JINSI YA KUSALI NA KUOMBA MUNGU !


Hatua saba(7) unazopitia pindi uombapo.
Ni vizuri kujua namna ya kusali na kuomba MUNGU kwa kuwa sala na maombi ndio funguo kuu kwa mkristo kupokea kutoka kwa BWANA.

Imeandikwa “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.”- Wafilipi 4:6


Sio maombi ilimradi maombi ,bali ni maombi ambayo MUNGU anajibu.





Hatuendi tuu kuomba kile tunachotaka bila utaratibu na tukapata bali kuna hatua za kumuomba MUNGU na kwa utaratibu utaowezesha kuomba MUNGU sawa sawa na kupokea kutoka kwake.


Vitu vya kuzingatia kabla hujaanza maombi ni:-

       1.Unatakiwa uwe na neno la MUNGU linalothibitisha  ombi lako kwa MUNGU.
Kabla hata ya kuanza kuomba jaribu kutafuta neno la MUNGU ambalo litathibitisha ombi unalolipeleka kwa BWANA.


Mfano: “unataka kumuomba MUNGU upate nyumba/ mtaji / fedha au upate utajiri” basi muendee MUNGU ukiwa na mstari kama ilivyoandikwa


2 Wakorintho 8:9 -Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.

Ukamuomba MUNGU kwa hoja kuwa umeasema ulifanyika masikini ili sisi tuwe matajiri ,leo naomba ule utajiri ambao kwa huo wewe ulifanyika kuwa masikini”


 Au waweza kutumia huu mstari Kumbukumbu la torati 15:4 “Lakini hawatakuwako maskini kwenu; (kwa kuwa Bwana atakubarikia kweli katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako, uimiliki, iwe urithi wako;)”

Nawe ukamuomba MUNGU kwa hoja ukimueleza kuwa “MUNGU wangu ni ahadi yako toka awali kuwa utanibarikia mimi na hapatakuwepo masikini kati ya wale wanaokuabudu nakuomba uniondolee huu umasikini nilionao”.

Kuna maneno ya MUNGU mengi mengi waweza kuyatumia  tofauti na hayo ambayo unaweza kuyatumia kuthibitisha ombi lako kwa MUNGU kwa kuwa neno la MUNGU lina pumzi hai ya MUNGU.

Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;”-2 Timotheo 3:16.

MUNGU anaangalia neno lake ili alitimize,nawe watakiwa umkumbushe neno  lake linaloshawishi kuwa ombi lako. 

Imeandikwa  Maana mimi ni Bwana; mimi nitanena, na neno lile nitakalolinena litatimizwa; wala halitakawilishwa tena; maana katika siku zenu, Ewe nyumba iliyoasi, nitalinena neno hilo na kulitimiza, asema Bwana MUNGU.- Ezekieli 12:25

Tena Imeandikwa “Nanyi mkiwa katika kusali, msipayuke-payuke, kama watu wa mataifa; maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu ya maneno yao kuwa mengi.”- Mathayo 6:7 .

            2.  Mahali unapotumia kuomba MUNGU
Unapotaka kuomba maombi yako binafsi chagua mahali pazuri patulivu uweze kuomba pasipo usumbufu .

Imeandikwa “Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.” -Mathayo 6:6




Kama katika sehemu unayokaa kuna kelele na vurugu ,basi waweza kufungulia redio za injili kwa sauti kipindi wewe unasali,au simu yako au redio ikiimba nyimbo za injili huku wewe ukisali. 


Hapo utakuwa umeepuka kelele zitazokuhamisha kwenye uwepo wa MUNGU.

         3.  Kumbuka kutumia jina la YESU pindi uombapo
Zingatia kuomba kwa MUNGU kupitia jina la YESU.Imeandikwa “Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana.” -Yohana 14:13.

Usiombe kupitia jina lolote bali katika jina la YESU ndilo tulilopewa lenye nguvu na mamlaka pekee ya kufanya upokee chochote unachoomba kutoka kwa BWANA.

Kuna hatua kwa hatua unapotaka kusali au kumuomba MUNGU.
Sio kwa kukariri sala bali Ili maombi yako yafike kwa MUNGU na kupata majibu vyema  basi ni lazima uombe kwa mtiririko na kwa mpangilio unaotakiwa.

Imeandikwa “Nanyi mkiwa katika kusali, msipayuke-payuke, kama watu wa mataifa; maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu ya maneno yao kuwa mengi”-Mathayo 6:7.

Kwa hiyo kuna utaratibu wa kuomba vyema na sio kuongea maneno tuu pasipo maana yoyote wala mpangilio.

