MBINGUNI, KUZIMU NA HALI YA SASA YA KANISA ----Mtumishi Rodolfo Acevedo Hernandez


Mimi ni mwinjilisti Rodolfo Acevedo Hernandez.Koo langu limeathirika sasa kwa kushuhudia huu ushuhuda, lakini nitaendelea kushuhudia na kushuhudia hata kama kunaupinzani.Utukufu kwa MUNGU !,Nakwenda kutoa ushuhuda utaobadili maisha yako na maelfu kwa mamilioni ya watu wengine.

Ufunuo 1:14-15 -“14 Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe, kama theluji; na macho yake kama mwali wa moto;
 15 na miguu yake kama shaba iliyosuguliwa sana, kana kwamba imesafishwa katika tanuru; na sauti yake kama sauti ya maji mengi.”

Kwa sababu sikupenda kuendelea kukaa katika hali ile ile ya kiroho nilipenda nikuwe zaidi kiroho,Ndipo nilipoamua kujifungia mwenyewe kanisani kwa siku nane.Siku nane za kufunga na kuomba, 
Kwanza hata kabla ya kuanza kufunga Bwana YESU aliniambia kupitia kwenye maono kuwa “Rodolfo, ni muda wa kujitenga mwenyewe kwa ajili yangu,” Na katika maono hayo nilipewa vazi jeupe lililo andikwa “Utakatifu mbele ya YEHOVA”.

Baada ya maono hayo dada mmoja kutoka kanisani kwetu ambaye alikuwa ni mmishionari alikutana name na kuniambia, “Rodolfo, nimekuota na katika ndoto hiyo Bwana ameniambia nikwambie ujitenge na madhabahu(kwa kuwa ulikuwa muhubiri); Bwana atakwenda kukuonyesha vitu vikubwa vitavyobadili maisha ya watu katika mataifa na dunia nzima.”
Nami nikaacha kuhubiri kwa huo muda na kuanza kujitiisha kumtafuta BWANA  kwa kuanza mfungo wa siku nane.Na ilipofika siku ya nne ya kufunga na kuomba, nilipokuwa nikiomba ghafla wakajitokeza mapepo wawili na nikawaona uso kwa uso.Mapepo haya yaliniambia “Rodolfo, hatutakuruhusu kuvuka mipaka yetu”;

Na wakapotea ghafla ,nami nikawa na hofu kubwa kutokana na jinsi nilivyowaona mapepo wale walivyotisha nao walikuwa warefu na wenye harufu mbaya ya kama sulfur kama vile wametoka moja kwa moja kutoka kuzimu.Walitumwa kunieleza kuwa hawataweza kuniruhusu kupita mipaka yao.shetani ndiye pekee mwenye kuzuia vitu,lakini YESUKRISTO alimshinda pale msalabani kalivari.Utukufu kwa MUNGU haleluya.

Nilipofika siku saba za kufunga na kuomba nilijikuta naishiwa nguvu sana nikamwambia Bwana YESU “Bwana, siwezi zaidi,mwili wangu u dhaifu sina nguvu.Bwana tafadhali nisaidie siwezi kutimiza makubaliano.Nisamehe mimi na unipe nguvu.”Ghafla, nilisikia kitu kimetoka nyuma yangu nakunisogelea mpaka kwenye sikio ikiniambia; “Rodolfo, usiache mfungo huu mpaka tutakapokuonyesha vitu unavyotakiwa kuviona”.Nilipata nguvu na kutiwa moyo kwa  sauti kwa sauti niliyoisikia.

Siku iliyofuata ambayo ilikuwa ni jumapili, nilikuwa najisikia dhaifu sana asubuhi.Jioni kipindi ibada inaendelea ,kulikuwa na neno lenye nguvu sana lilohubiriwa na mwinjilisti Ruben Bells.Ibada ilipoisha niliwasalimu kaka na ada zangu.

Papo hapo nikaanza kujisikia hewa inaniishia.Nilijisikia kuishiwa pumzi na sikuwa naweza kupumua.Watu katika kanisa wakaja kunizunguka na wakaanza kuniombea.Ghafla, nilijihisi kama vile kuna sindano nyingi ninazo chomwa nazo kwenye vidole na kucha zangu.

Kuna baridi ya hali ilikuwa inaingia mwili mzima kupitia yale maumivu ambayo yalikuwa kama vile mtu ananichoma sindano na nikajisikia nakata pumzi na moyo wangu ukashindwa.
Nilidondoka kwenye sakafu na watu wakazidi kuniombea, kulikuwa na wakaka kama kumi na wawili (12) hivi.Ghafla roho yangu ikauacha mwili nanikaona kabisa ninavyouacha mwili ukiwa umelala chini.Wallioko pale hawakulijua hilo na nini kinachoendelea, nilimuona dada mmoja ambaye ni muuguzi aliwaambia wengine “Atakuwa ana tatizo la shambulizi la moyo”.Nilitaka kuwasiliana nao ,kuwaeleza kinachoendelea hata kuendea mwili wangu yote hayo nilishindwa.

Bibilia imeweka wazi kuwa mwili wa mtu una roho,nafsi na mwili wenyewe.nafsi hurudi kwa MUNGU na roho huenda sehemu iliyoandaliwa ampbapo ni mbinguni au ni kuzimu.Bibilia imeweka wazi kuwa  mwili unarudi mavumbini kwa kuwa ulitoka mavumbini.

Ghafla nikaona kama taa zimezimwa na nikaanza kupaa kwenda juu kwa kasi isiyokuwa ya kawaida.Hata hivyo kuna vitu viliingilia ile safari ikawa kama nikaanza  kurudi chini ka kasi zaidi na zaidi nilivyozidi kwenda chini nikaanza kuhisia joto kali lisilo la kawaida.

Ilikuwa kuzimu na ilikuwa ikitisha sana na hapo nilikuwa ndio naingia na nikaona joka mkubwa ambaye kichwa chake kina nyembe nyembe badala ya magamba nikaendelea mbele nikakuta kuna jela.Kipindi naingia niliona macho ya kila aina yapo kwenye ukuta yakiniangalia.Ghafla, nikaona macho mawili yakitoka kwenye ukuta na kumbe ni pepo alikuwa anashani kwenye kifua iliyosomeka Mimi ni Kisasi”.

Muda huo mapepo wengi wakaanza kunijia kutokea kwenye ule ukuta.Pepo lililoandikwa Kisasi alisema kwa sauti “Mfalme Beelzebub, tunaye mmoja wa wakubwa aliekuwa akifanya vita kinyume nasi, ufalme wa giza..” Bibilia imeandikwa,  “21 Maana ingekuwa heri kwao kama wasingaliijua njia ya haki, kuliko kuijua, kisha kuiacha ile amri takatifu waliyopewa.”-2 petro 2:21.Kanisa linalomjua Bwana linapaswa kuendelea kuwa imara kwa kutambua YESUKRISTO ndiye tumaini pekee kwa ajili ya wokovu wa roho zetu.

Nilipokuwa pale ,Yule pepo aitwaye Kisasi alikuja karibu yangu na kuniambia, “Rodolfo,nataka unifukuze hapa kama mnavyowafukuza na kukemea mapepo ukiwa duniani”. Alipokuwa akisema ilijirudia rudia, ndipo akaanza kunipiga na kunitesa nikaona mapepo yapo kwenye msururu yakinifuata iliyaanze kunitesa.

Mateso yaliyopo kuzimu kwa wachungaji,wahubiri,wainjilisti….walioacha kutegemea nguvu ya MUNGU ni makubwa kuliko wengine.Hivyo kuwa imara unapotembea na Bwana,Huu ni muda wa kanisa kuwa imara.Muda ni sasa.Muda wa kanisa kucheza umefika mwisho.Tunatakiwa tuwe na ujasiri na ushujaa wa kushinda nguvu zote za kuzimukatika jina la YESUKRISTO,Yeye pekee ndiye nuru.

Yule pepo alinirushia mkuki mrefu ulioingia mpaka moyoni mwangu,Nilipatwa na maumivu makali sana yasiweza kuelezeka,Nilihisi kama mvua ya kemikali kali ipo kuzimu.Nilijisikia mwili wangu ukidondoka kutoka kwenye mifupa yangu na wadudu wakali wakitoboa mifupa yangu.

Bibilia imeandikwa “48 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.”-Marko 9:48, Zaidi katika Isaya imeandikwa “11 Fahari yako imeshushwa hata kuzimu, Na sauti ya vinanda vyako; Funza wametandazwa chini yako, Na vidudu vinakufunika.”-Isaya 14:11.Kuzimu ni kweli na YESUKRISTO hata agano la kale linaongelea kuzimu.

Mara nikaona kundi la mapepo wamebeba silaha, lakini zilikuwa za tofauti sana na za hapa duniani.Pepo anayeitwa Kisasi aliitoa sehemu ya chini ya mdomo wangu na akaniambia “Rodolfo,nataka sasa unikemee!,haya nguvu yako iko wapi?,Uko wapi utukufu uliokuwa nao?”
Ujumbe ninaotaka kuutoa ni huu kwa kuwa muda mwingine kwa sababu tunahubiri,na tunafikiri kuwa upako ni wetu na nguvu ya MUNGU ya kuponya,kutoa pepo ni yetu.

Bibilia inasema utukufu  watoka kwa MUNGU na huo utukufu ni wake MUNGU pekee.Kwa sababu ifananayo kuwa shetani alitupwa kutoka mbinguni kwa sababu alitaka kujitwalia utukufu wa MUNGU uwe wake.Kwa hiyo watu wengi huamini kuwa wagonjwa wanapona sababu wanaweza kutumiwa na MUNGU kuponya wagonjwa,au kufungua waliofungwa na mapepo.
Nataka nikambie kuwa hizo ni vipawa ambavyo MUNGU ametoa kwa huruma yake kwa lengo la kufungua roho zilizofungwa na kuwa huru.

Ghafla nikaona mapepo yakijificha kwa haraka na nilikuwa chini na kitu cha kwanza nilichokiona sitasahau.. ohh! utukufu kwa MUNGU!,Niliona mwanga mkuu….haleluya,niliona makovu kwenye miguu yake.

