Showing posts with label MBINGUNI. Show all posts
Showing posts with label MBINGUNI. Show all posts

Mtu mmoja(1) akiingia mbinguni, watu elfu moja(1000) wanaingia kuzimu-.Ushuhuda na Mchungaji Park Yong Gyu.


Ushuhuda wa Mbingu na Kuzimu, 1-1000, na Mchungaji Park Yong GyuMchungaji Park alikuwa amefariki kutokana na shinikizo la damu. Lakini kwa neema ya Mungu, maisha yake yaliongezwa kwa miaka 20 nyingine.
Hata hivyo, kwa miaka minne ya kwanza, hakuweza kuzungumza kutokana na hali yake. Alikuwa na umri wa miaka 50 hivi alipofufuliwa. Wakati wa kifo chake, Bwana alimpeleka mbinguni na kuzimu.Nataka ujue ukiwa na kiburi na majivuno utajiletea laana.
Nilikuwa na kanisa kubwa la washiriki 5000 lakini nilipigwa na Mungu kutokana na kiburi changu. Sasa namcha Mungu. Nilikuwa nikimiliki mali nyingi sana zenye kufikia thamani ya dola za kimarekani milioni 150, ambazo ni sawa na bilioni 349.86 za kitanzania.
Nilikuwa na magari matano(5) ya kifahari, Lakini baada ya haya niliyoyaona kwa neema ya MUNGU, niliyatoa yote na kuyagawa. Wokovu hauwezi kupatikana kwa mali zako bali kwa imani. Tafadhali, ninawasihi mashemasi, wazee, na viongozi wengine katika makanisa yao kumtumikia MUNGU chini ya wachungaji wenu kwa mioyo yenu yote.

Mnamo Desemba 19, baada ya kumaliza chakula changu cha mchana na nilipokuwa nikipumzika, nilianza kuhisi maumivu makali. Nilihisi kana kwamba nitakufa. Maumivu hayakuvumilika. Kisha nikapoteza fahamu. Nilipozinduka, watu waliokuwa karibu nami walisema miezi minne imepita.
Nilikuwa katika hali tete na nikiwa katika hali hiyo, daktari alikuwa amesema kwamba ningekufa.Kweli mara tu baada ya kufa, mara nikaona watu wawili wakiingia chumbani kwangu.
Lakini watu hawa walikuwa wameingia kwenye chumba changu kupitia ukuta. Nilipiga kelele, “Nani, wewe ni nani!! Nyumba yangu itabomoka ukifanya hivyo!!” Kisha malaika wakasema, “Sisi ni malaika tulioshuka kutoka mbinguni. Sisi tunatoka katika ufalme wa Mungu.” Nuru angavu ilimulika kutoka kwa malaika. Malaika waliniweka kati yao.
Nikauliza, “Mlikujaje ?”Walinijibu “Umekufa, familia yako inalia kwa huzuni nyingi huko,Baba MUNGU amependezwa kukupa muda zaidi wa kuishi. Ila kwa sasa, anataka kukuonyesha mbingu na kuzimu.
Atakuonyesha nawe utakwenda shuhudia kwa watu wa duniani. Kupitia ushuhuda wako idadi ya watu wanaoishia kuzimu ipunguzwe na idadi ya wanaokwenda mbinguni iongezeke. Hii itakuwa shabaha yako. Mungu alituagiza tukuambie usichelewe. Ukichelewa, hutaweza kuzuru mbinguni na kuzimu.” Malaika wa kulia kwangu alijitambulisha. “Ninafanya kazi kwa ajili ya Yesu katika ufalme wake. Yesu aliniita na kuniamuru nishuke duniani, akaniamuru nikupeleke mbinguni.
Kisha malaika aliyesimama upande wangu wa kushoto akajitambulisha. Alisema, "Wakati ulipozaliwa na hadi ulipokufa, nilikuwa pamoja nawe." Wakati huo, sikuelewa malaika alikuwa anamaanisha nini. Sasa najua. Yeye ni malaika wangu mlezi. Mimi nikasema, “Siwezi kwenda! Sitakwenda! Mimi ni mchungaji! Siwezi kukutana na Bwana katika hali hii ya kimwili. 
 
Ninataka kumwona nikiwa mtu mwenye afya njema. Pengine naenda kupokea karipio zaidi kuliko pongezi kutoka kwa Bwana. Nina kiburi mimi na majivuno, sasa nimelaaniwa na ni mgonjwa. Je, ninawezaje kuingia mbinguni? Ninaogopa sana. Tafadhali rudi mbinguni na umwombe Bwana aniponye. Kisha urudi na kunipeleka mbinguni kupitia ndoto yangu.
Tafadhali malaika omba rehema kwa niaba yangu.” Lakini malaika hawakusikiliza hoja yangu. Walinivua nguo zangu na kusema kwamba zilikuwa chafu sana kuvaliwa mbinguni. Kisha wakanivalisha gauni jeupe. Walishika mikono yangu na tukaruka moja kwa moja hadi mbinguni. Tuliruka kupitia mawingu na nilipotazama chini, niliona dunia ikizidi kuwa ndogo. Waliponiruhusu niende, ndani ya futi 3 kutoka kwangu, niliona Barabara ya Dhahabu isiyo na mwisho.
Tulikuwa bado tunaruka na kwa kasi kubwa. Kuangalia mbele, niliona mwanga mkali unaowaka. Sikuweza kutazama moja kwa moja kwenye mwanga.
 
 Nikawauliza wale malaika, Nuru inatoka wapi? Malaika akajibu, "Inatoka mbinguni." Nilipotazama mbele, nilijiwazia, “Lo! Ni kubwa!” Mbele yangu niliona makundi ya watu waliovalia mavazi meupe wakiruka mbele.
Niliwauliza wale malaika, “Ni nani hao?” Malaika akajibu, “Hao ndio waliokuwa wamemtumikia Mungu kwa uaminifu na kumtumaini Yesu kwa kutii na kufuata mwongozo wa Roho Mtakatifu kwa moyo wao wote. Miili yao imekufa duniani. Sasa ni nafsi zinazoelekea mbinguni.”Malaika mwingine akaendelea, “Kuna milango kumi na miwili(12) mbinguni. Wakati nafsi iliyookolewa inapokuja mbinguni, lazima iingie kupitia mojawapo ya milango hiyo.” Tulikuwa tumesimama kwenye lango la kusini lakini lilikuwa limefungwa.
Tulipokuwa tukingoja, nilimuuliza malaika, “Malaika, kwa nini lango hili halifunguki?” Malaika akajibu, "Ni kwa sababu huimbi wimbo wa kuabudu wa mbinguni." Niliuliza, “Malaika, mimi nilikuwa na kiburi na majivuno sana na matokeo yake nimelaaniwa na ugonjwa. Siko vizuri kuimba nyimbo za kuabudu za duniani. Je, ninawezaje kuimba nyimbo za kuabudu za mbinguni wakati sijawahi kuzisikia kabla?” Malaika akajibu, “Umesema kweli. Lakini bado unapaswa kujitayarisha kuabudu.
Wewe ni mtu wa kujivunia lakini jiandae kuimba.” Malaika walianza kuimba. Walipokuwa wakiimba, nilianza kuimba pamoja nao. Ikawa asili kwangu! Lakini basi, waliacha kuimba baada ya muda mfupi. Niliuliza, “Kwa nini umeacha kuimba? Nilikuwa nikifurahia.” Kisha nikagundua tayari tumeingia kwenye geti.
 
 Kwa jinsi mbingu ilivyo nzuri ,sitaweza kamwe kuelezea matukio ya mbinguni kwa maneno yangu ya kidunia. Nikasema, “Bwana! Asante sana! Ingawa, nilikuwa na kiburi na majivuno sana na kulaaniwa kwa ugonjwa, bado umenileta mbinguni ili kunionyesha pande zote. Tukio la mbinguni lililojitokeza mbele ya macho yangu lilikuwa lisiloelezeka. Kisha nikasikia sauti ya Mungu, “Mchungaji wangu mpendwa Park, Yong Gyu, ninakukaribisha.
Umefunga safari ndefu hapa.” Sauti ya Bwana ilijaa upendo na huruma. Nilijibu huku nikilia kwa machozi, “Bwana,….” Malaika walinisimamisha kulia mara moja, huku akisema “Umekuwa mchungaji kwa miaka 20. Je, hujui maandiko ya MUNGU?,kuwa mbinguni hakuna machozi. 
 
Tafadhali acha!” Sikuweza hata kulia.
Kisha Bwana akaniuliza maswali matano(5).
1. “Ulitumia muda gani kusoma Neno (biblia)? 2. Ulitoa kiasi gani cha sadaka?
3. Je, umehubiria watu mara ngapi?
4. Je, ulitoa zaka ipasavyo?
5. Ulitumia muda gani katika maombi?” Sikuweza kujibu swali la tano.
Bwana alinikemea kwa swali la tano. BWANA akaniambia “Baada ya kuwa mchungaji mkuu wa kanisa, umekuwa mvivu sana katika maombi. Na umekuwa na shughuli nyingi sana yakupasa ujue kuwa si kisingizio Kwangu!” Ilinibidi nitubu baadaye. Bwana aliendelea na kuniambia, “Malaika watakuonyesha sehemu nyingi mbinguni na kuzimu. Angalia kote kama unavyotaka. 
 
Utaondoka baada ya kushuhudia sehemu nyingi tofauti mbinguni na kuzimu.” Lakini Bwana hakuni ruhusu nione sura yake.Malaika walinipeleka kwanza sehemu tatu tofauti mbinguni. Sehemu ya kwanza, niliona watoto wadogo wakiishi pamoja. Sehemu ya pili ilikuwa mahali ambapo watu wazima waliishi. Sehemu ya tatu ilikuwa ni ya wale waliofika mbinguni kana kwamba kwa bahati bahati. Ingawa walifika mbinguni, walikuwa wameifika kwa aibu.
 
Watu wengi sana walikuwa wameniuliza watoto wadogo walikuwa na umri gani. Nadhani wanaonekana kufikia umri wa kusoma chekechea. Sikuweza tambua kuhusu jinsia ila kila mtoto alikuwa na malaika wake mtoto wa kuongozana nao. Mbinguni, roho nyingi zitakuwa na makao yao binafsi (Yohana 14:22). Hata hivyo, kulikuwa na wengine ambao hawakuwa na nyumba.
Nitalieleza hili baadaye. Isitoshe, watoto hawakuwa na nyumba zao binafsi pia. Niliuliza, “Watoto pia ni nafsi, kwa nini hawana nyumba zao wenyewe?”Malaika akajibu, “Kama vile watu duniani wanahitaji vifaa vya kujenga nyumba zao, sisi mbinguni pia tunahitaji vifaa vya kujenga hapa. Wakati mtu anatumikia kanisa na wengine kwa uaminifu kwa Bwana, matendo hayo yatakuwa nyenzo kwa ajili ya nyumba ya mtu mbinguni. 
 