Hatua saba(7) na mtiririko unaotakiwa kwenda nao unapotaka kuomba nazo ni :-         

1.KUMSIFU/KUMSHUKURU
Unapoanza kusali anza kwa kumsifu MUNGU kwa kukupa uhai/uzima /afya na hata mshukuru kwa kukupa nafasi ya kusali pia.Mtambulishe MUNGU unayemuomba kwa kuwa kuna miungu wengi ,tena mtambulishe kwa majiina ukimaanisha 

Mfano:wewe ambaye NIKO ambaye NIKO ,MUNGU aliye hai,MUNGU wa miungu ,MUNGU wa israel,MUNGU wa isaka ,yakobo,ibrahim.

Imeandikwa “shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.” -1 Wathesalonike 5:18 .

MUNGU anastahili kusifiwa na wenye dhambi na wasio na dhambi.MUNGU anastahili kusifiwa hata kama uanaona hajakusaidia kitu kwa kuwa yeye MUNGU hutuchagulia kilicho bora kuliko tufikiriavyo.

Huku ukijinyenyekeza na kuona MUNGU ndiye yeye pekee unayemtegemea kupata msaada kutoka kwake.

2.KUTUBU DHAMBI ZAKO ZOTE.
Hatua ya pili ni kutubu dhambi zako zote ulizowahi kuzifanya kama unazikumbuka unataja moja baada ya ingine.Omba msamaha hata kama unajihisi au unajiona kuwa wewe ni mtakatifu,Tubu kwa ajili ya dhambi unazozijua na zile usizojua !



Imeandikwa “Twajua ya kuwa Mungu hawasikii wenye dhambi; bali mtu akiwa ni mcha Mungu, na kuyafanya mapenzi yake, humsikia huyo”-Yohana 9:31


“15 Nanyi mkunjuapo mikono yenu, nitaficha macho yangu nisiwaone; naam, mwombapo maombi mengi, sitasikia; mikono yenu imejaa damu.”-Isaya 1:15

Hiyo inamaana maombi ya mwenye dhambi ni kelele kwa MUNGU na hayasikilizwi bali mtu anapotubu kwa kumaanisha kuacha hayo maovu basi naye MUNGU husamehe!. “9 Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.”-1 Yohana 1:9

Unapoomba msamaha basi kumbuka kusamehe watu waliokukosea kwa kuwa MUNGU hata kusamehe mpaka usamehe waliokukosea.

Imeandikwa “Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi.” -Mathayo 6:14 .Ukiomba msamaha utakuwa unanafasi kama mtoto wa MUNGU kusikiwa ombi lako KWAKE.

3.KUMSHUKURU/KUMSIFU MUNGU.
Hatua ya tatu ni kumshukuru na kumsifu  MUNGU kwa kukupa msamaha wa dhambi kukupa nafasi nzuri kama mtoto wa MUNGU.

Imeandikwa“na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo;”- Waefeso 5:20

Hapa unamshukuru kwa kuwa amekusamehe pale ulipo muomba msamehe, na una msifu kwa kuwa amekupa msamaha na nafasi nzuri yakukusikiliza kwa lolote umuombalo.




4.KUOMBA OMBI LAKO SASA
Imeandikwa “Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia.”-1 Yohana 5:14

Hatua ya nne ni  kuomba ombi lako kabisa,Hapa unaweza ukaambatanisha maombi matatu  kwa imani huku ukiongozwa na Roho wa MUNGU.Kwa kuwa tayari unakuwa na nguvu za MUNGU.


Imeandikwa “Hata sasa hamkuomba neno kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapata; furaha yenu iwe timilifu”- Yohana 16:24.

Peleka ombi lako kwa MUNGU huku ukiwa na mstari au neno la MUNGU linalothibitisha kupata ombi lako.

Mfano:Unataka umuombe MUNGU akuponye na magonjwa  basi waweza tumia mstari usemao kutoka  Isaya 53:5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.

Kwa hiyo unapomuomba MUNGU  unaenda na hoja kuu ukimwambia “Eee BWANA kwa kupigwa kwako YESU sisi tumepona nakuomba niondolee magonjwa haya!”

Katika hatua hii ya nne(4) una mamlaka ya YESU tena waweza hata kuamuru mapepo na nguvu za giza au kufunga kila kazi za shetani za uharibifu na ikafanikiwa.

5.KUSHUKURU NA KUMSIFU MUNGU.
Hatua ya tano(5) ya maombi yako unatakiwa umshukuru MUNGU na kumsifu kwa kuwa MUNGU wetu hupenda kusifiwa na kushukuriwa hivyo unapaswa kumsifu na kumshukuru  MUNGU

 kwa ajili ya maombi yote uliyoyapeleka kana kwamba umepata kile ulichoomba ingawa bado katika mwili huoni kitu.
Imeandikwa “Mshukuruni Mungu wa mbingu; Kwa maana fadhili zake ni za milele”- Zaburi 136:26

6.KUJITABIRIA NA KUKIRI USHINDI KABLA YA KUTUKIA
Hatua ya sita (6) ya maombi yako  ni ya kujitabiria na kukiri ushindi kabla hujauona.Kiri kwa kusema yote kwa furaha kama umeshayapata kabisa.Imeandikwa “Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.”- Mathayo 12:37.