Nilimuona huyu mtu alikuwa mzuri na mkanda kwenye kiuno imeandikwa, “MFALME WA WAFALME ,na BWANA WA MABWANA,”Alikuwa na taji kubwa la dhahabu,akanyoosha mikono yake kwangu na akasema “Rodolfo,NINAITWA YESU na MIMI nitaenda kukuonyesha wewe vitu vingi huku kuzimu, mbinguni na hali ya kanisa duniani.” Alinishika mkono wangu na kuniambia “Twende sasa, Rodolfo.”

MAKAHABA NA MALAYA
Niliona sehemu kubwa ambapo alikuwepo mwanamke.YESUKRISTO akasema, “Ninakwenda kukuonyesha adhabu anbayo shetani hutoa kwa wale ambao walikuwa malaya walipokuwa duniani,Wanapokufa malaya ndipo huja katika hii sehemu .Chunguza , Rodolfo.”

Nikaangalia nikaona akiwa amefungwa, na yuleyule joka niliyemuona mwanzo.Nimuona yule joka anamuingiliasehemu za siri za mwanamke Yule;napia ukumbuke nilikwambia ngozi ya joka hili ilikuwa ina viwembe na sio magamba.Yule joka alivyokuwa akimwingilia mwanamke ,anaharibu viungo vya ndani.Yule Joka anamwingilia kwenye sehemu za siri na kwenda kutokea kwenye mdomo.

Pepo anayeongoza ukahaba na umalaya duniani anaitwa, “Metresa au Martha”,au “Domineur”.Wengi wakatoliki wanaye huyu nao humuita mtakatifu kama mwanamke ambao mwili wake umezungushwa na joka na pepo hili nao ndio wahusika katika kutesa makahaba kuzimu.
WANAOTOA MIMBA
Bwana akaniambia ni muda wa kuhama hiyo sehemu na tukaacha Yule mwanamke akilia kutokana na mateso anayoyapata kwa uchungu. “Nahitaji mtu anisaidie mimi” Alilia sana kwa uchungu.Bwana YESU aliniambia, “Rodolfo, hukumu ilishatolewa kwao,Sasa Rodolfo, sasa nakwenda kukuonyesha sehemu ambayo shetani hutesa wanawake waliokuwa wametoa mimba(ujauzito)huku duniani.

Mara nikamuona mwanamke yuko katika hali ya kuzaa na nikaona lipepo lenye kutisha ambaye mikono na miguu yake ipo kama ya punda na kulikuwa na funza wakubwa wenye pembe kali na wenye meno makali waliokuwa wakimtoboa sehemu za siri za mwanamke yule.
Mwanamke anatobolewa kwa mateso makali mpaka mwanamke anaonekana kama vile mjamzito,Ndipo mapepo yanamwambia kwa sauti “zaa sasa huyu kwa kuwa ulikataa kuzaa ulipokuwa duniani ,mapepo huzidi kusema sifu, sifu shetani huu ndio ufalme wako! ”.

Nilipomuuliza Bwana kwa nini mateso ni makubwa sana kwa mwanamke huyu,Bwana YESU akanijibu, “Rodolfo, hukumu ilishawekwa kwa huyu mwanamke !”.Bibilia inasema wauaji hawataingia ufalme wa Mbinguni.Watu wanaotoa watoto au wanaoua wakiamini wanafanya hivyo kama vile kuua mnyama, lakini wanachofanya wanaua binaadamu mwenye nafsi,roho na mwili.

Shetani aliendelea kupiga makelele kwa yule mwanamke akimwambia msifu shetani kwa sababu ni ulikuwa ni ufame wako.Hao funza walikuwa wakitoka kwenye tumbo la yule mwanamke wakiwa wameharibu kila sehemu ya ndani ya yule mwanamke na walikuwa wakitoka na vipande vya nyama nyama midomoni mwao.

SIRI YA KATUNI NA GAME ZITOKAZO KUZIMU
Unaweza hisia ni maumivu na mateso kiasi gani aliyokuwa anayapitia.Bwana akaniambia, “Tutoke kwenye hii sehemu”.

Tukaenda kufika sehemu ambako kuna vitu vyeusi, ndipo nikaona watoto wengi hapo kuzimu.Nikamuuliza Bwana YESU, Kwa nini kuna watoto huku kuzimu ?” Lakini Bwana akaniambia hawakuwa watoto, kwa kuwa ufalme wa Mbinguni kwa watoto ni wao na mtu anazaliwa tena ili kuingia katika ufalme wa mbinguni.Nikamuuliza “Bwana, sasa vipi kuhusu hawa watoto ?”,

Bwana YESU akanijibu tena “Rodolfo, hawa si watoto”, Lakini aliniambia sikiliza amri ambazo shetani anawapa.Nilipowaangalia kwa umakini na wao walipogeuka nyuma nikagundua kuwa hawakuwa watoto lakini ni mapepo nao walikuwa wakicheza gemu(game) linaloitwa Nintendo.

Nikaanza kuona kila aina ya programu za kishetani na gemu zikitoa ishara za kishetani kutoka katika mikono yao.
shetani akiwaamuru mapepo hayo akisema “Watoto wangu,nendeni mkaibe,mkaue na kuharibu.”Alikuwa sahihi kwa sababu bibilia inasema shetani amekuja ili kuua,kuiba na kuharibu, lakini YESUKRISTO amekuja ili kuleta uzima tena uzima tele( yohana 10:10).

Nikaona hao mapepo wadogo wameingia duniani na Bwana akaniambia ndiyo maana watoto wa sasa duniani wanajiua wao wenyewe hata wanasaikolojia hawaelewi kwa nini kinatokea hivyo.Miezi michache iliyopita , ilitokea tukio la mtoto wa miaka kumi na miwili(12) aliyemuua mama yake kwa kisu,na mwingine akajinyonga yeye mwenyewe,na Marekani ,mtoto wa kiume wa miaka saba(7) aliyemuua mama yake, mdogo wake wa kiume na akajiua hata yeye mwenyewe na bastola aliyekutwa nayo.

Mtoto mwingine alijirusha kutoka kwenye gorofa ya pili na kujiua mwenyewe.Ujumbe na barua zilizoachwa na watoto hawa zote huazungumzia kuwa maisha hayana maana wala thamani yoyote.Haya yote yanatokea hawa mapepo yamewaingilia miili yao na kuwa ongoza kujiua na mauaji yeyote mabaya.

Baba na mama ,wazazi na walezi wote nawaambia muwe makini na watoto wako na kile wanachokiangalia kwenye luninga.Wanachokitazama kwenye mtandao,wanachokisikiliza kwenye redio.Mapepo sasa wanawaingia kupitia luninga,muziki na komedi za kishetani.Utukufu kwa MUNGU,Haleluya, Kwa kutuamsha na kutujuza ukweli huu.

Bwana YESU aliniambia kuwa hiyo ndio sababu ndoa nyingi zimeharibiwa kwa sababu baadhi ya wazazi huwalaumu watoto nao hufikiri wao ndio  haswa kigezo cha kutalakiana, Lakini watoto si tatizo bali tatizo ni mashambulizi ya nguvu za giza zilizo kinyume na ndoa na familia kiujumla.Mwite YESU ita kanisa tuombe tuweze kuwa na nyumba huru,huru kabisa.
WAABUDU SANAMU
Tulipotoka katika hiyo sehemu tukaenda sehemu ingine nikamuona mwanamke amezingirwa na moto mkali , huyu mwanamke alikuwa akilia sana huku akisema ‘nife !,nife!,nife! Nitoe hapa’ Nilimuona huyu mwanamke akiwa na picha mkononi mwake “Picha ya Moyo mtakatifu wa kutisha wa yesu wao kutokana na tamaduni za wakatoliki(waroma),”. Bwana , huyu mwanamke ni nani ?,Bwana akaniambia “Rodolfo,huyu mwanamke ni bibi yako”.
Bibilia inasema waabudu sanamu hawataingia mbinguni.BwanaYESU akanionyesha maisha ya bibi yangu alipokuwa duniani na nikaona jinsi alivyokuwa muabudu sanamu.

Niamuomba Bwana “tafadhali naomba umsaidie”.Bwana YESU alinijibu, “Rodolfo,siwezi kufanya chochote kwa huyu ,Hukumu ilishatolewa kwake”Bwana akaniambia, “Nitakwenda kukuonyesha wewe kitachokufanya wewe upitie mateso duniani.Wengi hawataamini kile unachokwenda kukiona, lakini usihofu nitakuwa pamoja nawe.”
CELIA CRUZ YUPO KUZIMU
Ghafla nikamuona mwanamke akiwa na miguu yake ikiwa imesagwa sagwa na visu vilivyo fikia hata magotini na muda huo huo mapepo mengi yalikuwa yakiendelea kumtesa, Nilipomuangalia nikagundua kuwa alikuwa ni Celia Cruz!.Bwana YESU alinionyesha mkanda wa Celia Cruz akifanya makubaliano ya kishetani akiwa na damu alipokuwa Hollywood ,

Nilimuona akifanya vitu vingi sana vya kishetani.BWANA YESU aliniambia, “alikuwa amejiunga kwenye ushetani na kuabudu shetani.Alikuwa mchawi mwenye kutumia damu ,ili afanye miziki yake  ifahamike sana(kuwa maarufu) na kufanikiwa.Yeye pamoja na kundi lake”.

Bwana YESU alinisikilizisha nyimbo yake moja iliyokuwa ikiitwa “Yemaya”,Nyimbo ambayo ni maarufu sana ingawa imeimbwa kiihispania.Unapoimba nyimbo hiyo na kurudia rudia kutaja “Yemaya”,Bwana YESU alinifahamisha kuwa maanayake ni “mfalme shetani, njoo na unimiliki mimi” na Bwana YESU akaniambia, “hukumu ishatolewa kwa Celia Cruz.”

Duniani:Celia Cruz alikuwa ni mkyuba wa kiamerika na alikuwa mmoja ya waliofahamika na kufanikiwa sana kama muimbaji wa muziki aina ya salsa kwa karne ya 20,akiwa na tuzo 23 za ushindi wa album za dhahabu.Naye alijulikana kimataifa kuwa ndiye “malikia wa salsa” pia alifahamika kama “la guarachera de cuba”.