Vifaa vinapotolewa, malaika waliopewa kazi ya kujenga nyumba ya mtakatifu wataenda kufanya kazi ya kuijenga. Watoto walio chini ya umri wa uwajibikaji hawajajenga nyenzo zozote za kujenga nyumba. Kwa maneno mengine, hawakuwa na wakati au nafasi ya kupata tuzo/nyenzo zao. Ndiyo maana hawana nyumba.”Niliendelea na maswali yangu, Na kuuliza “Nitafanya nini duniani ili kutoa nyenzo(materials) zaidi kwa ajili ya kujengea nyumba yangu?”
 
Malaika wakajibu, “Kuna mambo saba(7) ambayo mtu lazima afanye yatayosababisha mbinguni kupata vifaa/nyezo(materials) vitakavyo wezesha kujenga nyumba yake mbinguni.
1. La kwanza ni mkusanyiko wako wa ibada na sifa kwa Mungu.
2. Pili ni muda wako binafsi wa kusoma biblia.
3. Tatu, muda wako binafsi wa kusali.
4. Nne, muda wako ulioutumia kuhubiri injili kwa watu.
5. Tano, sadaka ya uaminifu ya mtu kwa Bwana.
6. Sita, zaka zao za utii kwa Mungu.
7. Mwisho, muda wao walioutumia kutumikia kanisa kwa njia yoyote ile.
 
Haya ni matendo au kazi za utii ambazo ndani yake mtu hukusanya nyenzo/vifaa kwa ajili ya kujengewa makao yao ya mbinguni. Ikiwa moja itakosekana katika maeneo haya, hawatakuwa na vifaa vya kujenga nyumba yao.Kulikuwa na watu wengi mbinguni na wasio na nyumba.
Wengi ambao hawakuwa na nyumba walikuwa wachungaji, mashemasi, wazee, n.k. Niliuliza kwa udadisi, “Watoto wanaishi wapi wakati huo?” Malaika wakajibu, "Wanaishi hapa." Nilipotazama pande zote, walikuwa wamekusanyika katika bustani yote ya maua. Bustani ya maua ilikuwa nzuri sana na harufu nzuri. Tukio hilo lilikuwa zaidi ya vile ningeweza kuelezea kwa maneno yangu. Sehemu ya pili ilikuwa kwa watu wazima waaminifu.
 
Kuna tofauti kati ya wokovu na thawabu. Mahali hapa palikuwa na nyumba nyingi sana. Nyumba zilijengwa kwa vito vya kupendeza na mawe adimu. Baadhi ya nyumba zilikuwa juu kama maghorofa ya juu zaidi duniani. Watu hao ambao walikuwa wamemtumikia Bwana kwa uaminifu walipokuwa wakiishi duniani walijenga nyumba zao kwa vito vya kupendeza na mawe adimu. Katika mahali hapa, watu wote walionekana wana wastani wa umri wa miaka 20 hadi 30.
 
  Hakuna wagonjwa, wazee, au vilema.Nilimuulizia mzee niliyemjua akiwa duniani, mzee anayeitwa, Oh, Im Myung. Alikufa akiwa na umri wa miaka 65. Alikuwa mtu mfupi sana, yaani mrefu kama mtoto wa darasa la 2 katika shule ya msingi. Alikuwa ameugua ugonjwa adimu unaoitwa rickets. Hata hivyo kwenye biblia, alikuwa amesoma hadi uzamivi(PHD). Alikuwa ameandika maoni mengi. Nilikutana naye Mbinguni, na hapo alikuwa mrefu na mzuri. Hakuwa mgonjwa tena bali mzima wa afya.
 
 Mbinguni ni mahali pazuri sana!! Mimi nimejawa na shauku kamili ya matarajio ya mbingu! Tafadhali amini ninachosema wapendwa!Sehemu ya tatu ni mahali ambapo waliookolewa kwa aibu wamekusanyika. Kijiji hiki ni kikubwa sana kwa ukubwa. Mahali hapa ni kubwa mara kadhaa kuliko mahali ambapo roho zilikaa mahali pa pili ambapo nyumba zimetengenezwa kwa vito na mawe adimu. Nilifika mahali hapa nikiendesha gari la dhahabu. Nilikuwa nimefika kwa kasi kubwa. Mahali hapa palikuwa mbali sana na sehemu nzuri za mbinguni. Niliwauliza malaika, “Naona nyika kubwa na mashamba. Kwa nini sioni nyumba?"Malaika akajibu, "Unachoona ni nyumba."
 
 Niliona nyumba kubwa pana za gorofa. Umbo la nyumba hizo lilinikumbusha banda kubwa la kuku au aina fulani ya ghala. Nyumba hizi zilikuwa chakavu sana. Kijiji hiki na nyumba zilikuwa kwa ajili ya roho zilizookolewa kwa aibu. Kulikuwa na nyumba nyingi kubwa zenye sura mbovu. Kijiji hiki ni kikubwa mara kadhaa kuliko mahali ambapo roho zilizotuzwa hukaa. Malaika akasema, “Je, unaziona nyumba mbili kubwa, moja kulia kwako na nyingine kushoto kwako?Nikajibu, “Ndiyo, ninaona.”Malaika alisema kwamba alitaka kunionyesha nyumba hizo mbili haswa. Alisema, “Nyumba za upande wa kulia ni kwa wale waliokuwa wachungaji duniani. Makao ya kushoto ni ya wale waliokuwa wazee wa kanisa duniani.”
 
 Tulipofika mbele ya nyumba hizo mbili, nikawaona wakiwa wacheshi.. Tulipofungua mlango na kuingia, Taya langu lilishuka mawazo yangu ya kwanza yalikuwa, ‘banda la kuku.’ Badala ya maelfu ya kuku wanaoishi kwenye banda lao, niliona nafsi. Malaika walinishauri niangalie kwa makini sana kwa sababu ningewatambua baadhi ya wachungaji waliokuwa maarufu huku duniani. Kweli nilitambua wachungaji wengi kutoka kwa historia.
 
 Nilimchagua mchungaji mmoja na kumuuliza malaika, “Ninamfahamu yule kasisi wa Korea! Ninajua jinsi alivyokuwa maarufu na kazi aliyokuwa amemfanyia Bwana. Kwa nini yuko hapa? Sielewi." Malaika wakajibu, “Hakuwahi kutoa vifaa vyovyote vya ujenzi kwa ajili ya nyumba yake.” Hii ndiyo sababu anaishi katika nyumba ya jamii.” Niliuliza kwa udadisi, “Hii ilifanyikaje? Kwa nini hakuwa na nyenzo yoyote? Malaika akajibu, “Alipokuwa mchungaji akitekeleza majukumu yake kama mchungaji, alipenda kusifiwa na watu. Alipenda kuheshimiwa. Alipenda kuhudumiwa. 
 

Hakukuwa na dhabihu na utumwa kwa upande wake.” Mchungaji huyu aliheshimiwa sana huko Korea na ni nguli(icon) kwenye historia ya Kikristo ya Kikorea. Lakini hakuwa na thawabu kubwa mbinguni !!. Mchungaji, tafadhali sikiliza! Inabidi uwaongoze watu kwa zaidi ya ibada za jumapili asubuhi. Lazima uwatembelee majumbani mwao. Lazima uwatunze maskini, viwete na wazee. Wachungaji ambao wametumikia bila kutoa maisha yao na kupenda kuheshimiwa hawana thawabu mbinguni. Baada ya kushuhudia tukio hili mbinguni na baada ya kurudi duniani, mara moja nilitoa mali yangu yote ikiwa ni pamoja na magari yangu matano ya kifahari. Maisha yetu ni ya kitambo tu. Katika Biblia, maisha ya wastani ni takriban miaka 70 hadi 80.Mungu pekee ndiye anayejua ni lini mtu atakufa. Mtu yeyote anaweza kufa kabla ya umri wa miaka 70 au 80. Nilikuwa nimeamua kutoa kila kitu hata nguo zangu.
 
 Watu niliowaona wamepokea wokovu kwa aibu walikuwa wachungaji, wazee, mashemasi, na waamini walei. Kulikuwa na umati wa wazee na mashemasi katika nyumba ile tambarare iliyochakaa. Lakini bila shaka, bado ni bora kuliko kuzimu. Hata hivyo, kwa nini mtu yeyote bado angependa kuingia mbinguni kwa njia hiyo? Sitaishia mahali pa aibu. Hata nguo zao zilikuwa chakavu. Ikiwa mtu anasema hawezi kufika kanisani kwa sababu hawana nguo nzuri, basi lazima umpatie baadhi. Ikiwa mtu huyo anasema hana Biblia, lazima umtolee.
 
 Ikiwa mtu anasema hana miwani ya kusoma, lazima umpatie. Ni lazima utoe chochote unachoweza pia ili mtu huyu aweze kuongozwa kwa Bwana. Wale wanaoishi katika nyumba bora zaidi ni wale ambao walikuwa wamehubiri mara nyingi.” Ni matakwa gani ili Wakristo wapokee makao hayo mazuri mbinguni? Hebu tuijadili. Kwanza, tunapaswa kuinjilisha kwa watu wengi zaidi kadri iwezekanavyo.Niliuliza swali muhimu. Je, tunapaswa kueneza injili jinsi gani? Malaika akajibu na kusema, “Fikiria kwamba kuna mtu asiyeamini ambaye hamjui Bwana. Mara tu unapoamua kuinjilisha mtu huyo, vifaa vya ujenzi vya nyumba zako vitatolewa. 
 
Unapowaombea wokovu bila kukoma, vifaa vingi vya ujenzi vinatolewa. Lazima uendelee kuwachunguza, kuwatembelea na kuendelea na uinjilisti wako. Kisha malaika akanisindikiza hadi mahali ambapo watakatifu waliishi katika nyumba nzuri. Hapa ndipo walipoishi watakatifu waliohubiri sana. Mahali nilipochukuliwa nilihisi kama mbinguni katikati mwa jiji. Katika historia ya Kikristo, kuna watu wanne ambao wana nyumba kubwa na nzuri zaidi.
 
 Malaika alinionyesha nyumba ya mwinjilisti wa Marekani D.L. Moody. Nyumba ya pili niliyoiona ilikuwa nyumba ya Mchungaji wa Uingereza John Wesley na ya tatu ilikuwa mwinjilisti wa Kiitaliano. Nyumba ya nne ilikuwa nyumbani kwa Mwinjilisti wa Kikorea Mchungaji Choi, Gun Nung. Watu hawa wanne wana nyumba kubwa zaidi mbinguni. Malaika waliniambia kwamba hawa wanne walikuwa wametumia maisha yao yote kuhubiri injili kwa watu hata hadi wakati wa kufa kwao. Ndani ya waumini wa Korea, kulikuwa na mwamini mlei ambaye alikuwa na nyumba kubwa. Muumini huyu mlei alikuwa amejenga majengo mengi ya kanisa pamoja na mali zake zote alikuwa amewapa maskini magunia elfu tatu ya mchele. 
 