Wewe mwenyewe ni nabii wa maisha yako mwenyewe.







Imeandikwa “28 Hata itakuwa, baada ya hayo, ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu, waume kwa wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono; ”-Yoeli 2:28

Mfano:Ulikuwa unamuomba MUNGU upate mpenyo wa kibiashara au akutoe kwenye umasikini basi anza kukiri na kujitabiria kwa kusema asante MUNGU kwa kuwa utanifanya niwe tajiri wa aina yake ,najiona nikisaidia watu wasiojiweza, leo BWANA amenikubalia ombi langu nitakuwa na fedha nyingi zisizo za kawaida.

Jitabiri makubwa kadiri uwezavyo huku ukiamini kila unachojitabiria na kukikiri .Usiogope kujitabiria mambo makubwa kwa kuwa si wewe ambaye unaenda kuyafanya bali ni MUNGU mwenyewe.

7.KUSHUKURU  NA KUMSIFU MUNGU
Mshukuru MUNGU kwa sadaka ya fedha ya kuifanya kazi ya BWANA.
Hatua ya saba(7) ni kumshukuru na kumsifu MUNGU kwa kukuwezesha kufanya maombi vyema teka mwanzo mpaka mwisho.Mshukuru MUNGU kwa ROHO wake mtakatifu aliyekusaidia kusali ipasavyo!.


Kama yalikuwa ni maombi ya mfululizo yaani maombi ya kitu fulani labda ulikuwa kwa muda mrefu unaombea nchi,labda familia,labda ndoa yako au chochote kilichokuwa kina kusumbua kwa muda mrefu ,ikiwezekana nenda kanisani au katika watu wenye matatizo na kutolea sadaka ya kumshukuru.


Imeandikwa “Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru; Mtimizie Aliye juu nadhiri zako”- Zaburi 50:14

Kwa kutoa sadaka ya shukurani kwa ajili ya lile jambo ulilomuomba MUNGU kwa imani.

Itakuwa vyema zaidi kwa kuwa kwa sadaka hiyo utakuwa umeweka kumbukumbu kwa MUNGU na hatasahau kulijibu  ombi lako kamwe.

24 comments :

  1. MUNGU hakubariki sana mtumishi Wa mungu

    ReplyDelete
  2. Replies
    1. Ubarikiwe na MUNGU, nakuomba uzidi kufuatilia mafundisho mengineyo.

      Delete
  3. Amen mafundisho mazuri yamenibariki sana na kukupa njia na muongozo jinsi ya kuomba kwa Mungu wangu. Barikiwa sana.

    ReplyDelete
  4. Mungu akubariki sana, pia nina swali Je, ni siku hipi inayo faa sana mtu kuwa kwenye mfungo

    ReplyDelete
    Replies
    1. Amina.Siku inayofaa sana kufunga ni siku yoyote ile,ila itafaa zaidi siku yenyewe uwe na na muda wa kuomba, kusoma neno la Mungu na kulitafakari kwa utulivu.Kitu kikubwa cha kuzingatia ni kuongozwa na Roho mtakatifu katika kila kitu unachokifanya.

      Delete
  5. Ubarikiwe Sana mtumishi wa Mungu

    ReplyDelete
  6. Asante Mtumishi wa Mungu, nilikuwa sijui kuomba kwa Mpangilio lkn kwa ninamshukuru Mungu nimejua. Ubarikiwe sana mtumishi

    ReplyDelete
    Replies
    1. amina, Utukufu kwa MUNGU.Nakuomba uzidi kufuatilia masomo mengine mbali mbali ili uzidi kukuwa kiroho.

      Delete
  7. Mungu akubariki mno maana nimepata Jambo... Mtumishi nisaidie kwa ufupi tofauti ya kuomba na kusali 🙏

    ReplyDelete
    Replies
    1. Ni vitu vinavyo endana sana lakini kuna tufauti ndogo tuu.Kuomba lazima uwe unahitaji au shida binafsi ukimpelekea MUNGU, Lakini Kusali ni kumwendea MUNGU ukiwa huna hitaji bali kama desturi njema ya kumfuata MUNGU iinaandamana na kuabudu .

      Delete
  8. Leo nimejifunza kitu kipya, kwanza nikuomba kwa mpangilio alf kuacha kulalamika wakati wakuomba asante sana na ubarikiwe

    ReplyDelete
  9. Nimejifunza Namna ya kuomba ubarikiwe mtumishi

    ReplyDelete

Andika maoni yako hapa !! ... You may comment here !!!

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...