamuzi  wako kwa MUNGU nao umefungwa.Mtu naye anaanguka na kuwa majeruhi pindi maisha ya kufunga na kuomba yamefungwa.
Unatakiwa udhibiti sana na kujiongoza katika maisha ya kuomba.Pindi maombi ya mtu yanapo athiri ufalme wa giza ,shetani hujaribu kutafuta njia za kuzima nguvu ili moto uwe mdogo na ufe.[ 1 Petro 5:8].

Bwana aliniambia, “Angalia mtu yule ambaye mapepo yanamtesa kwa hasira”.Bwana akaniambia, “Alipokuwa duniani kulikuwa sikuzote kuna mvurugano na maharibifu makuu kwenye ufalme wa giza pindi aombapo.Na Nilikuwa napenda hicho......maombi yake yalikuwa yanamzuia shetani na kuharibu mipango yake yote.”

Shetani na wajumbe wake wakaanza kutafuta shabaha ya kuondoa maisha ya maombi ya yule mtu. Na wakamshikilia kupitia kinyongo, chuki na uchungu katika moyo wake juu ya ndugu mwingine kanisani.Bwana akasema, “Nilimuonya, lakini alikataa kunisikiliza mimi”.Mtu huyo alipatwa na ajali na kufa,[Mathayo 5:44] na sasa yupo kuzimu ya moto.Kuna wanakwaya wengi wenye chuki ndani ya mioyo yao juu ya wenzao katika Kristo.Hii ni mara mmoja anapoonekana kuwa anakipawa kikubwa kuliko mwingine.Ndipo watu wanaendeleza wivu na majivuno kwa sababu ya hayo, wafanyayo hayo wako katika hatari ya kuzimu.[Mathayo 18:4].
MPANGO WA MUNGU.
Bwana aliniambia, “Mpango wa MUNGU ni mkubwa kwa mwanadamu.Na pale popote MUNGU anapokuwa na mpango na maisha ya mtu, mipango ya shetanini kuharibu ahadi na mpango wa MUNGU”.Nikamuuliza YESUKRISTO “Shetani anaweza kuharibu ahadi na mpango wa MUNGU kwa mtu ?”.

Bwana akasema, “NDIO”,na Bwana anielezea, “Kwenye kila mpango na ahadi ya MUNGU kwa mtu, mara zote kuna vigezo, na katika hivyo vigezo, kuna neema na rehema....Neema ni nafasi ya kufanya marekebisho kama mtu akivunja kigezo chochote.Rehema ni kwa ajili ya mtu kusamehewa na MUNGU.Shetani atahakikisha unavunja vigezo.Kipindi MUNGU ameweka ahadi na Abraham, Vigezo MUNGU alivyompa ni kutembea naye kwa uaminifu”.

[Mwanzo 17:1-7].Mungu anampango kwa ajili ya maisha yako na vigezo vimeandikwa kwenye maandiko[Wagalitia 5:19-21].Sio hayo tuu MUNGU mwenyewe atakwambia mengi zaidi.Usipoteze neema katika vigezo vya MUNGU na rehema itakunyanyua juu.[Zaburi 91:11-12].

MKE WA MCHUNGAJI W.F KUMUYI AKIWA KWENYE UFALME WA MUNGU.
Tukatoka kuzimu ya moto na Bwana akanichukua mpaka mbinguni.Nilimuona mwanamke mbinguni, alikuwa mzuri sana, alitoka nje kwenye nyumba kubwa sana nzuri naye ndiye aliyekuwa mmiliki wa nyumba hiyo !.