Alisaidia kwa siri maelfu ya wachungaji na viongozi kwa kutumia fedha zake. Alisaidia wanafunzi wanaosoma theolojia au shule ya biblia na masomo yao. Pia alikuwa amemchukua mchungaji (umri wa miaka 65) nyumbani kwake na kumtunza vizuri. Kanisa lake mwenyewe lilikuwa limemfukuza. Kisha ghafla, nikasikia malaika akipaza sauti, “Nyenzo/vifaa vinakuja!” Nilimuuliza malaika aliye kulia kwangu kuhusu nyenzo hizo. Alijibu, “Vifaa hivi ni vya shemasi kutoka kanisa dogo ambaye anatoka nchini. Kwa kweli, yeye hupokea vifaa kila siku. Ingawa yeye ni maskini, yeye huja kwenye ibada ya asubuhi kila siku, anawaombea washiriki 87 wa kanisa kila siku.
 
 Anapomaliza kusali, anasafisha kanisa.” Nilimsikia malaika mwingine akipiga kelele, “Utoaji maalum! Binti wa shemasi amempa mama yake pesa kidogo aliyokuwa nayo. Hata hivyo, shemasi hakuitumia yeye mwenyewe. Alinunua mayai matano na jozi mbili za soksi kwa mchungaji wa kanisa. Ingawa inaweza kuonekana kuwa sadaka ndogo, alikuwa ametoa vyote alivyokuwa navyo kwa siku hiyo. Hiki kilikuwa nyenzo maalum kwa ajili ya nyumba yake mbinguni.” Pili, wale ambao pia wana nyumba kubwa ni wale ambao wamejenga majengo ya kanisa au majengo mengine kwa ajili ya Ufalme wa MUNGU kwa mali zao.
 
 Mbinguni nilikutana pia na mzee anayeitwa Choi. Miongoni mwa wazee wote wa Korea na mashemasi walio mbinguni, alikuwa na nyumba nzuri zaidi. Nyumba yake ilikuwa juu sana kuliko jengo refu zaidi nchini Korea. Choi alikuwa amejenga makanisa mengi nchini Korea kwa utajiri wake. Nilimuuliza malaika, “Vipi kuhusu nyumba yangu? Je, iko katika mchakato wa kujengwa? Malaika akasema, Ndiyo.
Niliomba kuona nyumba yangu, Lakini waliniambia hairuhusiwi. Niliendelea kuomba. Baada ya kuomba kwa bidii, malaika walisema kwamba sasa Bwana ameruhusu. Tuliingia kwenye gari na kusafiri mbali sana hadi sehemu nyingine. Tulipokuwa tukiondoka, nilimuuliza malaika, “Hii itatuchukua muda gani?” Wakawawanasema kwamba ninazungumza sana. Hatimaye, baada ya muda fulani, malaika walinijulisha kwamba tumefika. Nilijawa na shauku kubwa. 
 
Nikauliza, “Nyumba yangu iko wapi?” Malaika akajibu, “Iko pale!” Lakini ilionekana kana kwamba mahali hapo palikuwa pazuri kwa bado haijakamilika kujengwa. Nililia, Nikieleza“Mngewezaje kunifanyia hivi? Hii inawezaje kutokea? Nyumba yangu inawezaje kuwa katika kutokamilika ?. Niliuza nyumba yangu pekee ili kujenga kanisa. Kanisa hili hatimaye lilikua na washiriki elfu tano. Niliandika vitabu vingi vilivyoongozwa na Roho Mtakatifu.
 
Kitabu kimoja kikawa kinauzwa zaidi. Kwa mapato ya vitabu, nilijenga shule za Kikristo. Shule hiyo ilizaa wachungaji 240. Wakati wa utumishi kama mkuu, nilikuwa nimetoa zaidi ya ufadhili wa masomo 400 kwa zaidi ya watoto 400 maskini. Nimewajengea wajane nyumba za kuishi. Hii yote iligharimu kiasi kikubwa cha pesa. Kwa hivyo hii inawezaje kuwa? Kwa nini nyumba yangu iko katika hali ya kuendelezwa ? Nimekasirika sana!” Malaika akajibu kwa ukali, “Hustahili kuishi katika makao mazuri kama haya mbinguni kwa sababu umeheshimiwa na watu mara nyingi. Kila wakati ulikuwa umejenga au umefanya kitu kizuri, ulisifiwa na watu. 
 
Uliheshimiwa hata na habari za kilimwengu. Kwa hiyo, kazi zenu zote ni bure.” Nilimuuliza malaika, “Kwa nini nina vyumba vidogo hivyo?” Hata hivyo, kwa kuwa tayari nilikuwa hapa, niliamua kuangalia nyumba yangu katika eneo la maendelezo. Nyumba yangu ilikuwa katikati ya nyumba zingine tatu. Nyumba yangu ilikuwa na safu tatu(3).
Nyumba hiyo ilikuwa na vyumba vingi vidogo kwenye orofa mbili za kwanza. Malaika akajibu, "Vyumba hivi ni vya wana wako na binti zako." "Nina watoto wanne tu" Hapana, si kwa ajili ya watoto wako wa udongo(yaani wa uzazi) bali ni kwa ajili ya wale uliowahubiria na kuokolewa.” Malaika alisema kwamba ilikuwa juu ya paa. 
 
Sikuipenda. Chumba changu hata hakijaisha. Kwa sauti ya hasira nilisema, “Ni ndogo sana! Kwa nini ni vigumu kumaliza?” Niliipenda! Nikauliza, “Chumba changu kikuu kiko wapi?” Malaika akajibu, “Hata wewe hujafa. Hatuwezi kumaliza nyumba au chumba chako kwa sababu hatujui ikiwa nyenzo zaidi zitatolewa. Unaelewa?" Tuliingia chumbani kwangu.
 
Niliona vyeti viwili vikining'inia ukutani. Nilikwenda kusoma kile kilichosema. Cheti cha kwanza kilichoelezwa nilipokuwa na umri wa miaka 18 nikiishi katika kituo cha watoto yatima. Siku ya Krismasi, nilikuwa nikirudi kwenye ibada ya asubuhi ya asubuhi. Nilikuwa nimemwona mzee mmoja akitetemeka barabarani. Nikavua koti langu na kumpa. Tendo hilo lilikuwa limenipa thawabu mbinguni. Cheti cha pili kilieleza tukio lilelile lakini kilikuwa cha kununua mkate kwa pesa kidogo niliyokuwa nayo kwa yule mzee. Kiasi sio suala. Tendo lazima liambatane na imani ya kweli.
 
** *NILITEMBELEA KUZIMU***
Malaika wawili(2) walinisindikiza hadi kuzimu. Wakasema, "Sasa utatembelea kuzimu." Hujui ukubwa wa kuzimu. Nilivyoiona nilipiga kelele, “Ni kubwa sana! Ni kubwa sana!” Hapa ndipo mahali ambapo roho zilizolaaniwa na kupokea laana ya milele zinawekwa.
Nilihisi kana kwamba mahali hapa palikuwa pakubwa mara elfu moja kuliko dunia. Nusu ya kuzimu ilikuwa na rangi nyekundu na nusu nyingine ilikuwa nyeusi sana. Niliwauliza malaika, “Kwa nini sehemu hii ni nyekundu?” Malaika wakajibu, “Je, hujui? Inawaka kiberiti.
 
 Nusu nyingine ni giza. Watu wakitenda dhambi na kuishia hapa, watateswa kutoka pande zote mbili.” “Mahali hapa ni pakubwa sana! Ni roho ngapi zilizo humu ndani?" Malaika akajibu, "Je, unaamini kuna mbingu na kuzimu?" “Ndiyo, ninaamini!” “Kuna wingi wa makanisa duniani na makanisa mengi yamejaa watu wengi.
Hata hivyo, wengi wao si wakristo wa kweli. Ni wahudumu wa kanisa tu. Makanisa ya kweli yataamini kabisa mbinguni na kuzimu. Maisha ya wakristo wengi yako katika machafuko kwa sababu hawaamini kabisa mbinguni na kuzimu. Nafsi moja(1) inapoingia mbinguni, roho elfu moja(1000) zilizolaaniwa huingia kuzimu. Kiwango cha uwiano wa mbinguni na kuzimu ni 1 kwa 1000." 
 
Chuo cha theolojia nilichokuwa nimesoma ni mojawapo ya shule kubwa zaidi za theolojia za kihafidhina nchini. Sikuamini katika mbingu na hadithi za kuzimu. Lakini sasa, mimi ndiye ninayeandika matukio kama haya ili kuwashuhudia wengine. Ingawa unaweza kuamini na kuwa Mkristo, ukiishi maisha yako kulingana na mapenzi ya mapepo, utaishia kuzimu.Mimi ni mchungaji wa Presbyterian. Mimi ni mzungumzaji maarufu.
 
Nimehitimu kutoka shule moja kubwa zaidi ya theolojia nchini Korea. Mahali pa kwanza waliponipeleka ni mahali pa salfa. Je, unaweza hata kufikiria jinsi moto wa kuzimu unavyoweza kuwa mkali? Hakuna mtu atakayeweza kuhimili joto kali. Kuzimu utasikia kauli tatu tu. Kwanza, ni joto sana na wanahisi kama kufa. Pili, wana kiu sana na wanahisi kufa. Tatu, utasikia wengi wakiomba maji. Ni ya milele! Watu wengi husema tuko huru katika Kristo na wanaishi maisha yao jinsi wanavyotamani.
Nikamwuliza yule malaika, “Wale waliomo humu ndani, wamefanya nini?” Malaika akajibu, "Kundi la kwanza ni la wasioamini." Wale ambao hawakuwa wamehubiria familia zao wenyewe lazima watubu! Malaika akaendelea, “Kundi la pili ni wale waliomwamini Yesu lakini hawakutubu dhambi zao.” Tunapaswa kutubu dhambi zetu na kukiri kwa Bwana.
 
Hatupaswi kutenda dhambi. Kuomba msamaha kwa midomo tu sio kutubu. Kwa moyo wa toba na wa dhati, lazima tutubu! Kisha niliwaona wachungaji, wazee, na mashemasi wengi kuzimu. Nilimuuliza malaika, “Ninawajua. Walikuwa wamemtumikia Mungu kwa uaminifu walipokuwa duniani. Walikuwa wamekufa wakati fulani uliopita. Sote tulifikiri walikuwa mbinguni pamoja na Mungu. Lakini sasa, ninawaona wote kuzimu na wanalia kwamba kuna joto sana! Sababu yao ni nini humu ndani?” Kulikuwa na idadi kubwa ya wachungaji, wazee, mashemasi na waamini walei wote. 
 
Wakiwa kwenye vitanda vyao vya kifo, walifikiri wamefanya kazi nzuri kwa hiyo hawakutubu mambo hayo. Hii ndiyo sababu walitupwa katika moto wa kuzimu.” Malaika akajibu, “Mchungaji Park Yong Gyu, mtu anaweza kuonekana kuwa mfuasi wa kweli wa Kristo kwa nje lakini Mungu anaujua moyo. Hawakuweka Jumapili Takatifu. Kwa kweli walipenda kupata pesa siku za Jumapili. Mashemasi na wazee wengi walikuwa wamekosoa mahubiri ya wachungaji wao. Hawakutoa zaka ipasavyo. Hawakuomba. 
 