Muanzilishi wa Mashaidi wa YEHOVA, (Charles T Russell) YUPO Kuzimu.
Tuliendelea kutembea na Bwana YESU naye akanionyesha mtu ambaye mikono yake ilinyooshwa chakushangaza mtu huyu alikuwa na upanga mzuri katika ulimi wake na huu upanga umepitiliza mpaka kichwani pake na kutokea nje ya mwili wake.

Miguu yake ilifungwa na nyororo na mgongoni mwake kulikuwa kumejaa nyembe zimewekwa kila namna kiasi kwamba hata ajisosogeze kwa namna gani lazima akatwe.Nilipo ona yule mtu yupo katika hali ile ya mateso makali sana,

Nikamwambia Bwana YESU, “Bwana, tafadhali msaidie,mfanyie chochote Bwana YESU,Angalia maumivu makali anayoyapata mtu huyu”.Bwana akaniuliza mimi “Je wamjua mtu huyu?,” Nami nikamjibu “hapana simjui mtu huyu,Ila nimeona visu vingi katika ngozi yake na hata katika mifupa yake na jinsi ilivyojia hadi nje ya mwili wake na jinsi anavyo piga kelele kwa maumivu makali anayo yapata”.

Bwana YESU akaniambia “Hukumu ishatolewa kwa mtu huyu, Sasa nitakwenda kukufahamisha huyu ni nani.” Kwasababu ya ufunuo huu,Bwana aliniambia “Utakimbia mji mpaka mji kwa sababu haya yatakuletea mateso makubwa lakini nitakuwa nawe.”Akaendelea kusema “Rodolfo, huyu mtu anaitwa Charles T. Russell,huyu ndiye muanzilishi wa madhehhebu ya Mashahidi wa Yehova”.

Nikamwambia “Bwana YESU tafadhali naomba umsaidie” naye Bwana akaniambia “Hapana, Rodolfo”.Bwana YESU akaunyosha mkono wake,mara nikaona roho nyingi za watu zinazo anguka chini kuzimu kwa kila njia inayowezekana:walikuwa wakiangukakichwa kwanza,miguu kwanza,tumbo kwanza na n.k.

Bwana akaniambia “Rodolfo, kwa ajili ya huyu mtu aliyelaaniwa roho nyingi za watu zinaenda kuzimu.Huyu mtu anafundisha kuwa MUNGU ni tuu MUNGU wa upendo.Bibilia inasema MUNGU ni moto ulao.Huyu mtu Charles Russell ametoa neno ‘kuzimu’ kutoka kwenye bibilia neno ‘sheol’ na ‘Abadon’.

Pia wanakata uungu wa YESUKRISTO na kukataa uungu wa Roho Mtakatifu nao wameweka neno pekee Yehova katika bibilia.
Ameondoa YESU na Roho mtakatifu.Kwa ajili ya huyu mtu aliyelaaniwa roho zote hizi zina anguka na kwenda kuzimu” (ufunuo wa yohana 22:18-19).Ndipo Bwana alisema: “namlaani mtu huyu”.

Tafadhali sana ‘Mashahidi wa Yehova’ nisikilizeni sitataka kuwafanya mjisikie vibaya au kuwaumiza ninyi.Ondoka upesi na mje kwake YESU.Sikuchukii na sichukii dini yako, lakini mpo katika uongo mkubwa sana,sasa mje kwa YESU.YESUKRISTO anawasubiri kwa mikono iliyofunguka kwa wote wataobadilika.Charles Russell yupo kuzimu kwa sababu ya kuanzisha na kufundisha uongo.Msifuate uongo.

Tulipotoka pale na milago ya gereza lile ikajifunga na motomkali ukaendelea kuunguzana ye Charles Russell akalia kwa uchungu sana na kumlaani YESUKRISTO nakurudia rudia kwa sababu YESU alisema “Hukumu ishatolewa kwa mtu huyu”.

Bwana YESU akaniambia  “Rodolfo, sasa ninakwenda kukuonyesha jela nyeusi ambazo zipo huku kuzimu.Jela ambazo zinamateso zaidi,” Nami nikamwambia Bwana YESU “Hapana Bwana ,tafadhali sana Bwana !,nimeshaona vingi vya kutisha nitoe hapa Bwana”.Bwana YESU akaniambia, “Sawa,Rodolfo, sitafanya chochote usichoniruhusu mimi.Ninakwenda kukuonyesha mbinguni sasa”.

MBINGUNI
Tuliondoka kwa kasi sana natulipo kwenda kusimama tukakutana na malaika wazuri wawili katika lango walikuwa wakubwa sana.Hao malaika wawili waliniambia mimi “Rodolfo, na hizi nguo zako za dhambi huwezi ingia katika ualme wa MUNGU.” Ndipo wakanipa mimi mavazi mapya nahayo yaliandikwa UTAKATIFU.

Wachungaji, Wainjilisti, Wahubiri, Wamishioni; Tafadhali sikia hili,MUNGU hajakuita ili uhubiri wingi wa utajiri au unabii kuhusu hayo.MUNGU amekuita ili uhubiri utakatifu na utakaso, sababu bila ya utakatifu hauwezi kumuona Bwana.Chukua neno na ulisambaze neno la utakatifu na ulihubiri kwa watu wote.

Ndipo hao malaika wakaniruhusu baada ya kunipa mavazi ya utakatifu na wakaniambia YESU anakusubiri ,YESU akaniambia “Rodolfo mtoto wangu, karibu kwenye Ufalme wa MUNGU wako”.Nilipoanza kutembea kwenye mitaa niliona mitaa yenye dhahabu halisi na nikaona mto kama kioo  nan i maji haswaa.Pia nikaona mapambo ya almasi kwenye mitaa,kitu ambacho watu wanauana duniani ili kupata almasi hiso nawakati mbinguni zimejaa tele.

Bwana akanishika mkono na kuniambia “nakwenda kukuonyesha hekalu”  napo palikuwa pazuri nikaona bilauri za dhahabu,vyombo vya dhahabu na nikasikia sauti nzuri nao walikuwa watoto waliokuwa wakiimba vizuri sana.Bwana akaniambia kwamba hao watoto ni wale waliokataliwa duniani lakini wakaufikia ufalme wa MUNGU.Utukufu kwa MUNGU, haleluya !

Tukaendelea tukitembea  nikaona vazi kubwa sana na zuri sana jeupe lililopambwa na dhahabu na taji juu yake na Bwana akaniambia hiyo ni kanisa lake,Kwamba linatakiwa kuwa takatifu nakusafika.Taji ni taji ya uzima ambayo Bwana atakwenda kulipa kanisa.Tukaendelea na nikaona mstari mkubwa wa watu nao walikuwa wamevaa mavazi meupe, nikawaona malaika wakubwa wawili kwa kuangalia kwenye macho yao nikaona amani,upendo usiokuwa wakawaida.

Malaika mmoja akaniambia “Karibu kwenye ufalme wa MUNGU”.Nikawaona watu wenye furaha sana na hapo nikakumbuka kile alichokisoma katika neno la MUNGU(bibilia) kuwa shida na tabu za dunia si kitu ukilinganisha na utukufu ambao Bwana MUNGU aliotuandalia mbinguni.

Bwana akanichukua na kunionyesha meza ndefu bila ya mwisho,meza ya dhahabu,bilauri,visu, umma, viti na vyombo vine vyote vya dhahabu.Nikaonyeshwa taji kubwa na ndogo naye Bwana akaniambia zile taji kubwa ni kwa ajili ya watumishi wake, Watakapo kuja kwenye karamu ya arusi ya Mwana kondoo.
Bwana akasema “Kwa sababu karamu ya arusi ya Mwana kondoo iikaribu kuanza.Ninakuja si muda kwa ajili ya kanisa  langu.Waambie nitakuja kunyakua kanisa”.

Nikamuuliza Bwana YESU “Haya mataji adogo ni kwa ajili ya akina nani ?,” Naye YESU akanijibu “Haya mataji madogo ni kwa ajili ya wale ambao wapo ndani ya kanisa ambao wameishi maisha matakatifu, lakini hawakufanya chochote kwenye Ufalme.Hata hivo nawaambia usiridhike na taji ndogo bali wewe fanya kazi ya Bwana kwa bidii ili naye Baba akupe thawabu kubwa”.Kilichonishangaza ni kwamba kila kiti kimeandikwa jina lake nyuma ya kiti hicho na hakuna yeyote anayeweza kukaa atika kiti hicho.
HALI YA SASA YA KANISA
Bwana YESU akaniambia “Rodolfo, ninakwenda kukuonyesha hali ya kanisa sasa hivi”.Nikaona samaki mdogo anamsifu na kumuabudu YESU kwa sababu Bibilia inasema:Wenye pumzi na wamsifu Bwana !

Ndipo Bwana akanionyesha dunia kuwa nikirudi duniani natakiwa nihubiri.Bwana alinipa uelewa kuwa yeyote anayeingia mbinguni husahau kila kitu kilichotokea duniani,Na huku wale walio kuzimu hukumbuka yote waliokuwa wakiyafanya duniani,familia zao, ndugu zao.
Kwa sababu hiyo sio petro sio maria sio Stefano sio Elisha wala yohana wanaweza kuwa nakumbukumbu ya jambo lolote walilolitenda au lililotokea duniani kwa kuwa ukiwa mbinguni unakuwa na ufahamu wa mbinguni na sio wakidunia.

Hivyo petro hawezi dhani hata siku moja kuwa wakatoliki wanamtukuza au mtakatifu yeyote yulei.YESU aliniambia , “Hakuna jina chini ya mbingu liwezalo kuokoa bali YESUKRISTO,mwana wa MUNGU anayeishi,”.Maria alipokuwa katika harusi kana aliwaambia kuwa “Neno lolote atakalowaambia YESUKRISTO hilo ndilo mlifanye”.