Alikuja kwangu na sura ya kutabasamu, mawazo yake yalikuwa nami nimefika mbinguni kama mkazi.Nilishangaa nikijiuliza anaweza kuwa nani kwa kuwa utukufu wa MUNGU ulikuwa umembadili uzuri wa dunia.Bwana akaniambia, “Ni mke wa mchungaji W.F KUMUYI, Mtumishi wangu”.Nilikuwa na furaha kwa kuwa alikuwa amejaa utukufu wa MUNGU.Mbingu ni nzuri sana sehemu yote ilikuwa imejaa utukufu wa MUNGU.
Bwana akanionyesha mimi mto wa damu, nao ulikuwa baridi na umetulia na ilikuwa kama bwawa la kuogelea, Popote tunapomtenda dhambi MUNGU na tukaomba msamaha na kutuosha naye hutuosha kwenye mtu huo wa damu.
Bwana akanionyesha tarumbeta zitakazotumika kwa unyakuo.Akaniambia , “UJIO WANGU UKO KARIBU SANA”.Tarumbeta zilikuwa zinang`aa na zimetengenezwa na dhahabu safi.Bwana alinionyesha maandalizi ya Unyakuo.
Bwana akanichukua mimi kwenda kwenye ukumbi mkubwa na nikaona watakatifu wengi akiwa wamevaa mavazi meupe kabisa, wakiwa wanaimba,wakimsifu MUNGU, wakipaza sauti kwa Bwana-Utukufu wa MUNGU ulikuwa kati yao.Mbinguni ni kuzuri, kulikuwa kunanga`aa kila sehemu kwa sababu mwanga wote pale ulikuwa utukufu wa MUNGU.
NYUMBA KUBWA SANA YA MWANAMKE, MBINGUNI.
Bwana akanionyesha nyumba nzuri na kubwa sana mbinguni, Nikashangazwa ni nani anaweza kuwa mmiliki wa nyumba hii.Bwana akaniambia “Ni ya mwanamke na jina lake ni Margret.Amevuna roho nyingi sana kwenye ufalme wangu !.Roho alizovuna haziwezi hesabiwa na mtu, Ni tuu MUNGU mwenyewe .Kazi yake imejenga hii nyumba”.
[Mathayo 10:7] Alisalimisha maisha yake Kwangu, na vitu vya duniani vilikuwa si kitu kwake, Sasa ameishia katika utukufu wa ufalme wangu.Mkristo yeyote anayekataa kuvuna roho(watu) kuja kwenye ufalme wangu hawezi kuingia katika utukufu wangu”.[Mathayo 28:19-20],[Mathayo 10:32].

NJIA YA KUZIMU YA MOTO.
Bwana alinionyesha mimi njia ya kwenda kuzimu, ilikuwa ina watu wengi katika ile njia.Baadhi wanaonekana kama wakristo lakini walikuwa wakiendea katika njia ya kuzimu.Baadhi wameshikana mikono, mume amemshika mkono mkewe huku wakielekea kuzimu, mke akimshika mkono mume,Wazazi wameshika watoto wao mikono na baadhi wakienda wo wenyewe.Na kulikuwa kuna mzigo mikubwa mgongoni mwa kila mmoja wao.Kwa kadiri YESU alivyo kuwa akiwatazama ndivyo alivyozidi kulia kama mtoto.

Niliona kitu kilichonishangaza sana mimi; Niliona kundi la watu nao walikuwa wanawake na walikuwa wakijaribu kwa jitihada zote kupita kuingia njia ya mbinguni, lakini nguvu ilikuwa ikiwarudisha nyuma kuwatoa.Ndipo Bwana akaniambia , “Kisicho kisafi hakiwezi kupita kwenye njia Yangu”.[Isaya 35:8-9].Nikamuuliza, “Kitu gani kisicho kisafi kwao ?” .Bwana akaniambia, “Ni mavazi yao, wanavaa hereni, weavon, mapambo kichwani mwao(attachments), mikufu, vito.Wanavaa nguo za kiume, wanajaribu hata kujiremba wao wenyewe---Wanataka kupita kwenye njia yangu.Hiyo HAIWEZEKANI ! utii ni bora kuliko dhabihu !”.....Akaendelea kulia.
[Isaya 3:16-24],[1 Petro 3:3],[Kumbukumbu la torati 22:5].Bwana akalia kwa uchungu na akalia kwa sauti kama mwanamke wodini.Ninyi mnaodhani unaweza kufanya vyovyote unavyodhani baada ya kumpa maisha yako KRISTO, Unajidanganya mwenyewe !.Usisikilize uongo wa shetani, unapozaliwa upya ,ya zamani yamepita [2 wakorintho 5:17].
NJIA YA MBINGUNI
Bwana alinionyesha mimi njia ya kuelekea mbinguni.Niliona watu lakini sio wengi kama kwenye njia ya kwenda kuzimu.Kwenye hiyo njia niliona baadhi wakiendelea mbele, baadhi wanasonga kwa furaha, na wengine wakicheza kumsifu MUNGU.[2 Wakorintho 13:9], [2 Wakorintho 12:9].

Muda kidogo nikagundua wako wachache zaidi na hakuna milima mirefu katika njia ile , ambayo mtu akifika hapo anatakiwa apande ndipo ashuke kuendelea na safari.Nikagundua kuna baadhi ya watu walisha vuka vile vilima lakini wanaanza kurudi nyuma, walikuwa wamechoka kuendelea mbele.