Hawakuwa wamehubiri injili kwa watu hata kidogo. Wengi wa wazee hawa na mashemasi walikuwa wamewasumbua wachungaji wao na wangekuja kinyume na mamlaka yao. Walikuwa wameingilia kazi na shughuli za wachungaji wao. Kisha nikaona mfalme na mwana mfalme ambao walikuwa wamewatesa wakristo huko Korea kwanza. Mfalme na mkuu huyu aliwakata vichwa waumini wengi wa kwanza huko Korea. 
 
Waliwekwa katikati ambayo ilikuwa mahali pa moto zaidi kuliko zote. Pia nilimwona Hitler, Stalin, Mao Zedong, na mchungaji maarufu kutoka Korea kaskazini aitwaye Mchungaji Kang, na shujaa maarufu wa Kijapani, na mengi zaidi. Kisha tukafika mahali pa giza sana. Sikuweza kuona mahali ningekanyaga. Nilipaza sauti, “Malaika! Malaika! Ni giza sana! Ninawezaje kuona chochote?" Malaika walinipigapiga bega na kusema, “Subiri kidogo tu.” Ndani ya dakika chache, niliweza kuona. Niliona idadi isiyohesabika ya watu uchi.
 
 Wote walikuwa na wadudu wanaotambaa kwenye miili yao.
Hakuna hata inchi moja iliyosalia kwani miili yao yote ilikuwa imefunikwa kabisa na wadudu. Watu waliokuwa uchi walijaribu kuwafukuza wadudu hao huku wakisaga meno yao. Niliuliza, “Watu hawa walifanya nini walipokuwa wakiishi duniani?” “Ni wale ambao wamekosoa na kupinga mambo ya MUNGU. Hawakuwa waangalifu kwa yale waliyoambiana.”
Niliona mapepo yakitoboa na kuchoma matumbo ya watu kwa mundu. Vilio vyao vilikuwa havivumiliki kwangu.
 
 Nilimuuliza msindikizaji wangu, “Malaika, watu hawa walifanya nini walipokuwa wakiishi duniani? “Watu hawa walikuwa na kazi, nyumba, na familia lakini hawakuwa na cha kumtolea Mungu.
Hawakuwasaidia maskini, makanisa yao, au makusudi mengine ya kimungu. Walikuwa wabahili sana na wachoyo. Hata walipokutana na maskini, waliwapuuza na hawakujali. Walijijali wenyewe na familia zao tu. Walivaa vizuri, walilishwa, na walikuwa na maisha ya starehe.
 
Ndio maana matumbo yao yamechomwa kwa sababu matumbo yao yalijaa uchoyo. Lilikuwa ni tukio la kuogofya sana. Baada ya kushuhudia tukio kama hilo, niliporudi duniani, nilitoa pesa na mali zangu zote kwa wengine. Wokovu hauwezi kupatikana kwa pesa au mali. Ni kwa imani. Kuzimu ni mahali pabaya na pabaya. Ni mateso ya milele! Kisha nikaona vichwa vyao vimekatwa na msumeno mkali sana.
Nilimuuliza malaika kwa mara nyingine tena, “Watu hawa walifanya nini ili kustahili mateso ya kutisha namna hii?” Malaika akajibu, “Akili zao zilitolewa na Mungu kufikiria mema na yenye manufaa. Lakini watu hawa walikuwa wamefikiria mambo machafu. Walifikiria mambo ya ashiki(tamaa za ngono).”
 
Kilichofuata nikaona watu wakichomwa visu na kukatwa vipande vipande. Mtazamo huo ulikuwa wa kutisha. Nikauliza, “Vipi kuhusu watu hawa?” Walifanya nini hata kuteswa namna hiyo?” “Hawa walikuwa wazee na mashemasi ambao hawakutumikia makanisa yao. Kwa kweli, hawakutaka hata kufanya kazi au kutumikia! Mambo pekee ambayo walikuwa wamependa yalikuwa kupokea na kupokea kutoka kwa kundi.” 
 
Niliwaona wazee, mashemasi, na waamini walei wengine wakiteswa na mapepo. Mashetani walitoboa tundu kwenye ndimi zao na kuweka waya kupitia ndimi za wao kwa wao. Kisha mapepo yakawakokota watu kwa sime. Nikauliza tena, “Walifanya nini duniani?” Malaika akajibu, “Walikuwa wametenda aina nne tofauti za dhambi.
Kwanza, walikuwa wamewakosoa wachungaji wao. Wangezungumza mambo mabaya kuhusu wachungaji wao. Walikuwa nyuma wakiuma na kuwadhihaki wachungaji wao. " Nawasihi waliofanya vitendo hivyo WATUBU, WATUBU!! Malaika aliendelea, “Pili, walitukana kanisa kwa maneno yao. Walikuwa wamewasumbua Wakristo wengine hadi kufikia hatua ambayo hata waamini waliathiriwa na wakaacha kwenda kanisani na hata kuwafanya wengine waache kuamini. 
 
Walifanya yote waliyoweza ili kuwazuia Wakristo waaminifu wasifanye kazi ya Mungu. Waovu hao waliwafanya wengi waaminifu wajikwae. Mwisho, kuna wanandoa ambao walikunywa pombe na kuwatusi watu wa familia zao. Niliona mapepo yakiwatoboa wanaume na wanawake kwenye matumbo yao kwa msumari mkubwa sana wenye ncha kali. Nikauliza, “Walifanya nini?” Hawakuwa wametubu kamwe. “Hawa ni wanaume na wanawake ambao walikuwa wameishi pamoja lakini hawakuwa wameoana. 
 
Hawa wana hatia ya kutoa mimba kwani pia walipata ujauzito. Niliona kundi lingine la watu. Mashetani hao walikuwa wakipasua midomo yao kana kwamba mtu anapasua nyama au mboga. Niliuliza, “Kwa nini watu hawa wanateswa namna hiyo?” Malaika akasema, “Hawa ni wana, mabinti, wakwe zao na wakwe zao ambao walikuwa wamewajibu vibaya wazazi wao.
 
Walichopaswa kufanya ni kusema, ‘samahani’ badala ya kufanya mambo kuwa mabaya zaidi. Wengi wao walikuwa wametumia lugha ya matusi. Walikuwa wamewashambulia wazazi wao kwa lugha kali. Walikuwa waasi. Ndiyo maana midomo yao inakatwakatwa.”Ndugu, sisi sote tutakufa siku moja. Hatujui siku tutakufa.
Tafadhali jitayarishe. Kuwa tayari kwenda mbinguni. Tafadhali sameheaneni mara kwa mara kadri inavyohitajika.Tubu kwa toba ya kweli na ufanye hivyo siku zote.Ndugu zangu wapendwa, nilikuwa napuuza shuhuda hizo. Nilikuwa mchungaji wa Kipresbiteri ambaye alipuuza mambo kama hayo. Lakini sasa, lazima nishuhudie na nishuhudie kwako kile nilichoona.Tafadhali usisite kuishi maisha matakatifu. 
 
Tafadhali epuka adhabu na hukumu mbaya. Okoka! Msiishi kwa ajili ya miili yenu bali mtiini Ufalme wa Mungu. Tafadhali ombea wale wasiomjua Yesu. Kuinjilisha na kuzaa matunda. Tafadhali omba mapema asubuhi na uitakase Jumapili kuwa Takatifu. Tafadhali toa zaka kwa Bwana ipasavyo. Jikusanyieni thawabu zenu mbinguni na sio duniani. Nakuombea na kukubariki katika Jina la YESU!Kumbuka KUSHIRIKISHA wengine ujumbe huu : ubarikiwe!.

SIRI ZA MBINGUNI NA KUZIMU SEHEMU YA TATU(3)

Mwisho wa dunia hii uwadia hivi karibuni.Hivyo uwe mtu wa kukesha a kuomba(1 Petro 5:7).Namshukuru MUNGU kwa ajili ya hii neema juu ya maisha yangu. “Bwana ni nguvu zangu na ngao yangu. Moyo wangu umemtumaini, Nami nimesaidiwa; Basi, moyo wangu unashangilia, Na kwa wimbo wangu nitamshukuru.” ( Zaburi 28:7 ).Bwana aliniahidi kunitembelea tarehe 9 februari ,2013 na akafanya.Yeye ni MUNGU mwaminifu sana.( Zaburi 33:11).

Siku ya tarehe 9 ya mwezi wa February 2013, mishale ya saa Saba(7) mchana, Nilikuwa nimejilaza kitandani na nikasikia sauti ikisema, “Huu ndio muda mwanangu, Jiandae mwenyewe sasa hivi !” Ndipo nikaanza kuomba damu ya YESU inisafishe na kunitakasa na kunifanya niwe safi.Ghafla usingizi mzito ukanijia.Nilipofumbua macho , nikajikuta kwenye chumba ambacho nilikutana na YESU mara ya kwanza.Nikamuona YESUKRISTO anaingia.Akasema, “Mwanangu, nataka nikuonyeshe mambo mengi leo , kwa ajili ya siku za mwisho, Kwa kuwa hii ni mara yam wish kukutembelea wewe.Unatakiwa uwaambie kile ulichokiona kwa sababu haukuwa unawaambia watu wengi kuhusu yale niliyokuwa nakuonyesha wewe kipindi cha nyuma”.Bwana akaanza kulia kwa sababu ya haya.Nilikuwa na huzuni alipokuwa akilia kwa ajili ya uzembe wangu.Tulipotoka katika kile chumba , Bwana akaniambia mimi, “Mwanangu, njoo. Ngoja nikuonyeshe Hukumu Kuu.”Ndipo tukafika mbele ya enzi kubwa.