Watu wa kwanza wanao mwabudu shetani wapo VATICAN;  wao ndio wanaoficha kila njia za dhambi watendazo mapadri/makuhani kwa kulala na masista; makuhani kufanyisha ngono watoto wadogo(uzalilishaji watoto kijinsia) na hata katika jamuhuri ya Dominika,Nicolaus Lopez de Jesus Rodrigruez ni ushetani mwingine tena, naweza hata kukuhakishia hayo kupitia maandiko,Lakini bado Wakatoliki huendelea kuamini katika uongo wao wote huo.

Bwana YESU akaanza kulia sana alipoanza kunionyesha hali ya kanisa.Nilimuona mchungaji duniani amebeba begi kubwa lililojaa fedha.Bwana YESU akaniambia, “Hawa wahubiri na wainjilisti ambao wamekuwa matajiri kutokana na sadaka kwa sababu ya kuhubiri uongo kwawatu wangu na kusababisha watu wangu kupotea”.Nawaambia wahubiri na wainjilisti, muhubirini YESU hatakama hutapata mafungu ya kumi na sadaka.Takasa kanisa.
WATUMISHI WANAOPENDA FEDHA
Ghafla !,nikaona fedha zile zilizokuwa zimejaa begi zimeyeyuka na hazikuwepo tena.Nikamuuliza Bwana YESU maana yake naye akanijibu; “Vivyo hivyo kama fedha zilivyoyeyuka ,ndivyo navyo wao watakavyo yeyuka na kuondoka na mpinga Kristo.Lakini bado nina masalia ya watu wangu ambao ni waaminifu na hawajaharibiwa na chochote.”

Naona siku hizi jinsi watumishi,manabii,wahubiri,wainjilisti,mitume,wachungaji walivyo matajiri na mamilionea.Ingawa waumini katika makanisa yao wako kwenye umasikini, ni wahitaji wa chakula na huku mchungaji yupo katika utajiri mkubwa pasipo kuwasaidia waumini wao.Ni wainjilisti wengi sana ambao ni mamilionea hata hivyo ni mabilionea wakiwa kwenye magari ya kifahari sana.

Usamaria mwema uko wapi ?,Na nikaona wachungaji wengi wakihudumu kwenye madhabahu hata nikamuona mchungaji mmoja ambaye alipomaliza kuhudumu siku hiyo hiyo akaiacha familia yake nyumbani ambako mke wake alikuwepo na akaelekea kulala na mwanamke mwingine ambaye ni muumini wa kanisa hilo pia!.

VIJANA WASIO WAAMINIFU KWA MUNGU
Baada ya hayo Bwana YESU alinionyesha kundi la vijana katika kanisa ambao wakitoka makanisani huenda katika siri kwa kuwa hudhani Bwana YESU hawaoni na wanapofika huko huanza kujichua(punyeto) na kufanya uzinzi kwa kutumia miili yao wenyewe,Na baada ya hayo huenda kusimama ili kuhudumu madhabahuni !,raisi wa vijana,kiongozi wa kanisa!.

MAKANISA YALIOJAA NYIMBO ZA KIDUNIA
Bwana YESU alinionyesha disco na kanisa naye Bwana akaniambia nichunguze kwa makini,na nilipochunguza nikaona kanisa kama disco na hakukuwa na tofauti.Kulikuwa kuna aina ya muziki kama muziki wa disko,mpangilio wa kufanana,vifaa vya kufanana,vilivyotoka katika dunia na kuingia kanisani.
Dunia inabidibadilike kuufuata ukristo na sio vyovyote vile.
Sasa tumeileta dunia ndani ya kanisa!,Na pia ninapaswa niwaambie ukweli kuwa huwezi msifu aukumuabudu MUNGU na aina ya muziki wa rege,bachaton au rock.

Na hata sasa kuna nyimbo za kikristo zinazoimbwa kwa MUNGU na kwa dunia,wakitumia maneno yale yale !, Hawataji neno MUNGU lakini wanatumia tuu neno ‘upendo’.
Na pia nimeona muziki wa RAP na PERREO ikiimbwa na imo ndani ya kanisa na hiyo haikubaliki.Bibilia inatueleza tumuabudu MUNGU kwa uzuri wa utakatifu.Sasa ni nani alieanzisha muziki aina ya ROCK ?,Naye ni Anton Lavey,naye huyo ndiye muanzilishi wa kanisa la shetani.

Ametengeneza na kuandika bibilia ya kishetani na ndiye aliyeingiza muziki wa rock ndani ya Hollywood.Kama aligundua Rock, hiyoinamaanisha ni kwa ajili ya kumtukuza shetani na sio MUNGU.Kwa maneno mengine kile anachopewa shetani nasi twataka kumpa hicho hicho MUNGU? !,Hicho hakiwezekani na hakikubaliki kwa MUNGU.Rock ni miziki ya kishetani na imegunduliwa kuzimu.

Anton szandor LaVey,born Howard Stanton Levey, naye alikuwa ni muanzilishi wa kanisa la shetani pia ni muandishi,mwanachamahuru na mwanamuziki.
Wachungaji na wainjilisti , tafadhali tokeni kwenye hiyo miziki iliyo laaniwa na itoeni kanisani.Rap iligunduliwa na mtu aitwaye Selassie.Huyu ni nani ?,Huyu ni mtu aliye jiita mwenyewe kuwa yeye ni “Mfalme wa wafalme na Bwana wa bwana”.Na kanisa linatumia aina hiyo ya miziki na huku bibilia imeandikwa kuwa pekee aliye Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme ni YESUKRISTO,Mwana wa MUNGU anaye ishi.

WAIMBAJI WA INJILI WALIOPOTOKA
Bwana alinionyesha wanamziki waliokuwa wameacha sana njia yake(Bwana).Walikuwa wakiimba kanisani kwa mkono mmoja na wakiwa wanatengeneza tenda ingine  kuimba katika migahawa kama waimbaji binafsi:  wanamsifu Bwana kanisani!, nataka niwaambie kuwa muziki na uimbaji wa namna hiyo Bwana hautaki na pia unisamehe kwa kukwambia ukweli.

Kipi ni cha Bwana ni kile ambacho ni kitakatifu nan i kile kilichotengwa tuu kwa ajili ya Bwana pekee.Na hawa waimbaji wanaimba kanisani na baada ya kuimba huondoka hatakama ni katikati ya ibada,Kwa sababu inaonekana kana kwamba ni mchezo wa kutaka mkataba wa fedha kutokana na uimbaji wao, wanajihisi hawatakiwi kuwepo katika ibada nzima nao huondoka na kuishi maisha ya umaarufu.
Na katika wakati wote, Bwana akaniambia “Kwa bahati mbaya, aina ya kanisa hili halitaingia mbinguni.”
KANISA LILILO SAFI
Baada ya hayo Bwana akanionyesha  kundi la watu,maelfu kwa maelfu ya watu wanaojilinda wenyewe kwa utakatifu.Nikaona kwa mfano dada akimwambia mwingine; “Je umekula leo ?”,nina kipande cha mkate nyumbani kwangu.”
Nikamuona mwingine amebeba viatu vingi kwa mtu asiye navyo hata kimoja.Nikaona wengine wakiwapa nguvu wale wasio na nguvu.Wengine wanajua shida za wenzao na kuaanza kuzitatua, wakiwatunza na kuwaombea kwa ajili ya mahitaji yao bila yeyote kujua.
Lakini leo katika makanisa mengi kuna umbea mwingi kwa sababu hawajui namna ya kukaa kimya kuhusu mambo ya wengine.

Tubu; Leo YESUKRISTO anataka kukupa kukufungua na hata kukuokoa.Naye anaweza kukupa kipawa na neema ya kutubu.


UFUNUO WA KIMUNGU WA MBINGU NA KUZIMU na Mwinjilisti Margret Osasumwen Amure.


Naitwa mwinjilisti Margaret Amure;Mzaliwa wa Jiji la Benini nchini Nigeria.Nimezaliwa mwezi mei,mwaka 1957 na kuolewa na Mchungaji Olusola Amure.


Nilikuwa  nikiumwa na hata nikapelekwa hospitali mbalimbali  kwa vipimo na tiba lakini yote hayakuzaa matunda.Kuna daktari ambaye alinishauri  nitafute namna kama naweza ombewa kwa kuwa hali ilionekana kitabibu haiwezekaniki.
Kwa kuwa nilikuwa karibu na watumishi mbali mbali nikaombewa lakini hali yangu ya kiafya bado ikionekana mbaya bila auheni.

SAFARI YANGU YA KWENDA MBINGUNI
Mwezi septemba tarehe 29 mwaka 2012, mimi na familia yangu tuliomba kabla ya kwenda kulala.Nilipo lala siku hiyo kuna kitu cha ajabu kilinitokea kwa kuwa nilijikuta kwenye ardhi tupu iliyojazwa utupu.
Hakuna aliyekuwa anaingia wala kutoka, hakuna miti wala mito.Nikawa najiuliza “nipo wapi?”.
Nilikuwa nimeinamisha kichwa na nilipo nyanyua kichwa nione ndipo nikaona gati zuri kubwa la dhahabu.Pameandikwa kwenye geti ‘UTAKATIFU NA HAKI’.Nilianza kujiuliza kama nimekufa huku nikiwaza kuna jambo fulani ambalo halijakaa sawa.

Malaika wa BWANA waliponitokea
Nikaangalia kushoto kwangu nikaona msururu mkubwa wa watu wengi wenye watu aina mbali mbaliweupe,wafupi ,warefu n.k.Wazo likanijia likitaka nijiunge nao na nilipotaka kujiunga, sauti ikanijia nikasikia jina langu likaitwa, “Margret,... Margret ,....usijiungue.Kama ukijiunga ujue uko njiani kuelekea kuzimu.”