Kama wewe ni mKristo wa aina hiyo, umechoshwa na majaribu, shida,umasikini na vitu vingine vingi.Na unadhani uamuzi mzuri ni kuacha wokovu, hivyo acha na umrudie YESUKRISTO kwa kuwa u kama mtu aliyemkimbia jambo lenye kutisha tuu/hofu na kuangukia kwenye shimo la simba.Bwana bado anakuhitaji wewe,lakini unatakiwa uvumilie. “Tunatembea kupitia mateso mengi ili kuingia kwenye ufalme wa MUNGU”[Matendo 14:22].Rudi kwa YESUKRISTO naye atakuokoa !,Kumbuka mateso ya wale waliorudi nyuma kuacha kumfuata YESUKRISTO yalivyo kule kuzimu ya moto [Yeremia 3:21-22].

Niliona baadhi wamesimama wakiwa hawaendi,wapo tu wamesimama hapo hapo.Kama wewe umKristo wa aina hiyo unafikiri niendelee kumtumikia MUNGU au niache, Unabidi uache mawazo maovuna usonge mbele.Chaguo zuri ni kusonga mbele hivyo omba upata nguvu ya kuendelea mbele[Waefeso 6:18].

Nikaona wengine wakitambaa, walikuwa wakipenda kuendelea katika njia hiyo, lakini walikuwa wamechoka.Kama wewe umKristo wa aina hiyo unaogopa wazazi wako zaidi kuliko unavyoogopa vitu vya KRISTO, unatakiwa uache.Hii ni hatari sana na baadhi yenu wazazi wenu wanawatesa ninyi, wanawafanya ili mmtende MUNGU dhambi.Unatakiwa uombe na kusema “hapana” kwa maamuzi ambayo ni tofauti na mpango wa MUNGU, Bwana anasema, “USIOGOPE”[Mathayo 10:28].

Omba upate nguvu ya kusimama na kuanza kusonga mbele kwa sababu MUNGU wetu ni mwenye nguvu.Lia Kwake, naye Atakusikia maombi yako[Efeso 6:14-18],[Yeremia 33:3].YESU alilia kwa uchungu na ilikuwa huzuni--- Bwana akaniambia mimi “Kimetokea nini mpaka umekuwa na huzuni ?,Kama kweli una huzuni, ndipo utawaambia watu kile ulichokiona”.

TUBU SASA
Ni muda wa kutubu kutoka kwenye dhambi yeyote.Haijalishi ni dhambi ya aina gani ambayo umeitenda,MUNGU ni mwaminifu kukusamehe wewe dhambi zako zote[Warumi 10:9-10].YESUKRISTO anapenda roho yakona hataki roho yako iende kuzimuya moto[Habakuki 2:13].MUNGU alimtuma mwanawe wa pekee,YESUKRISTO kufa kwa ajili ya dhambi zako na zangu !,Yeyote amwaminiye Yeye hata angamia lakini atakuwa na uzima wa milele[Yohana 3:16].YESUKRISTO ni njia pekee  ,ya Kweli, na uzima na hakuna atayeweza kuja kwa Baba pasipo kwa njia ya YESUKRISTO [Yohana 14:6].

Tubu sasa na uokolewe[Matendo 17:30-31].Kama ukotayari kumpa maisha yako KRISTO basi omba sala hii:-
     Bwana YESU, Najijua mwenyewe kama mwenye dhambi , Najijua niko gizani, lakini sasa niko tayari kufanya kile onachotaka mimi nikifanye.Tafadhali nisamehe dhambi zangu zote,nioshe mimi katika mto wa damu yako, niponye,nitie nguvu,nipe uweza, na nguvu zaidi dhidi ya mwili na achilia ufalme wako uje ndani ya moyo wangu.Andika jina langu katika kitabu cha uzima na iwe furaha kubwa mbinguni juu ya wokovu wa roho yangu.Katika jina la YESUKRISTO nimeomba .Ameni.

Tafadhali nakuomba u SHARE kwa wengine nao wapate habari hizi za wokovu lakini ,Kwa shuhuda nyingi zaidi angalia kwenye www.jasirimbarikiwa.blogspot.com. Ubarikiwe !.



5 comments :

Andika maoni yako hapa !! ... You may comment here !!!

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...