WAUAJI
Tulipofika mbele ya enzi kubwa nikamuona mwanamke pale akisema, “Nisamehe sana.” Bwana akaniambia mimi, “Muangalie yule mwanamke anaeye lia.Anajua hawezi kuingia mbinguni na ndio maana analia.”Nikamuuliza Bwana niambie mimi sababu ,kwa nini anahayo mawazo.Bwana akanijibu, “Mwanangu, muangalie.”Tazama nikaona historia ya maisha yake.Alikuwa mKristo alipokuwa duniani.Alikuwa akitafuta mtu wa kumuoa na Bwana akamwambia kuwa mvumilivu, lakini tamaa yake ya kuolewa ilikuwa kubwa mno.Haku subiri muda wa Bwana.Badala yake akamuua rafiki yake kwa sumu, rafiki yake akafariki(Mathayo 5:21).Ndipo akafanya mpango akaolewa na huyo mume wa rafiki yake.Baadae mume wake akagundua kuwa ndiye aliye husika kumuua mke wakeyaani mke wake wa kwanza.Mwanaume huyo naye akamuua yule mwanamke pia kwa sumu na ndiyo maana mwanamke yule alikuwa akilia sana mbele ya enzi ya hukumu( Luka 11:47).
Bwana akasema, “Nalimuonya asifanye hayo lakini hakunisikiliza mimi na sasa yuko analilia kusaidiwa na ili apate nafasi ya pili.Hio haiwezekani, ufalme wangu ni sehemu takatifu.Sio sehemu ya wauaji.Nilikuonya utubu lakini hukunisikiliza mimi.Umechelewa kwa wewe!”(Isaya 59:1-3).Bwana akamwambia, “Ondoka kwangu !” na nikaona kimbunga kikubwa kikambeba mpaka kuzimu !.(Mathayo 25:41,46).Usiue au usinyonge kwa sababu afanyaye hayo ni hatari kwa hukumu.Tubu sasa na uokolewe.Tukaondoka hiyo sehemu.
Tafadhali elewa hii:KRISTO anakuja tuu kwa ambao ni WAAMINIFU,WAKESHAO,WAANGALIFU.Sio tuu yatosha kuwa unasifa za kuingia mbinguni bali unatakiwa uendelee kila muda kuwa safi , tayari kwa ujio wake.Fanya maisha yako yaone kila siku tazamia maisha yako ya milele.Haitoshi kuonya na kuwaangalia wengine.
Unatakiwa pia ujiangalie na wewe mwenyewe na kuendelea mbele na wokovu wako kwa ajili ya roho yako.Popote unapofikiri ujio wake KRISTO na ukajawa na hofu au mashaka, hiyo inaonyesha kuna kitu hakiko sawa katika maisha yako na unatakiwa kumruhusu Roho mtakatifu kufanya kazi yake ndani yako.(Wafilipi 2:12-13).
Ni bora uende nae kwenye unyakuo kuliko kuachwa.Kama ukiachwa, mpinga KRISTO atakukejeli na kudharau Imani yako, utakuwa kwenye adhabu kubwa kwa ajili uliijua kweli na ukaiacha.Vipi kama ukifa kabla ya unyakuo? Unatakiwa uwe tayari kwa kurudi kwa Bwana.Kama ukifa na ukawa hata unadoa moja kwenye vazi lako utatupwa.[Note:Hii sentensi itasababisha kutoeleweka sana kwenye kanisa, 1 Yohana 5:17 Kila lisilo la haki ni dhambi, na dhambi iko isiyo ya mauti.]. Kama unaendelea kumtenda dhambi MUNGU na wafikiri bado una muda wakutubu unajidanganya mwenyewe.Ni bora utubu dhambi zako SASA kwa sababu kesho inaweza ikawa umechelewa kwa wewe. “USIUE ! ”
Bwana akanichukua mimi mpaka Kuzimu.Tukapita kwenye handaki lile lile ambalo tulipita mara ya kwanza na tukafika kuzimu.Kuzimu imejiongeza yenyewe kwa sababu shetani anafanya kazi kwa bidii. (Isaya 5:14)
MIAKA 250 AKIWA KUZIMU.
Nalimuona mtu akilia na kupiga kelele ndani ya Kuzimu ya moto akisema,”Uko hapa kuniokoa mimi?,Nipo hapakwa miaka 250.Nimekusubiri kuona kama nitampata mokozi, lakini nilishakata tamaa.Lakini sasa nimekuona wewe, nina mashaka kama uko hapa kuniokoa mimi.” Bwana akamwambia, “Nilituma watumishi wangu wengi kwako kukwambia utubu lakini hukunisikiliza mimi.Walikueleza ukweli kuhusu kuzimu ya moto lakini uliwaambia sio kweli; ni utani na ukadhani maisha yako ni mazuri tuu.Ulitumia muda wako tuu kwenye kunywa pombe, kwenda hoteli moja baada ya ingine, kufanya uzinzi (1 Wakorintho 6:9-11, Yakobo 4:4).Ulikuwa ukiumwa sana kiasi kutaka kufa , lakini sikuruhusu ufe ili uweze kutubu na kuokolewa lakini haukutaka kusikia jina langu likitajwa.Sasa ndio unakumbuka kumtafuta mokozi.Siwezi kukuokoa tena.Umechelewa” (Mithali 1:24-33)
Bwana YESU alikuwa akilia alipokuwa akiongea na huyo mtu kwa sababu hafurahii kifo cha mwenye dhambi.(Ezekieli 18:30-32).Hapa ulipo duniani unayo nafasi ya kutubu, lakini baada ya kufa, hakuna tena nafasi ya kutubu.YESUKRISTO ndiye pekee mwokozi wa wote wanao ishi lakini sio waliokufa.
Pumzi yako ni nafasi yako.(Muhubiri 12:1-8) tukatoka hiyo sehemu.
BINTI YA MTOTO WA MIAKA 15
Bwana akanichukua mpaka sehemu ingine ya kuzimu.Nikamuona mtoto akilia sana.Kulikuwa na funza na wadudu wengine wengi sana mwilini mwake.Anapomtoa mmoja ,funza wengine wengi wanakuja katika sehemu hiyo aliyomtoa.Alipotuona ,alikuwa akilia ili kupata msaada.Nikamuuliza sababu ya yeye kuwepo hapo.Akaniambia historia ya maisha yake,akasema “Nilipokuwa duniani, nilipenda kwenda kumbi za starehe kucheza(clubs to dance), [1 Timotheo 5:6].Wazazi wangu hawajawahi kunionya kwa sababu nilikuwa ndiye mtoto pekee walionizaa.Nilipenda kutembea na wavulana kufanya ngono nao.( 1 Wathesalonike 4:3-8)(Waefeso 5:3-6), nilisikia kuhusu kuzimu lakini sikutaka kuwasikiliza.Marafiki zangu wengi waliniambia nitubu nami nikawa nawachukia.Nilikuja kupata ujauzito na mama yangu akanikumbusha juu ya ndoto zangu za kuja kuwa mwanasheria.Kwa sababu ya hiyo niliamua kutoa ujauzito na kwenye hali ya kutoa nikafariki nami.Ndipo nimeishia hapa kuzimu na nipo hapa kwa miaka kumi sasanikiteswa na kuungua moto.Nikiondoa funza mmoja basi wengi zaidi huja.Tafadhali nisaidie.Sasa nipo tayari kutubu.” Nilipatwa na huzuni kubwa sana kusikia hayo.Bwana akamwambia , “Huwezi kutubu tena.Umechelewa.” Bwana alikuwa akilia kwa uchungu sana kwa ajili ya huyo mtoto lakini hakuweza kumuokoa.Yule mtoto alilia kwa kupiga makelele sana akisema, “Hapana ! hapana ! hapana! Hapana ! Nimoto sana nataka nife !”Lakini hakuweza kupata kufa.(Ufunuo 9:6) Nikamuomba Bwana anitoe huko kwa sababu sikuweza kuvumilia kuangalia mateso wanayopata.
Wazazi nisikilizeni,Mfundishe mtoto wako katika njia ya Bwana.Wafundishe Neno la MUNGU.Wasahihishe pale walipofanya makosa tofauti na maagizo ya Bwana.(Waefeso 6:1-4) (1 Yohana 2:1-6). Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee. (Mithali 22:6).Tukatoka hiyo sehemu na kwenda sehemu ingine.
MTOTO WA KIKE WA MIAKA 14
Tunatakiwa tuwe makini na kujiondoa wenyewe kutoka kwenye dunia ya dhambi kwa sababu uvumbuzi mwingi unatuharibu sisi mbele za Bwana(Mhubiri 7:29).Bwana akanionyesha msichana akiwa Kuzimu, Mateso aliyokuwa akiyapata yalikuwa mazito na ya kutisha na likuwa akipiga makelele, “Inatosha ! inatosha! Inatosha ! Tafadhali nitoe !” Alikuwa akitumia mkono wake wa kushoto kuziba sikio lake kipindi akijichua(masturbating) na kitu cha moto sana kwa mkono wake wa kuume.{alikuwa akilazimishwa na mapepo kujiingiza hicho chuma cha moto ukeni na kukitoa mara zote }.Alikuwa akilia kwa uchungu lakini hakuacha kufanya vitendo hivyo.
Nikamuuliza yeye kwanini anafanya hivyo huko motoni nilipata historia ya maisha yake, “Nilikuwa na miaka 14 nilipofariki.Nilipokuwa duniani, nilipenda kusikiliza miziki ya kidunia.Na muda wowote nilipozisikia nilikuwa napatwa hisia za mapenzi ambazo zilinipelekea kujichua(masturbate).Niliwahi sikia kuhusu sehemu hii ya mateso, lakini siku amini kama iko kweli.Watumishi wengi wa MUNGU walinionya kuhusu miziki ya kidunia lakini niliwaita wapumbavu.Walinionya kwenye mahubiri yao kuwa kujichua/punyeto (masturbation) ni dhambi , lakini niliwaambia MUNGU ni mwenye rehema.Sasa nimeamini sio wajinga.Sababu ya kujishika sikio ni kwa sababu bado nazisikia nyimbo za kidunia na zinaniumiza sana.Nilikuwa najichua kutumia kitu nilipokuwa duniani ndiyo sababu ya kunitesa mimi motoni kwa jinsi hii.Tafadhali nisaidie mimi, siwezi kuacha na inaniumiza sana !”
Bwana akamwambia , “Siwezi kukusaidia wewe tena.Umefanya neema yangu kuwa si kitu ulipokuwa duniani, lakini mahali hapa,hakuna tena neema zaidi.Umechelewa kwa wewe kutubu !” Alikuwa akipiga kelele na kulia lakini Bwana alimwambia, “Siwezi kubadili maneno yangu.Yameandikwa tayari.Neno langu litasimama milele(Mathayo 24:35)(Mathayo 13:31) Wazazi,tafadhali mjali na uwatunze watoto wako(2 Wakorintho 12:14)(Waefeso 6:1).Kumbuka hasira ya MUNGU inakuja kwa watoto wasio watii.(Wakolosai 3:6)Tukatoka hapo na kwenda sehemu ingine.
MTU WA MIAKA 25
Bwana akanichukua mpaka sehemu ingine kuzimu ambapo niliona mtu akilia kwa sauti, “Nitasikia !, nitasikia ! tafadhali niko tayari kusikia !”Nikamuuliza kwa nini ndipo akasema, “Nilipokuwa duniani, nilipenda kufanya mapenzi na wasichana hasa wanaojiuza/makahaba.Rafiki yangu aliniambia nitubu na niokolewe lakini nikamjibu sitaki kusikia ujinga huo wa mahubiri-Niko tayari kwenda motoni,we niache kivyangu.Lakini sasa nipo tayari kusikia na kutubu.Tafadhali ! tafadhali nisaidie mimi ! ”
Bwana akamwambia, “Nilikupa neema ya kutosha mpaka ulipokufa umri wa miaka 25, lakini hukusikiliza maonyo yangu.Sasa unaomba kusikia.Umechelewa !,Hakuna mtu awezaye kukwambia kuhusu MIMI hapa kwa sababu kila mtu aliyepo hapa anatafuta njia ya kutoka humu.Kila roho ifikayo hapa haiwezi tena kutoka.Umechelewa(1 Wathesalonike 4:3).Mwili wako sio kwa ajili ya uasherati(1 Wakorintho 6:13).”
Mtu huyo akalia.Akimuomba Bwana amtoe hiyo sehemu ,sikuwa na muangalia tena na tukatoka hiyo sehemu ya kuzimu.
UFALME WA MUNGU
Bwana akanichukua na kunipeleka Mbinguni.Bwana YESUKRISTO asifiwe ! Baraka kwa Bwana Mungu wa Israel kutoka milele na milele ! Ameni na Ameni(Zaburi 41:13).Mbinguni ni pazuri sana.Ardhi yake ni kama kioo.Nilikuwa nafuraha na nilidhani kuwa nitabaki hapo na kuishi milele.Nikasikia sauti nzuri za malaika zikimsifu MUNGU(Zaburi 103:1-3).Bwana akasema, “Waambie watu wangu kuwa ufalme wangu upo kweli.Wamebarikiwa watakao urithi.”Kulikuwa na maua mengi mazuri(Zaburi 119:129-135).