Nilipogeuka, niliona malaika wawili wakiwa nikimbilia mbio kuelekea kwangu. Wao waliniambia kwamba Bwana Yesu amewatuma kwangu ili kunizuia kuelekea katika makutano hayo, kwa kuwa yanaelekea kuzimu.
 Niliposikia neno kuzimu, machozi yakaanza kunitoka kwa kuwa  nilianza kufikiri ya sadaka yangu yote katika kanisa; miaka 20 katika kwaya, miaka 20 katika huduma, miaka 4 kama mchungaji. Hayo yote yalikuwa mawazo yangu yalionijia kwa haraka kwa njia ya mawazo yangu.Kitu cha ajabu ni kwamba malaika waliweza kusoma mawazo yangu kwa usahihi.
Wakaniambia “Tunajua sadaka zako zote, tena ni zaidi ya jinsi unavyofikiri tutapokuchukua kukupeleka kwenye nyumba yako iliyoko mbinguni ndiyo utajua zaidi.”
Nikawauliza wale malaika“Mmejuaje hadi mawazo yangu”.Wakajibu, “Hapa ni mbinguni hakuna tena siri .Duniani mna siri lakini si mbinguni”.
Nikawauliza “nimekufa?” ,Wakanijibu “Ndio, umekufa.Kila muda mtu anapolala iwe ni usiku au mchana , mtu huyo ni kwa muda huo ni sawa na amekufa.Ni YESUKRISTO ndiye huwaamsha”.Nikaanza kulia sana.
Malaika walisema wamepewa jukumu la kunichukua mimi na kunionyesha pande zote mbinguni, kuona mambo mimi ambayo ningeyakosa kutokana na maisha yangu ya kutojali na kuishi hovyo hovyo duniani.

Ghafla,nilipotazama vizuri nikamuona Yesu mwenyewe akatokea mbele yangu! ,Nilipomuona tuu, Nikainama kwa aibu. Sikuweza kuvumilia kuangalia katika uso wake.
Muda huo mimi nilikuwa nimelala chini kifudifudi.Nikaanza kumuomba YESUKRISTO msamaha, ili anipe nafasi ya pili. Bwana alinishika na kuninyanyua kwa kidole,lakini bado sikuweza kumuangalia na macho yake yalikuwa yenye moto.
Nilijihisi nisiostahili. Hata hivyo,nilijisikia vigumu kusimama kwa miguu yangu vizuri.
Kisha akasema, "Margret, nimekuleta wewe  hapa  ili ufanye ziara mbinguni, na ujionee mwenyewe nini waweza kukosa  kutokana na uzembe unaoufanya huko duniani.
Nimekuleta hapa kwa sababu nimeona nguvu yako kubwa toka moyoni na kutokana na matendo yako yote, kuzimu ndiko haswaa unapostahili.''. Nililia zaidi;

Kisha Yesu aliwaamuru malaika wanichukue na kunionyesha nyumbani yangu iliyo mbinguni.Basi sisi tukaanza kupaa kwa njia ya anga,Kuna sehemu tulipofika tukasimama na nikaona mwanamke mzuri  na Yesu alipojitokeza tuu mwanamke huyu alimsujudua YESUKRISTO mbele yake .
Malaika wakaniuliza kama mimi namjua mwanamke huyo ambaye anamuabudu YESUKRISTO,Mimi nikamjibu “mimi ni mgeni humu hivyo simjui mwanamke huyo”. Wao malaika wakanijibu kuwa huyo ni Maria ,mama wa YESU alipokuwa duniani.

Mimi nikasema kwa mshangao mkubwa na kuuliza malaika,
“Inawezekanaje mama kumuabudu mtoto wake, kusujudu mbele yake?” .Wao malaika walicheka na kusema kwamba “hilo ndilo ni kosa watu wengi hufanya juu ya nchi, kwa kusema kwa sababu Maria ni mama yake Yesu, nao wanamuabudu.
Maria si wakuabudiwa au kupigiwa magoti mbele yake, yeye ni mmoja ya watakatifu mbinguni.
Ulikuwa ni upendeleo miongoni mwa mabikira wengi katika Israeli wakati huo, kutumika kama chombo tuu cha kumzaa Bwana wetu Yesu Kristo.
Kwa kweli, kumbukumbu ya kuwa Maria alikuwa mama yake Yesu ilifutwa kutoka katika kumbukumbu zake muda mrefu sana.”

Nakumbuka kuna maneno ambayo Maria  aliniambia ambayo yameleta athari za kudumu nayo yalikuwa ya utulivu aliniambia “Margret , usikose nafasi hii. Margret usikose mbinguni”.

Tukaenda nao malaika ili  kuonyeshwa nyumba yangu iliyoko mbinguni, lakini kabla ya hapo, nilimuona mtu mwingine “nika uliza huyu ni nani ?,”  Wakanijibu , “huyu ni Ibrahimu, baba wa imani”. Cha kushangaza yeye anaonekana kama mtu wa umri wa miaka 25.
Kwa haraka nikainama na kutaka kumwabudu, lakini yeye haraka haraka akanishikilia kuniinua na kuniambia. “Mtu pekee wa  kuabudiwa mbinguni ni YesuKristo.” Ibrahimu alizidi kunitia moyo na kuniambia “Hufahamu kile ambacho Yesu anachokifanya kwa ajili yako kwa  kutoa nafasi hii ya pili. Utaporudi  duniani, wataarifu  mchungaji wako wakupe  majina yote ya Yesu Kristo, na uanze  kumwabudu  YEYE kila asubuhi ya maisha yako.”
Tukaendelea kwenda nilikuwa nachunguza chunguza pande zote na kuona kila kitu mbinguni.Na kwa mshangao wangu mkubwa kuna kitu nikagundua , tulikuwa tunapita na kupishana na  karibu na wanaume 2000  lakini wanawake  walikuwa wachache kama  watano(5) !.
Nikauliza, “wanawake wako wapi ?,Mbona wanawake ni adimu sana mbinguni ?.”. 
Malaika akanihakikishia mimi kwamba atanionyesha  wanawake wanapopatikana. Nilidhani labda wao wanawake wamewekwa sehemu fulani maalumu labda baadae nitaweza kuwaona.
Niliona nyumba ambazo ziko katika ujenzi maalum, nikazidi kuona nyumba mbalimbali zikiwa chini ya ujenzi.
 
Nikaiona nyumba fulani kwamba ilikuwa kama inataka kuporomoka, imepinda  na kuanza kuharibika.Nilivyoiona nikasimama na nilipoangalia juu nikashangazwa kuona imeandikwa Margret juu ya nyumba hiyo.
Nilidhani inaweza kuwa Margret yangu mwenyewe.Nao malaika waliweza kusoma mawazo yangu na wao waliniambia kuwa ni kweli nyumba hiyo ndiyo yangu. Mimi  nikaanza kulia, kuona hali mbaya ya nyumba ile, ilivyo ilikuwa kama inatakakuanguka. Nilianza kuomba kwao malaika ili wanisaidie ili nyumba hiyo isianguke wao malaika walisema “ni Yesu peke yake ambaye angeweza kuleta utulivu katika jengo hilo na kuliweka sawa.”. 
Nilipokuwa nikilia si muda, Yesu akajitokeza  mbele yangu! Naye akaniambia, 'Margret uliniita ?' nami nikajibu “hapana sijakuita Bwana”.
Yeye YESU alizidi nisisitiza kwamba nilikuwa namuita na mimi nikamjibu “hapana sijakuita Bwana !.”
YESU alieleza kuwa hakuna kitu kinachomgusa kwake zaidi kama kilio na machozi ya watu wake na kwamba kila wakati mtakatifu anapopatwa na maumivu au kilio,YEYE mwenyewe KRISTO huja sio malaika.
Nikamwambia kuwa tatizo langu ni nyumba yangu, kwamba  iko vibaya na sina uwezo wa kujenga nyumba tena kutokana na kuangalia umri wangu. Nilivyoteta  kwake, na Yeye YESU aliingilia kati na kutamka: “amani, iwepo”na mara nyumba ikawa sawa na kusimama vizuri.

Yesu aliniambia mengi kuhusu nyumba yangu ya mbinguni. Yeye aliniambia kuwa chini ya miaka 3 ya kubadilika kwangu(KUOKOKA) kabla ya kuolewa, nilikuwa tayari kumaliza nyumba yote na nilidhani mimi kwa Mungu hawakuwa na rekodi yangu kumbe la mbinguni wana rekodi zote. Alinikumbusha mambo yangu kuhusu wakati mimi nilipokuwa katika kwaya ya kanisa na jinsi mimi kutumika kuhamasisha wale waliokuwa wamekata tamaa na kutaka kuacha wokovu, jinsi mimi nilivyotumika kwenda kanisani kwa upande wa watoto na kwenda  kufanya kazi huko, jinsi Nilivyokuwa natumia fedha yangu binafsi kununua vitu kwa ajili ya kanisani na kwamba nilijua nyumba ya kila mtu ilipo, na kuwatembelea endapo sikuwaona ibadani, kanisani. Huduma hizi zote zilikuwa malighafi kwamba kumenisaidia kumaliza nyumba yangu ndani ya miaka 3. Yeye YESUKRISTO aliniuliza “nilianza kuabudu mwaka gani ?” mimi nikamjibu “nikamwambia ni mwaka 1980,” lakini Yeye akanisahihisha na kuniambia kuwa nilikuja kanisani mwaka 1979,mwezi Mei na Yeye ndiye aliyeniponya na maradhi makubwa niliyokuwa nayo.

Nilikwenda kila mahali na pande kuhubiri injili bila kujali kejeli za watu kwa kutokujua kwangu Kiingereza na hali yangu maskini. Hizo kazi zote niizokuwa nikizifanya zilikuwa malighafi ambayo hutumika katika kujenga jengo(nyumba) iliyoko mbinguni. Kulingana na Yesu, 'Hii ni mara ya saba ungekuwa unajenga upya nyumba hii, na hii ni nafasi yako ya mwisho na kwamba ni kwa nini tuna kuleta wewe hapa  ni ili uweze kuona utakavyovikosa na kwenda motoni kutokana na kutojali'


Kulingana na Yesu, jambo la kwanza kwamba hatia yangu ni chuki yangu kwa mume wangu. 'Kwa nini wewe chuki mtu sana?'  Yesu aliniuliza. 'Unataka nini mume wako afanye hivyo yeye haijafanya? Mimi najua wewe si kuhitimu na wewe daima kunung'unika kuhusu hili, lakini una wanne(4) wahitimu kama watoto wako .Je unafikiri ni kwa njia na uwezo wako mwenyewe kufanikiwa hivyo? Mimi YESU mwenyewe nalifanya hivyo kwa ajili yenu.Sasa badala ya kusaidia mume wako huyu ili aweze ingia mbinguni, wewe waushika uovu pamoja naye na bila kuzungumza naye kwa siku, miezi na wewe wote wanaishi chini ya paa moja.’