MTI WA UZIMA
Bwana akanichukua mimi mpaka sehemu ambayo niliona Mti wa Uzima kwa mbali.Ulikuwa mzuri,unang`aa kama dhahabu(Ufunuo 22:2).Bwana akasema, “Nimeulinda Mti wa Uzima kwa ajili ya watu wangu.Waambie wamebarikiwa wale wazifanyazo na kutii amri zangu, hao ndio wenye haki kwenye Mti wa Uzima.”(Ufunuo 22:14) tukaendelea mbele.
WATOTO WALIOTOLEWA MIMBA DUNIANI
Bwana akanipeleka sehemu ingine mbinguni kulikuwa na ukumbi mkubwa na nikawaona watoto wengi wadogo waliojawa na utukufu wa MUNGU.Walikuwa wakimsifu MUNGU(Zaburi 86:11-13).Bwana akasema, “Hawa ni watoto ambao wanawake wanawatoa uja uzito wao(arboted) duniani.Wanamilikiwa nami na watakuwa katika ufalme wangu tukufu.”(Zaburi 89:1-2) Ndipo tukatoka hiyo sehemu.
MALAIKA GABRIEL AKATUTEMBELEA
Kipindi Bwana anaongea nami, tazama nikamuona malaika.Alikuwa mrefu na mzuri, amevaa taji katika kichwani.Bwana akaniambia, “Ni malaika Gabrieli.”Nilikuwa na furaha kukutana nae na Bwana akaniongoza kunichukua mimi kwenda sehemu mbali mbali Mbinguni ili niwezekuwaambia wengine nilichokiona.
MFALME DAUDI
Malaika Gabrieli akanichukua mpaka kwenye jumba kubwa sana.Akasema, “Ni nyumba ya mfalme Daudi”Nikasema nataka kumuona mfalme Daudi uso kwa uso.Tukaenda ndani ya chumba chake na nikamuona mfalme Daudi akimsifu MUNGU kwa zaburri na kucheza(Zaburi 34:1-6).Nikamsalimu na akaniita jina langu, “Senayon, Karibu”.Nilishangazwa kwa kuwa alikuwa analijua jina langu.Akasema, “Senayon, haumsifu MUNGU.Hutaki kucheza kwa MUNGU.Unapomsifu MUNGU nakucheza kwa Ajili yake, neema Yake inakuwa karibu na wewe.”Nikamuuliza . “Umejuaje hayo?, je uliniona nilipokuwa duniani? Au unayajua tuu maisha yangu ya duniani ?”
Akawa anacheka na akasema, “Sijisemei kwa uwezo wangu”..Baadae nikagundua ni MUNGU anaongea na mimi kupitia yeye.Akanipa mimi kitabu kidogo akaniambia, “Kula !Kula hicho !.”Nilipokila hicho kitabu nikawa na kiu sana.Nikamwambia , “Nina kiu.Nina kiu.”Wakanipa mimi damu ya YESUKRISTO kuinywa.Nilipokunywa nilikuwa natetema kama vile nimepatwa na baridi kali kwa muda wa zaidi ya dakika tano.
Nilipokuwa natetema;Malaika Gabrieli na Mfalme Daudi walikuwa wamepiga magoti wakisema, “UTUKUFU KWA MUNGU!”(Zaburi 29:1-11).Nilipoacha kutetema baada ya muda ndipo mfalme Daudi akaniambia, “Sasa utamsifu MUNGU na kucheza kwake.Waambie watu wamsifu MUNGU na neema Yake itakuwa karibu nao.”
Malaika Gabrieli akasema, “Senayon,unavitu vingi vya kuona, Tuondoke.”Nikamwambia, “Hapana,sitaki kuondoka kumuacha Mfalme Daudi, tafadhali .”
Bali hakunisikia na tukaondoka pale kwa mfalme Daudi.
NYUMBA YA NABII ELIYA
Malaika Gabrieli alinichukua mimi mpaka kwenye nyumba ingine kubwa na nzuri sana.Aliniambia ni ya nabii Eliya.Nilikuwa nafuraha iliyopitiliza.Nikamwambia, “Nataka nimuone!”Malaika Gabrieli akanichukua mimi mpaka kwenye nyumba ambapo alitoka mvulana kijana mzuri sana na kuniambia “Senayon karibu !” Nilikuwa nafuraha sana kumuona yeye.Nikamwambia, “Ulikuwa shujaa sana duniani.Nimesoma kuhusu wewe kwenye Bibilia.”Naye akanijibu, “Kuna moto unawaka ndani ya moyo wako.Utakuwa shujaa kuliko mimi.”(2 Wakorintho10:4-5).Aliniambia mengi kuhusu mimi.Malaika Gabrieli akaniambia, “Senayon, tunatakiwa tutoke sasa hapa kwa sababu unavitu vingi vya kuona.”Tukatoka na kwenda kwenye nyumba ingine.
NYUMBA YA MTUME PAULO
Malaika Gabrieli akanichukua mpaka sehemu ingine ambako kulikuwa na nyumba kubwa sana ,Nayo imetengenezwa kwa dhahabu, na imepambwa na mawe mazuri sana.Akaniambia, “Hii ni nyumba ya mtume Paulo.”Nikasema nataka nimwone yeye.Yeye amekuwa mfano wa kuigwa wakristo wengi.Malaika Gabrieli alinichukua mpaka kwenye hiyo nyumba, tazama nikamuona kijana mdogo amepumzika kwenye chumba kizuri. Senayon,” akesema , “Karibu sana.Ninayo furaha kukuona wewe.”Nilishangaa kuona anajua jina langu.Wanajua yote kwa sababu ya utukufu wa MUNGU uko pamoja nao.Na haikuwa muhimu mimi kuwa ambia jina langu kwa sababu wao walini jua jina langu kwa nguvu ya MUNGU.
Akaanza kuniambia historia yake kwenye kitabu cha Matendo(Matendo 8:1-4)(Matendo 9:1-31).Alipomaliza, aliniambia, “Nimtumia neema ambayo YESU amenipa mimi na sikuifanyia mchezo.”Akanipa kitabu kidogo na kuniambia, “Kula !, Kula hicho !.”Nilipokula sikuwa na kiu na kiukweli kilikuwa kitamu.Mtume Paulo akaniambia, “Sasa utahubiri injili na kufundisha shuhuda za YESUKRISTO.Utafundisha baadhi ya nyaraka(epistles) zangu ambazo bado sikuziandika.”(Warumi 8:35-39)Wote kwa pamoja Malaika Gabrieli na Mtume Paulo tulikuwa tukimsifu MUNGU.(Warumi 4:20-25)(2 Wakorintho 5:13-18).Ndipo tukamuacha .Nilikuwa na furaha.Mbingu imejawa na uzuri na utukufu wa MUNGU.(Ufunuo 21:18).
NYUMBA YA BABA ABRAHAMU
Ndipo Malaika Gabrieli akanichukua kwenda sehemu ingine Mbinguni ambako kulikuwa kuna nyumba nzuri iliyopambwa kwa maua na mawe mazuri.Akasema ni nyumba ya baba Abrahamu.Nikamuomba anipeleke nimuone baba Abrahamu.Nikafika pale na kumuona Baba Abrahamu, nikamwambia, “Baba wa imani, Baba wa imani.”Akaanza kunipa mimi ushauri kuhusu vitu vingi katika maisha yangu.Aliniambia, “Unatakiwa uwe na imani katika lolote unalomuomba BABA na kuwa mvumilivu katika hali yeyote ile”(Yeremia 33:3) (Mathayo 17:20) Imani ni hakika.(Mathayo 21:21-22)(Waebrania 11:1).Tukatoka hapo.
MALAIKA SABA(7) WAKIWA NA TARUMBETA NA WATANO(5) WAKICHEZA.
Malaika Gabrieli alinichukua mpaka sehemu ingine ambako niliwaona malaika watano(5) wakicheza kwa furaha.Pia nikaona malaika saba(7) wakiwa na matarumbeta.Nikamuuliza Malaika Gabrieli aniambie kuhusu kazi ya hao malaika.Akaniambia kama mtu akimpa maisha yake YESUKRISTO duniani , ndipo wao hao malaika saba(7) hupuliza tarumbeta kama ishara kwa roho moja inapotubu.Malaika watano(5) wanakuwa wakicheza na mbingu nzima hushangilia.Pia kama roho ikiingia mbinguni wao pia husherehekea kwa hiyo roho.(Luka 15:7).Kuna furaha kubwa mbinguni juu ya mtu mmoja mwenye dhambi akitubu.(Luka 15:10).
WASHINDI
Malaika Gabrieli alinichukua mpaka kwenye kumbi kubwa.Akanipa mimi upanga ili niunyanyue juu.Nilipounyanyua nikajikuta mwenyewe kwenye uwanja wa vita.Nikaona watu wasio hesabika wamefungwa chini.Kulikuwa na mapepo wengi waliowafunga hao watu.Baadhi yao bado wana silaha za vita.Zimeandikwa migongoni mwao , “WASHINDI”.Walikuwa wakiwapiga mapepo ili kuwaweka huru wale waliofungwa.Ambao wamewekwa huru huyo mtu hukimbia mpaka kwenye chumba kiitwacho “SEHEMU YA SIRI YA MUNGU ALIYE JUU” Nikamuuliza Malaika Gabrieli kunitafsiria akasema, “Washindi ni wakristo hai wa kweli(1 Yohana 5:4-5) nawale waliofungwa chini ni wadhambi.Wale mapepo wanawasimamia ili waendelee kukaa kifongoni ili waende kuzimu ya moto.(1 Petro 5:8-9)Kupambana na mapepo wale waliowafunga inamaana ‘kuhubiri kwa wadhambi na kuwaombea’.Chumba wanachokimbilia ni salama ambacho ni YESUKRISTO.(Mathayo 11:28-30) na hiyo ndiyo sababu kinaitwa ‘SEHEMU YA SIRI YA MUNGU ALIYE JUU’(Zaburi 91:1)”.Unatakiwa uombe sana ili MUNGU akufungue wewe kutoka kwenye pepo ambaye yupo kwenye hiyo kazi ya kupeleka watu kuzimu ya moto.
UTAKASO
Malaika Gabrieli akanichukua mpaka sehemu nzuri sana mbinguni, iliyopambwa kwa dhahabu safi.Nayo ardhi ilikuwa nyeupe na safi kama glasi.Kulikuwa na maua mengi mazuri na mawe mazuri mengi.Niliona dhahabu zilizo pachikwa.Nikamwambia Malaika Gabrieli kwamba ntaka niguse dhahabu zilizopachikwa juu.Akanibeba juu kwenye mabega yake ili niweze kugusa.Nikamwambia malaika Gabrieli sitaki kuondoka hiyo.Nilikuwa nikilia kwafuraha kwasababu sehemu ile ilikuwa nzuri sana.(Ufunuo 21:18-19).
Malaika Gabrieli alisema, “Hapana.Unavitu vingi vya kuona hapa na ni muhimu sana uvione”.Nilizidi kumwomba nikimwambia,”tafadhali sitaki kuishi maisha yale ya dunia.tafadhali fanya jambo kuhuso hicho.”Malaika Gabrieli alisema, “Senayoni njoo twende zetu”.Tukatoka tukaenda kwenye bwawa la damu ya YESUKRISTO.Malaika Gabrieli akaniuliza, “Sanayon, unakumbuka hii sehemu ?”Nikamjibu, “Ndio.Niliona hili bwawa la damu kipindi cha kwanza na YESUKRISTO.”Malaika Gabrieli akasema, “Sawa uko sahihi.”Tulikuwa tukisimama pale kwa zaidi ya dakika tano lakini hakutoa neno hata moja kwangu.Mara, Nikaona mwanga wa Blue mzuri.Huo mwanga ukanichukua mpaka kwenye hilo bwawa la damu ambapo kulikuwa na mkono usio onekana ukaanza kuniosha ndani ya ziwa la damu.Iliniumiza mimi na nilikuwa nikilia.Nikamuomba Malaika Gabrieli kunitoa lakini alikuwa amepiga magoti akisema, “UTUKUFU UWE KWA MUNGU KUTOKA MILELE HADI MILELE, MFALME WA WAFALME NA UZURI WAKE MUNGU !”(Zaburi 95:1-6).