Hiyo ni nini ?,hiyo dhambi itakuleta kuzimu '. Angalia katika lango hapo, wakati wowote mtu yeyote akifa na hufika katika lango, Shetani naye husubiri mtu na Biblia. Biblia ni kitabu pekee,kinachotumika mbinguni na duniani.Vitabu vingine vyote vimetokana na hiyo. Shetani ataanza kutafuta vazi lako kama kuna doa lolote, na ataanza kunukuu dhambi yako kutoka katika Biblia. Yeye huuliza wewe kama mchungaji wako hakukwambia mahali fulani na fulani katika Biblia kuwa ni kosa. (Ufunuo 21: 27).Wakati wewe  unasema, Nasikitika, sauti itakuja kutoka mbinguni na kusema, “ondokeni kwangu ''.

Niitaka kujitetea ili kumwambia  Bwana sababu ya kutoeewana ambako kupo kwenye ndoa yangu, Yeye Bwana YESUKRISTO aliniambia nikae kimya kwa kuwa sina chochote cha kumueeza Bwana. Yesu kaniagiza kuwapa wanawake wote duniani, mistari hii ambayo shetani huitumia sana kuwaweka hatiani nayo ni:
Ø  Efeso 5: 22-24 22 Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu.
 23 Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili.
 24 Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.”-Waefeso 5:22-24

Ø  ,1 petro 4:9, “9 Mkaribishane ninyi kwa ninyi, pasipo kunung'unika;”-1 petro 4:9

Ø  1 Yohana 4: 20, 20 Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona.”-1 yohana 4:20

Ø  Waebrania 11:2 “2 Maana kwa hiyo wazee wetu walishuhudiwa.”-Waebrania 11:2.
YESU akazidi kuniambia kuwa  kuna wingu la mashahidi wa wale ambao walipitia majaribu duniani ambao sasa wako mbinguni na watu handio watakao hukumu Wakristo. Yusufu atahukumu wale walioanguka kwa kujipenda fedha na uzuri.Yusufu alivumilia yote kwa ajii ya utukufu wa MUNGU alieuona.Bwana YESU aliniambia kuwa wanawake wote ambao si watiifu kwa waume zao, haijalishi hali za waume za hata waweje, lango la kuzimu linawasubiri kwa ajili yao.Bwana YESU anataka wanawake wawe watiifu kwa waume zao.

Baada ya hayo, Bwana Yesu Kristo aliniambia mambo mengi kuhusu mume wangu na ugomvi wake na uovu wa kiroho. Yeye YESU akaniuliza kwa nini napenda kwenda kuzimu kwa sababu ya mtu mwingine.Akanionyesha kwenye kioo kikubwa ; sasa akanionyesha nyumba yangu ya hapa duniani, nikaona mwenyewe bado nimelazwa juu ya kitanda changu kando ya mume wangu . Alinionyesha jinsi tulivyokuwa tukiishi kwa kinyongo ambapo pia alinionyeshea tukio ambapo mume wangu na mimi tulikuwa tunapishana kwenye mlango na sisi tulihakikisha kwamba miili yetu haikuwa inagusana kutokana na kinyongo na uchungu tuliokuwa nao juu ya kila mmoja.


Nilipata upendeleo wa kuona baadhi ya nyumba za wachungaji huko mbinguni, baadhi hazikuwa tayari, baadhi zipo katika hatua ya msingi kabisa huko mbinguni. Yeye YESU alisisitiza kuwa wale ambao hawaja peleka vifaa juu mbinguni, hawapati nyumba yoyote mbinguni, kwa sababu hakuna anayeishi kama mpangaji huko. Mtu asiyeweza kumaliza kujenga nyumba yake mbinguni basi hawezi ingia mbinguni.

SAFARI YA KUZIMU
Yesu aliamua kunichukua mimi na kunipeleka kuzimu ili aweze kunionyesha baadhi ya mambo. Mimi nilipanga kumwomba basi anisimulie tu hayo mambo ya huko kuzimu na sio kunipeleka mimi huko kuzimu.Kwa jinsi mbinguni palivyokuwa ni mahali pa zuri sana. Kuna muziki mzuri usioweza kuelezeka  kutoka kila mahali.

Njia yetu ya kuzimu, tulianza kwenda chini na nilipofika karibu, nikaanza kuhisi hali ya joto kali. Wakati kuzimu ilipofunguliwa mbele ya macho yangu, mimi nilianza kulia.Kuzimu ilikuwa kubwa kama dunia nzima.

WACHUNGAJI
Niliona wachungaji, hata baadhi ya hao wachungaji ,wachungaji watatu  nilihudhuria mazishi yao. Sikuamini ninachokiona. Yesu naye alikuwa kando mti akilia. Kwa hasira, Yeye akaniambia simama na ghafla, baadhi ya watu walikuwa wanakuja kutoka ndani ya kuzimu.

Alizungumza kwanza, 'Dada Margret uko hapa? Je, kuja na maji? koo langu ni kavu '. Niliona pia mchungaji ambaye alisema nini kilimleta kuzimu ilikuwa ni uchoyo. Kabla ya hakuweza kueleza zaidi, yeye akachukuliwa .Mimi pia aliona mchungaji mwingine ambaye alikuwa kuzimu kwa sababu ya uasherati.
Yesu alikuwa kwenye kilio na Nikamuuliza kwa nini ulikuwa analia. Alisema yeye analia kila siku kwa sababu ni kana kwamba kifo chake juu ya mti wa calvary ni bure. 'Nalikufa kwa ajili yenu na nikakupeni kitabu changu kitakatifu, lakini mmekitupa mbali na kuchukua ile njia ya shetani, bwana wenu.’

Mimi nalimuuliza mtu mwingine, mchungaji ambaye alikuwa huko kwa sababu ya kuto kusamehe.Yeye alikuwa na ugomvi na mke wake na mkwe wake alikuja kutoka kijiji akachukua watoto na kuwaweka mbali na mkewe.Mumewe alikaa kwa wiki ndipo mkewe akamfuata alisafiri hadi kijiji na kulikuwa na ugomvi mkubwa huko, na tatizo bado halikupata ufumbuzi.Huyo mumewe ambaye ndiye mchungaji aliamua kurudi kwa njia yake, na alipatwa na ajali na ndipo alipojikuta kuzimu kwa kosa la kutomsamehe mkewe, kwa sababu yeye alikufa bila kukiri na kutubia dhambi yake;

Yesu alisema sisi sote ambao tuna wakati sasa wakutubu tutubu.Wakati huo wengi waliomuona YesuKristo, walikuwa wakimuomba hata dakika moja tu ya kutubu, lakini Yesu aliwajibu kwamba toba ni duniani tu.

WASIOTOA / KUMALIZIA MAHARI.
Mimi pia akaona mtu mwingine akihesabu fedha mbinguni. Mimi aliuliza mtu kwa nini alikuwa kuhesabu fedha na alijibu kwamba alikuwa anaenda kulipa mahari ya mke wake. Mimi nilishangazwa kuwa mahari ?, Hivyo mtu anaweza kujikuta katika kuzimu kwa sababu ya kutotoa mahari ya mke wake?
Kisha Yesu alinionyesha andiko linalounga mkono hayo.

WASIOAMINI KUNENA KWA LUGHA.
Bwana pia aliniambia kuwa mume asiachane na mkewe. Niliona pia mtu ananena kwa lugha katika moto wa Jehanamu. Nilipomuuliza, alisema duniani hakuamini katika kunena kwa lugha na pia alilaani wale ambao walifanya hivyo. Nilipomuuliza kwa nini. Kabla ya hakuweza kujibu, alivutwa kwenda katika moto.
MANABII WA UONGO.
Kisha nikaona kundi la watu wakisujudu katika mwelekeo fulani. Nilipomuuliza Bwana, alisema wale walikuwa manabii wa uongo kwamba walidanganywa na shetani mwenyewe. Baadhi yao wamezika mambo mbalimbali juu ya madhabahu zao, kama vile wanawake wajawazito, na hata wachungaji wenzao, wote katika jitihada za kupata nguvu, umaarufu na fedha. Alisema baadhi yao walianza vyema katika huduma, kabla ya kudanganywa na shetani. Yesu alisema hao wachungaji waliweza kwenda sehemu yoyote ili kupata nguvu na fedha. Kisha Yesu alitaja maeneo matatu hapa duniani ambayo ni India, Ghana na Ijebu -Ode ambapo wachungaji hao huenda ili kupata nguvu.


Nilishangaa kwamba Yesu aliweza hata kujua Ijebu-Ode! Yeye alijibu kuwa anajua kila
Nilishangaa kusikia YESU akiitaja Ijebu –Ode iliyopo hapa nchini Naijeria,Yeye YESU alisema anajua kila sehemu kwa kuwa yeye ndiye aliyeziumba zote .Yeye Aliongeza kuwa, kwamba hiyo ndio sababu mahali popote anapo omba mtu duniani, yeye daima huko. Yesu alizidi niambia kwamba wakati wowote mtu mwenye  wito anapo anza huduma, mtu huyo kawaida hupitia jangwa; Jangwa ni kipindi ambacho mambo huonekana si sawa(hayako vyema)bila , hata kwa sala, lakini kama mtu anaweza kuvumilia, yeye hufikia kwenye nchi ya ahadi, lakini hao wachungaji hawakuweza kusubiri. Hiyo ndio sababu wako hapa kuzimu '.