Tazama ! Nikaona mwili wangu duniani uko kitandani.Kitu fulani cheusi kilikuwa kikitoka nje ya mwili wangu.Nilishangaa kuona hicho kitu kuwa kilikuwa ndani yangu mimi(Zaburi 51:12-15).Kipindi ambapomkono usioonekana ulipomaliza kuniosha mimi, mwanga halisi ukanitoa nje ya bwawa la damu(Zaburi 51:8-11).Tazama 1nikasikia sauti kubwa ikisema, “Sasa utakumbuka kile ulichokiona na utaishi vile nitakavyo, wewe sio tena mtu wa kawaida kwa sababu nimekutakasa wewe.”Hiyo sauti ikaanza kuongea kuhusu kaka ambaye alinifundisha mimi kwenye njia za Bwana, Jina lake ni IJAWJAW EAMON MARK.Bwana akaniambia mengi kuhusu yeye kwamba atalitimiza agano lake naye na amempa vazi la ukamilifu.Sauti ikaniambia kuhusu watu wengi.Nikamuuliza Malaika Gabrieli, “Tafadhali, Nataka nione nani ninayemsikia sauti yake.”Malaika Gabrieli akajibu, “Sina nguvu ya kukupeleka pale , lakini nifuate mimi.”Tukatoka hiyo sehemu.
ENZI YA BABA MUNGU
Malaika Gabrieli akanichukua mimi mpaka kwa YESUKRISTO.Akamuelezea YESUKRISTO kuwa nataka kumuona BABA na mwisho nikagundua kuwa ni BABA aliyekuwa aliyenichukua mimi kwenye bwawa la damu.YESU akatabasamu na kunishika mikono yangu akisema, “Wataka kumuona BABA ?”.Nikamjibu, “Ndio.”
Katika kwenda kumuona BABA ,tulipita katika ukumbi ambapo kulikuwa na malaika wengi.Mara wakapiga magoti na kusema, “UTUKUFU UWE KWA MUNGU !”(Zaburi 84:11).
Tulipotoka kwenye huo ukumbi ,na tazama nikaona mwanga mkali kwenye enzi.Ulikuwa mwanga kama moto unaowaka.Ingawa tulikuwa mbali sana kiasi cha maili nyingi lakini nilihisi nataka kuanguka.Sikuwa na nguvu ya kutembea kuelekea kwene enzi tena.Nikamuomba Bwana nikisema, “Tafadhali nirudishe.” Bwana YESUKRISTO akaniambia, “Huyo ni BABA,Hutaki kumuona TENA?”Nikamwambia , “Ndio,tafadhali, tafadhali, Nataka kufa.Siwezi kupumua zaidi.”YESU akatabasamu na kunirudisha kwa malaika Gabrieli.
VITABU MBELE YA MALAIKA.
Malaika Gabrieli akanichukua mimi mpaka kwenye chumba kibwaa ambako kuna makundi ya malaika.baadhi walikuwa wakiandika majina na wengine wakifuta majina kutoka kwenye vitabu.Nilipewa nafasi ya kutembelea malaika wa nne(4) kati ya wengi.Nikamuliza malaika Gabrielii anielezee kila kitu akatabasamu.Malaika wa kwanza ni malaika anayehusika na kitabu cha uzima.Malaika Gabrieli alisema, “Hiki kitabuni kitabu ambacho kina majina ya wale walio okoka wapya na wale wakristo wakweli na walio okolewa.”(Ufunuo 3:5).
Nikauliza sababu ya malaikaa kufuta baadhi ya majina na kuandika majina mengine.Naye akanijibu, “Wale walioacha wokovu waliorudi nyuma.”(Ufunuo 2:4-5).Nikamuuliza tena, “Unamaanisha majina yao yanfutwa milele kutoka kwenye Kitabu cha Uzima ?.”Akatabasamu na kusema, “HAPANA.Hiki ni kitabu kitakatifu na hakiwezi kuwa na majina ya wenye dhambi.”Nikamwambia, “Niambie hayo majina yanayofutwa yanawekwa wapi ?”.Akanichukua mpaka kwa malaika mwingine ambaye naye alikuwa akiandika na kufuta baadhi ya majina.Malaika Gabrieli akasema, “Hiki ndio kitabu cha waliorudi nyuma katika wokovu na kina majina ya wote walio iacha njia ya Bwana.Sababu ya malaika kufuta baadhi ya majina ni kwa sababu ya wale waliokuwa wamerudi nyuma na kuiacha njia ya Bwana wamemrudia MUNGU,Majina yao huandikwa tena katika kitabu cha Uzima.(Ufunuo 20:15)”Majina aliyokuwa akiyafuta ni majina ya waliorudi nyuma katika wokovu (Yeremia 3:22).Akanichukua na kunipeleka kwa malaika mwingine aliye kuwa akifanya kazi kwa bidii sana.Hata hivyo alikuwa akiandika tuu majina, nasio kuyafuta.Malaika Gabrieli akasema, “Hiki ni kitabu chenye majina ya wote ambao huishia Kuzimu ya moto kila siku.Kitaitwa kitabu cha hukumu(The condemnation Book).’”Malaika Gabrieli aliniambia, “Majina yanaandikwa ni yale ya ambao walikufa bila kuwa na YESUKRISTO maishani mwao.”(Ufunuo 20:12).Tukatoka hapo na kwenda sehemu ingine.
Malaika Gabrieli akanichukua mpaka kwa malaika mwingine ambaye alikuwa anaandika tuu majina bali hayafuti.Malaika Gabrieli akasema, “Hiki ni kitabu chenye majina ya wale wanaotoa zaka zao.”(Malaki 3:8-12).Malaika alikuwa akiandika majina na kupiga kelele akisema, “Amelipa ! amelipa !” Na mara nikamuona malaika akaja pale.Akafungua chumba kizuri na katika kile chumba kulikuwa kuna vitu vingi vizuri vya dhahabu kwenye maboksi.Malaika akaingia katika hicho chumba na kuchukua moja ya vitu vya vyahabu nzuri kuenda zake.Nikamuuliza Malaika Gabrieli aniambie nini kilichokuwa ndani ya boksi ambacho malaika amekichukua na kuenda nacho.Malaika Gabrieli akanijibu, “Ndio.Ni baraka kubwa kutoka kwa Bwana kwa yule aliyetoa fungu la kumi(zaka) kwa uaminifu.”(Obadia 1:15).Tukatoka hiyo ssehemu.
DAKIKA TANO (5) ZAIDI.
Malaika Gabrieli alinichukua mimi mpaka kwenye ukumbi ambao kulikuwa na malaika wengi wakisema, “Bwana ni muda.Acha watu wetu waje.”Nikamuona Bwana YESUKRISTO akilia kama mtoto akisema, “Acha tuwape DAKIKA TANO ZAIDI !” Baada ya hapo Malaika Gabrieli alinionyesha mimi maandalizi yote kwa ajili ya unyakuo yako tayari.Kila kitu kii tayari Mbinguni na YESUKRISTO anasubiri kuambiwa NENDA kutoka kwa BABA MUNGU(2 Wathesalonike 5:2-6).Tena Malaika Gabrieli alinipeleka kwenye ukumbi mwingine ambako kulikuwa na mavazi mazuri mengi sana.Yalikuwa yamepambwa na uzuri,kushangaza na utukufu kwa dhahabu safi.Nilimuuliza malaika Gabrieli, “Ni watu gani wataomiliki hayo mavazi mazuri !?” Naye akanijibu, “Haya ni mavazi ya Wakristo watayavaa kwa ajili ya ndoa ya mwanakondoo.”(Ufunuo 19:7-9)
Nilimuuliza Malaika Gabrieli anionyeshe mimi vazi langu.Naye alilionyesha moja ya vazi na kusema , “Hili vazi ni lako.” Nilikuwa na furaha ya ajabu na ndani yangu nikijisemea, “Sitaenda kuzimu ya moto.” na tazama nikasikia sauti kubwa ikisema, “TAZAMA NAKUJA HARAKA; SHIKA SANA ULICHO NACHO USITAKE MTU YEYOTE AKUNYANG’ANYE TAJI YAKO !”(Ufunuo 3:11).Niliogopa sana niliposikia hiyo sauti kwa sababu inamaanisha “Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke.”(1 Wakorintho 10:12) (1 Wakorintho 9:24-27).Tukatoka sehemu hiyo na kwenda sehemu ingine.