Niliona pia wachungaji ambao bado walikuwa hai,lakini walikuwa wakitembea juu katika moto wa Jehanamu. Mimi alishangaa jinsi mtu kwamba bado yu hai ,inawezakanaje kuwa katika moto wa Jehanamu haafu hapati maumivu ?.YESU Alisema kwa sababu  roho zao bado hazijajiunga nao huku kuzimu, kwamba ni sababu ya wao kuto hisia maumivu yoyote.Biblia  imekwisha kuandika kuwa wamehukumiwa tayari kwa sababu wao walifanya maamuzi katika akili zao na hakuna kitu au mtu yeyote anayeweza kuwaambia lolote litalowafanya kubadili mawazo yao.YESU Alisema wachungaji hao hawatakuruhusu uingie katika makanisa yao, kwa sababu wanajua kwamba  waumini  wao watabadiika na kuijua kweli.
WATAZAMIA MWEZI.
Niliona kundi  la watu walionyeshwa kwangu wakiwa katika moto wa Jehanamu. Watu hawa wana ang`aa kwenye vipaji vya nyuso na mimi nilimwuliza Bwana , watu hao walikuwa ni akina nani?,Naye YESU Alisema hawa ni watu ambao kabla ya kuomba, huangalia kwa mwezi na nyota. Alinionyesha andiko hilo lilosema hayo ; Kumbukumbu la torati 4:19-“19 tena usije ukainua macho yako hata mbinguni, na ulionapo jua, na mwezi, na nyota, jeshi la mbinguni lote pia, ukashawishwa na kuviabudu, na kuvitumikia, ambavyo Bwana, Mungu wako amewagawanyia watu wote chini ya mbingu zote.”. Neno la MUNGU lina laani hayo.

MAPADRI NA MASISTA
Niliona pia baadhi ya watu wamevaa misalaba mikubwa juu ya vifua vyao .Moja wao alikiri kwamba alikuwa Padri na kwamba yeye ni muongo na alidanganya kwa watu kuwa yeye ni bikira, lakini alikuwa na mke na watoto kwa siri. Alikuwa akiomba msamaha. Niliona dada ambaye ni sista naye na uhalifu huo. Bwana YESU akasema, Yeye hakuagiza mtu yeyote asiolewe au asioe, lakini hao watu walikuwa wanafiki.

WANAWAKE WANAOVAA SURUALI,VITO NA BANDIA(wanao paka makeup).
Kulikuwa na swali nilisha wahi kumuuliza Bwana; kabla ya sasa na yeye aliahidi kunijibu mimi baadaye. Mimi nilimkumbusha YESU  wakati huo, na swali ni, kuwa kwa nini kuna wanawake sana katika kuzimu ikilinganishwa na wanaume?, Lakini YESU akamuita kwa ishara mwanamke mmoja kuja kunijibu mimi. Alikuwa ni mwanamke na hakuwa na nywele juu ya kichwa chake. mwanamke alianza kusema, 'Nilipokuwa duniani, Sikujua ni dhambi kwa mwanamke kuvaa suruali, kwa mwanamke kupaka rangi midomo yake kwa sababu ni damu za ndugu zetu humwagwa na shetani katika ajali za barabarani na kwamba kuvaa weave-on hutoka kwa mkuu wa joka(dragon), kwamba kuvaa vito imekuwa na kugeuka kuwa sanamu ''.

Mimi sasa nilijiuliza maana yake nini?, mbona wewe hapa hujavaa weave-on sasa .Yule mwanamke akanijibu na kunipa habari juu ya kifo chake,Kuwa alivyokufa tuu  ndipo joka alikuja kutoka ardhini na kumuondolea weave -On kutoka kichwani mwake kwa sababu ni mali yake.


Suala la vito lilinipa wasiwasi na mawazo kwa sababu hata mimi nimejikusanyia vingi duniani, mimi sasa Nikamuuliza Bwana kwa kunukuu ; Kutoka 3:21-22. Kwamba wewe ndiye ambaye uliwataka wana wa Israeli kuchukua vito vyao , na kuvaa mambo hayo. Alitabasamu na akaniuliza kusoma Kutoka 32: 1-6-. wana wa Israeli walipomwomba Haruni awatengenezee mungu kutoka pete,mnikufu yao,hereni zao na vito vingine vyao .YESU alisema siku hiyo, kulikuwa na machozi mbinguni kwa sababu 'Nilijua ni gharama niliyoitumia Mimi kuleta watoto wangu Isreal kutoka Misri' '.
Alisema, ilikuwa tangu siku hiyo kwamba Mungu aliilaani chochote vito, ama dhahabu au fedha au kitu chochote kuweka kwenye kupamba mwili kwa sababu, Baba yangu ni Mungu mwenye wivu. Yeye akaniagiza kutoa maandiko haya kwa kia binaadamu-Isaya 3: 16-24, Ezekiel 7: 19-21, Mithali 6: 16-19, Ufunuo  20: 15, Ufunuo 21: 8 -21.

Alisema kuna sababu mbili(2),zinazopelekea kuwa dhambi kwa viito kwanza viito hunajisi mwili wako ambalo ni hekalu la Roho takatifu. Pili, mambo haya kuwapotosha kwa kuwatongozesha wanaume/watu na kuwaleta kuzimu. Wanaume wana nguvu  lakini wengi wao wamekuwa wametongozwa na kupelekwa kuzimu.
Alisema wakati wanawake wanapovaa mambo haya na wanaume wawaonapo, wao huwa na tamaa na kuendelea katika mchakato wa kuzidi kuwatamani na kwa kufanya hivyo wanakuwa na hatia itayoweza kuwapeleka kuzimu.
Mwanamke ambaye atasababisha mtu mwingine aanguke, yeye pia hawezi kutoroka kuzimu. Yesu alisema mwanamke pekee katika Biblia ambaye alikuwa akipaka uso wake rangi  ni Yezebeli. Alisema tunapaswa kurudi na kuiga mfano wa kanisa la Deeper Life Bible Church jinsi wanavyo vaa kama unataka kuingia mbinguni.


Bwana YESU pia anapenda kujulisha kwamba Yeye hajawahi kuwa chanzo cha ajali yoyote na wakati wowote ,Bali Shetani anapohitaji damu ya kutengenezea lipstick, anatupa  jiwe kwa kusababisha ajali. Karibu wakati huo huo, kwa vile hakuna kitu kinachofichika kwa Mungu,Basi MUNGU hutuma malaika ili kuepusha ajali hiyo iwe ni baharini, hewani au juu ya barabara.


Nao mawakala wa shetani waliojipanga kusababisha ajali huwafuata  Malaika ndani ya gari na kuuliza, “ni hawa watu unataka kuwaokoa? ,Wanawake katika suruali, na makeups? Nk”. Malaika huamua kwenda kwa wanaume ili kuwaokoa lakini hukosa wa kuwaokoa kwa kuwa baadhi yao huwa na cheni,hereni,pete  ambavyo hivyo vyote ni mali ya shetani.

Malaika huyshindwa kuokoa watu hao kwa kuwa watu wote wana vitu ambavyo ni vya shetani. Matokeo yake itakuwa ni ajali na waadilifu na wasio waadilifu wanaangamia.
YESU  aliniambia mara nyingine inapotaka kutokea ajali watu huokolewa kwa sababu watu hao hawakubeba chochote cha shetani iwe nje ya mwili au ndani ya mwili. Yeye alisema kitu chochote kichafu hakita ingia mbinguni kama vile uovu, uchoyo, uongo, wivu ambayo umekithiri sana miongoni mwa wanawake.
YESU aliniambia kuwa ni damu ya ndugu na dada zetu ambazo hutumika katika kutengenezea hizi make-ups na vipodozi mbalimbali.

YESU alinionyesha tukio moja inavyoonekana eneo la tukio duniani. Kulikuwa na mzee wa kanisa, yuko tayari na akimsubiri mke wake nje katika gari, wakati mke alikuwa akijipaka make up kwa muda mrefu. Walipofika kanisani na mwanamke yule alikuwa nje tena bado kuweka make up kwa kugusa gusa kumalizia make up yake.

Bwana YESU akaniagiza niuambie ulimwengu kwamba tarumbeta itapigwa hivi karibuni .Bwana akanichukua kunionyesha makutano ya njia ambayo inaongoza kwenda mbinguni na kuzimu na nilipo kuja na kuona umati wa watu unaotiririka ndani ya kuzimu!.Hata hivyo nilivyokuwa pale kuna kitu cha ajabu kilitokea mbinguni. Kulikuwa na mabadiliko ya ghafla mbinguni kote na mimi nikajifunza kwamba ni Mtakatifu anakuja mbinguni. Mimi nilikuwa natarajia kuwa sasa atakuwa ni mwanamke, lakini ole, ni mwanamume.


Alikuwa tayari ana taji zuri lenye utukufu mkubwa na alikuwa akiimba haleluya alipofika kwenye geti la mbinguni lilifunguka naye akaingia bila kujisumbua kuja na kumshukuru na Yesu akasema atakutana naye wakati wa ibada ya jioni.

Bwana aliniambia Sababu ya pili kwa nini nilikuwa natakiwa kwenda kuzimu;nayo ni kuipenda dunia katika kuvaa kwangu, lakini Namshukuru Mungu kwa sababu ya huruma yake, Alisema mimi lazima  niueneza ujumbe huu kwa jamii yote. Alisema kuna malipo kwa kila mtu.Kila mtu anayetaka kuja mbinguni lazima asamehe kila mtu, na kutoa angalau saa moja la ibada kwa Mungu kila siku.
Wanapaswa kumpenda kila mtu, hata mwenda wazimu katika mitaa, kwa sababu hajafanywa hivyo na Mungu. Kumpenda ndani kwa moyo wako kwa sababu yeye bado ana roho ambayo Mungu ana nia nayo.Bwana pia alisema, '' Waambie wajenge nyumba zao mbinguni kwa sababu hakuna mpangaji huku mbinguni.Kama huja maliza nyumba yako iliyo mbinguni , huwezi kufika mbinguni. ''

Bwana YESU alinionyesha mtu aIiyemaliza nyumba yake chini ya miezi 6 .Mimi nalimwomba Mungu aniambie ni jinsi gani aliweza,Naye YESU aliniambia kuwa mtu huyo badala ya kutoa asilimia10% kama fungu la kumi yeye alitoa 90%. (Mtu huyo katika alikwenda katika familia yake, iliyopo kijijini na kuwahubiria injii nao wakaokoka na kubadilishwa wote.YESU Alisema kuna mambo mawili ambayo yanaweza kufanya mtu aweze kujenga nyumba yake huku mbinguni kwa haraka; nayo ni kutoa kwa kazi ya Mungu na kuleta watu kwa KRISTO. Nilikuwa nina hofu ndani ya moyo wangu  hofu kuhusu hatima ya huyu mtu kwa yale aliyoyafanya asije akaikosa MBINGU, ila Bwana YESU akanihakikishia kwamba kama mtu huyu anaendelea hivyo basi atamtuma malaika wake ili daima amuongoze katika haki milele.

WASIOTOA ZAKA
Wale ambao wanakataa kulipa zaka zao watakuwa wamefungwa kabla ya kutupwa kuzimu. Mwambie wachungaji kwamba wakati ukitoa nyumba za waumini nakuziwekea wakfu kanisani, ni lazima kwanza mtu huyo hujitolea mbinguni na ni kwa njia hii kwamba Bwana atawapa neema ya kujenga moja mbinguni.
Waambie  watenda maovu  wanipe nafasi ya baba na nitawapa zaidi ya shetani anavyo wapa.
WATENDA KAZI KANISANI
Mwambie wafanyakazi wa kanisa ambao wamechukuliwa muda wao na ndoa zao na watoto kuwa ni wakati wa kunipa nafasi na kurudi na upendo wao wa kwanza. Alisema kuwa ndiyo sababu kubwa wasichana wasasa huangaika kutafuta  waume siku hizi, kwa sababu wale aliowapa waume wameruhusu na wamewapa waue zao muda wangu wote na  kuchukua upendo wao kwa Bwana.

WAABUDU JUMAPILI TUU
YESU Alisema siku ya Jumapili tuuu, waabudu Jumapili tuu hawaji mbinguni, kwa sababu mbinguni si kwa ajili ya watu wavivu. Kawaambie wawe wafanyakazi, kwa sababu kama ni wafanyakazi wasinge kuja kanisani mara moja tu kwa wiki. Aliuliza kwa nini ungependa kutoa kujipa mwenyewe siku 6 katika juma na kutoa  siku moja tu kwa MUUMBA wako. Alionya wale wachelewaji kanisani ndiyo sababu ya kutokuwa na shuhuda zaidi katika kanisa.

YESU alisema kila wakati kunapotangazwa matangazo kanisani, Malaika nao huandika na kwamba ni nini itakuwa kutumika kwa Mungu na kuwahukumu watu.YESU alisema Malaika wa Mungu huwapo karibu dakika 15 kabla ya mpango mlioupanga kama ni ibada au nini nao wanakuwa na mabakuli nje ya miujiza kwa waiowahi mapema na kwa wakati.

Malaika wengine huja mwishoni mwa ibada wakati baadhi ya wakristo huondoka kugawa miujiza kwa ambao hawajatoroka. Hiyo ndio inatoa sababu ya kufa kwa miujiza katikainaeleza ukosefu wa makanisa ya leo.YESU anasema kwamba, ni wae tuu ambao ni watii ndio hupokea miujiza kwa kuwa Hata kama Mungu akitaka kubariki watu wasio watiifu, shetani mshitaki wa ndugu huja na kuongeza pingamizi kutokana na kosa mtu alilotenda. Kama ikiandikwa katika kanisa lako kwamba unapaswa kuzima simu wakati wa ibada, hiyo inakuwa dhambi kwenu kama wewe ukienda kinyume na agizo hilo. Alisema kama si kuandikwa una adhabu mdogo.

WENYE MAJINA YA MIUNGU
Bwana pia anaonya wale ambao majina yao ni yenye mahusiano na miungu wayabadilishe hayo kwa sababu kama una jina kama hilo halitaweza ingia rekodi yoyote mbinguni. Majina haya si ya kumtukuza Mungu. Kama unadai kuwa ni jina la familia, basi sasa beba jina lako mwenyewe jina la kibinafsi. Hata aliniambia maana ya jina langu.

Pia alionya kuwa lipstick, cortex, mini-skirt/sketi fupi, mapambo, shanga, suruali kwa wanawake, minyororo, vikuku, mapambo, jewelries, na wote wavao mavazi ya kidunia waachane navyo mbali. Alionya kuwa uamuzi wa kwenda mbinguni upo kwako wewe binafsi na kwamba kama utaamua kutokuja mbinguni, Yeye YESU ana viumbe vya kutosha kwamba kumwabudu Yeye milele.

Mimi sasa nilimuuliza Bwana YESU kwamba,Mbona katika maandiko yanaonyesha kuwa Mungu anaangalia tu roho na si mwili sasa suala la nini sisi kuhusu kuvaa? ,Yeye YESU aliniambia nikafungue Warumi 12; 1 niliyoyatenda na kusoma: 'nawasihi Basi ndugu kwa huruma zake Mungu itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana. '' YESU alisema: "Kila sehemu ya mwili wako umenibeba mimi ''.

Nikamueleza habari ya huduma ambapo nilikuwepo kuwa ilikuwa haikui kabisa,Ndipo Bwana akaniambia nijitoe kwenye huduma na wachungaji ambao hawaelekei popote,Pia YESU aliniambia ananituma kwa wale wote wanaowateta wachungaji kuwa yeye YESU ndiye aliyewaita na Yeye ndiye atakayewahukumu na sio ninyi.
WAZINZI
Bwana pia akaniagiza kuwaambia wote wanaomfanyisha ngono waache kufanya hivyo. Nilisimama nikashtuka sana kwani sikuweza kuelewa na jinsi ya kuifikisha kwa watu .Mimi nikamuuliza Bwana jinsi kitu hiki kinawezekana je ?,. 'Bwana, upo mbinguni na sisi ni katika dunia, jinsi gani sisi tunafanya ngono na wewe? Bwana YESU alielezea. Wakati wanandoa wanapofungishwa ndoa iwe ni mahakamabi, jadini,au kanisani, daima kuna tangazo huwa linatangazwa kuwa: 'Alichokiunganisha Mungu amejiunga pamoja, basi binadamu asikitenganishe.’

Kwa sababu ya tangazo hilo, wakati wowote mume na mke wanapotaka kukutana, mimi hujiudhuru kwao na wanapomaliza kukutana  mimi hurudi tena ndani yao haraka (wao ni hekalu yangu na wao undani yangu) ili shetani asipate nafasi ya kuwaangamiza. Sasa fikiria mvulana na msichana wakija pamoja kujamiiana na wao si jawaunga katika ndoa takatifu, na wao wanatakiwa kuwa hekalu yangu hapo inakuwaje ?.

Hiyo ina maana kila wakati wao wanaposhiriki tendo la ndoa na huku hawajafunga ndoa nami huwa bado nimo ndani yao hivyo wao hunitenda ngono Mimi. Kawaambie Mimi nimechoka kutendeshwa dhambi! ,Kuwaonye kwa sababu nataka kuanza hukumu juu yao, hasa wale walio Wakristo na kukiri kubeba Jina langu. Waache tena waondoke kanisani kwa sababu wao huzuia sala. Bwana YESU pia aliwahimiza wale walio katika ndoa kukaa na kuwa na furaha ya urafiki, kwa sababu ndiye aliyeteuliwa na Mungu na ni kwa njia hiyo kwamba urafiki zaidi na ukaribu unaweza kuwa zaidi akamilishe kati ya wanandoa. Basi mimi naweza kusema nao. Bwana alisema.

Baada ya kihistoria hii ya ufunuo, mimi nilirudi tena duniani. Bwana YESU aliniambia ni muda wa kwenda na mimi nikamuomba anihakikishie kuwa dhambi zangu zote zimesamehewa. Yeye kisha ghafla nilimuona Yeye mwenyewe juu ya msalaba. Mimi  kwa haraka nikainamisha kichwa changu chini ,Naye YESU alianza kukusanya damu kutoka sehemu zote za mwili wake, Yeye baadaye akamwaga juu ya kichwa changu .Kutokea hapo alianza kuniita  binti yangu na baadaye akajirudi kwenye utukufu wake.


Biblia ni ya kweli na iwazi, sisi ni wenye dhambi, na yeyote atakayeomba kwa jina la Bwana YESUKRISTO, ataokoka. Yesu alisema Kama ukikiri nami mbele ya wanadamu, hadharani, ndipo namimi nitakiri jina lako mbele ya Baba yangu aliye mbinguni na Malaika Mtakatifu. Lakini kama wewe atakayenikana mbele ya watu, nami nitakukataa wewe mbele za Baba yangu. Kumbuka, Yesu alitundikwa uchi juu ya msalaba, katikati ya watu hata kwenye masoko, Yeye alitundikwa huko kwa ajili yako wewe na mimi ,kwa ajili yetu.Alivumilia aibu yako. Kama unataka kufanya kuwa uamuzi ili kumpokea  Bwana Yesu Kristo, kisha kusema sala hii:

"Mungu naamini katika wewe. Wewe ni Muumba wangu. Mimi ni mwenye dhambi. Nimekosa kwa njia nyingi, makusudi, na bila kujijua. Nimekuwa nikianguka, nimekosa alama zako ee Bwana.. Mimi nina nilibadilika na dhambi. Sasa Yesu mimi naamini katika Wewe. Wewe ni Mwana wa milele wa Mungu. Wewe ni kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu, aichukuaye dhambi yangu. Ninaamini ulikufa msalabani, na kumwaga damu isiyo na hatia yako kwa hatia yangu binafsi. Naamini ulizikwa na siku ya tatu ukafufuka. Wewe u hai milele zaidi. Nakuita Wewe uwe Bwana wangu. Nakuita uwe  Mwokozi wangu. Nakupa maisha yangu. Mimi nitakupenda WEWE, na kukutumikia Wewe siku zangu zote za maisha yangu. Mimi ni wa wako, sehemu nzuri, sehemu mbaya, sehemu za dhambi, mipango yangu yote, ndoto zangu zote, mimi natoa kila kitu kwako. Utakalo lifanyike ndani yangu lifanyike Bwana. Naamini nimeokolewa. Wala si kwa matendo mema, bali kwa imani, kwa kukutegemea Wewe. Katika YesuKristo Naomba. Amina.

Najua umebarikiwa kwa shuhuda hii ni vyema ungewashirikisha na wengine ili nao wabarikiwe hasa wale Wakristo waliokufa ili waweze kuamk Kiroho na MUNGU naye atakubariki.


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...