UTEMBELEO WA MALAIKA URIELI
Malaika Gabrieli alinichukua mpaka kwenye nyumba nzuri sana .Tulipofika pale tuka kaa kwenye kiti.Mara ghafla nikasikia kiashiria kikubwa Mbinguni na malaika akapiga magoti na kuanza kusema, “Utukufu uwe kwa MUNGU,Yeye anastahili kupokea utukufu wote.AMENI !” Malaika Gabrieli akaniambia mimi niangalie.Tazama !nkaona malaika akikimbia na kupiga kelele akisema, “Ushindi ! Ushindi ! Ushindi !” Malaika akakimbia kwa YESU nakusema, “AMEINGIA ! AMEINGIA ! ”Nikamuona mtu akija kwenye Ufalme wa Mungu.Malaika akamkimbilia kumchukua kumuingiza ndani kwa sababu alikuwa tayari amechoka.Afadhali ameweza kuingia mbinguni ! Malaika Gabrieli akasema, “Malaika anayepiga kelele ‘USHINDI ! USHINDI !’ alikuwa ni malaika mlinzi wa yule mtu aliyeingia Mbinguni.”Mbingu yote ilijawa na furaha kwa sababu ya mtu aliyefanikiwa kuingia.Malaika Gabrieli akatoka nje ya chumba na kuniambia, “Senayon, unakaribishwa !”na alinikabidhi kwa Malaika Urieli ili kunionyesha baadhi ya vitu Mbinguni.
Malaika Urieli akanichukua mpaka sehemu ingine na kuniambia, “ANGALIA! .ANGALIA !.”Nikaona Ufalme wa Shetani.Shetani alikuwa akiwapa mapepo amri ili kuvamia Wakristo kwa sababu ya yule mtu aliyefanikiwa kuingia mbinguni.Shetani alisema, “Msiruhusu yeyote yule kukwepa mitego yetu na uvumbuzi wetu.Lazima tuzipate roho zao !.”Nikaona mapepo , yakikimbia na kasi kubwa kwa sababu roho moja imefanikiwa kuingia mbinguni.
Malaika Urieli alinichukua mimi kwenda sehemu na kusema, “Angalia duniani.”NIkaona dunia imeonekana ndogo sana na chafu sana kama sehemu ya kuweka uchafu.Mara ghafla ! nikaona mishale mingi ikaanza kuanguka duniani.Nikamuona Mtu Mzee aliyepokea mishale michache.Baadhi ya mishale hiyo iliangukia watu wengine waliopo duniani.Nikaona moto ukija duniani lakini yule Mtu Mzee akausimamisha ule moto na kuurudisha ulipotoka.Nikamuuliza Malaika Urieli, “Tafadhali nitafsirie hiki kwa sababu ni maajabu sana kwangu.”Malaika Urieli akasema, “Mtu Mzee uliyemuona ni YESUKRISTO, na mishale michache iliyompata katika mwili wake ilikuwa ni mishale ambayo shetani anatuma kinyume na watoto wa MUNGU.(Zaburi 91:1-7).Mishale mingine iliyo anguka kwenye dunia ilikuwa ni mishale kutoka kwa shetani kwa watenda dhambi.(Zaburi 92:7) Moto uliouona ni mipango ya shetani ya kuharibu dunia lakini Kristo hakuruhusu hicho kitokee.”(Isaya 60:1-2)

MALAIKA AKIWA NA TAARIFA MBAYA ZA MTU
Malaika Urieli akanichukua mpaka sehemu ambayo niliona malaika wengi wakitoa taarifa mbaya kwa Bwana.Malaika wa kwanza alikuja na kumwambia Bwana, “Mwishowe , Amepoteza roho yake.Nilimuonya lakini hakunisikiliza mimi.”(Marko 8:36).
Malaika wa pili akamwambia Bwana, “Bwana, yule mtu amefanya uzinzi.Nilimuonya asifanye lakini akamruhusu shetani kuutumikisha moyo wake.”Bwana akamuuliza malaika, “Ulimwambia akiri kosa lake ?”Malaika akajibu , “Ndio, lakini kila akitaka kukiri yule mwanamke aliyefanya naye uzinzi anajitokeza na huyu hushindwa kukiri tena anapomuona yule mwanamke aliyefanya naye uzinzi.”Bwana anamwambia, “Endelea kumwambia akiri na kuacha (dhambi zake )naye ataokolewa.”(Mithali 28:13)
Malaika akajibu, “Sawa BWANA.” Na akaondoka zake. 
Malaika wa tatu akaja naye alikuwa malaika mlinzi wa mchungaji W.F Kumuyi.Malaika akamwambia Bwana, “Bwana, shetani ametuma baadhi ya watu waovu kwenye huduma ya DEEPER CHRISTIAN LIFE (Kanisa la Mchungaji W.F Kumuyi), kifanyike nini ?” Bwana akamjibu, “Mwambie Kumuyi, mtumishi wangu awe muombaji na nitampa USHINDI.”Malaika asema, “Haya BWANA.”Akaenda zake(1 wathesalonike 5:17).Malaika wengi walikuwa wakija pale.Kitu kilichokuwa nikikisikia sana ni, “Mwishowe, amepoteza roho yake.”
                                                        NYUMBA YA MCHUNGAJI E.A ADEBOYEKipindi malaika aliyekuwa akitoa taarifa kuhusu mchungaji W.F.Kumuyi alipo ondoka, Nilimuuliza Bwana kama mchungaji E.A.Adeboye ni mtumishi wake au sio.Bwana akasema, “Ndio mchungaji Adeboye ni mtumishi wangu na mimi ndiye mwanzilishi wa REDEEMED CHRISTIAN CHURCH.Angalia ile nyumba.” Nikaangalia na kuona nyumba kubwa mbinguni.Bwana akasema, “Hio ndiyo nyumba ya mchungaji Adeboye , mtumishi wangu.”
Nilipiga kelele, “Hii nyumba kubwa ! unahakika atakuja kuingia ?” Bwana akasema, “Ndio kama akiendelea kufanya mapenzi Yangu na kuzidi kuvuna watu kwa Ufalme Wangu.”(Mathayo 28: 19-20).
Nikamuuliza Bwana anionyeshe nyumba yangu.Bwana akatabasamu na kusema, “Iangalie mwanangu.” Nikaona nyumba ndogo nzuri.Bwana akaniambia ni yangu.Nikacheka na kusema, “Lakini sijawahi lipa fungu la kumi.” Bwana akatabasamu na akasema, “Sio zaka pekee zinazo jenga nyumba hapa, lakini, pia unapowahubiria na kuwa ambia watu kuhusu Mimi na wokovu, hiyo ndiyo thawabu inayojenga nyumba huku mbinguni; unaponiletea watu hiyo nayo ni thawabu kubwa ya kujenga nyumba yako mbinguni.pia unapo waombea watu hiyo ni thawabu ingine kubwa inayopelekea kujenga nyumba.Unapotenda vyema kwa wengine nayo ni thawabu kubwa kwa wewe kujenga nyumba mbinguni.Kama watu wanataka kujenga nyumba hapa wanatakiwa watii kile nilichokueleza wewe.Hivyo, unayo hii nyumba kwa sababu umekuwa ukichukua muda mwingi kuomba kwa ajili ya wenginehaswa katika kundi Nililolianzisha:THE OVERCOMERS GROUP, na pia kwa sababu unawaambia watu kuhusu Mimi na kuleta watu Kwangu.”(Marko 1:15)
Malaika Urieli akanichukua mpaka kwa malaika Gabrieli ambaye alinionyesha mimi jinsi hizi shuhuda zitavyokuwa kubwa duniani.Aliniambia mambo mengi ya siri kuhusu mimi.Malaika Gabrieli alinichukua mimi mpaka kwenye kumbi kubwa na tazama , Nikaona malaika wengi wakiimba sifa kwa Bwana.Walicheza vyombo vingi kulitukuza jina la MUNGU aliye JUU.Nikajiunga nao nikimsifu Bwana.Nyimbo zilikuwa zakuvutia.Sauti za malaika zilikuwa nzuri sana.Kulikuwa hakuna aibu mbinguni.Malaika walikuwa wakicheza.Wengine walikuwa wakiruka mara ghafla wakapiga magoti na kuanza kusema, “Utukufu uwe kwa MUNGU !”(Ufunuo 5:9-14) Nilikuwa na furaha kuwa kati yao nilipenda niwe pale milele, kumsifu MUNGU wa Utukufu(Ufunuo 4:11).Tukatoka.
Malaika Gabrieli akanichukua kunirudisha mpaka kwa Bwana Yesukristo.Bwana Yesukristo akaniambia, “Mwanangu, niambie mimi, nini unachotaka kuona hapa au kipi unachotaka mimi nikuonyeshe ?” Nikajibu, “YESUKRISTO , mapenzi yako yatimizwe kwa sababu unajua vyote ninavyotaka kuviona hapa.”
Akanichukua mimi na huku akitabasamu akisema, “Mwanangu,Njoo.
MATUNDA YA ROHO MTAKATIFU
Bwana akanichukua mpaka sehemu moja mbinguni kuna kioo kikubwa sana.Kwenye kioo hiko kimeandikwa matunda tisa(9) ya Roho mtakatifu.Bwana akaniambia, “Matunda yako tisa(9) ya Roho mtakatifu yanatakiwa yawe yamekamilika.Kama tuu moja limekosekana, huyo mtu hawezi kuja kwenye ufalme wa MUNGU kwa sababu viwango vyangu vya mbinguni vinasimama milele.”(Wagalatia 5:22-23)
UNYAKUO
Ujio wake Bwana YESUKRISTO,kutokea kwa YESUKRISTO katika anga kupokea Utukufu wake kwa tumaini kuu la wote wamwaminio.Ni mara na yeyote asiyenyakuliwa na KRISTO ataporudi ata “aachwa”(Mathayo 24:42-44).
Bwana akasema, “Mwanangu,njoo nikuonyeshe jinsi unyakuo utavyokua.Angalia kwa umakini sana.” Tazama ! nikaona kanisa kubwa duniani.Lina zaidi ya watu milioni tatu (3) wakiwa wapo kanisani, kulikuwa na kitu kama kongamano.Kufumba na kufumbua unyakuo ukatokea na tuu wanafunzi watatu (3) kati ya milioni tatu (3) wakaondoka na Bwana YESUKRISTO.Wengine wote wakaachwa ! (Marko 13:30-37).
Nikamuona muanzilishi wa hilo kanisa naye alikuwa ameahwa na alipiga magoti pale pale na kusema, “Oh Bwana, nina makanisa 200 na sikuwahi hubiri kweli, lakini sasa nimeachwa ,tafadhali nisamehe mimi.” Bwana akasema, “Umechelewa(unaweza ukatengeneza) tuu kama utavumilia na kukataa kupokea alama ya mnyama.”(Ufunuo 13:16-18) (Ufunuo 19:20).
Kama wewe ni mchungaji au muhudumu ambaye huihubiri kweli, kumbuka huwezi jitetea mwenyewe mbele ya MUNGU(1 Petro 5:2-4).
Nikaona shule ambapo mkuu wa shule alikuwa akihutubia wanafunzi.Mara ghafla ,mkuu wa hiyo shule akanyakuliwa na wanafunzi wakabaki (1 Petro 4:7).Nikaona mwalimu alikuwa akifundisha wanafunzi, mara nikaona wanafunzi watatu(3) na mwalimu wamenyakuliwa, wanafunzi wengine wote wamebaki.(2 Petro 3:9-14).
Nilimuona mama mjamzito alikuwa akienda zake nyumbani .Ujauzito wake ukapotea kwa sababu mtoto alinyakuliwa lakini mwanamke aliachwa(Mathayo 24:40-51). Kulikuwa na huzuni kubwa dunia nzima (Mathayo 25:31-46).Wakristo wengi walikuwa wameachwa kwa sababu ya dhana zao juu ya dhambi aliozigundua mwanadamu(Zaburi 106:39-40).
Bwana akasema, “Hivyo ndivyo unyakuo utakavyotokea.Ni muda wa kwenda duniani .YEYE ALIYE NA SIKIO NA ASIKIE ROHO WA BWANA AAMBIACHO KANISA.KESHENI NA KUOMBA ! ” Ndipo Bwana akanirudisha duniani.
OMBI LA MSAMAHA
Kama uko tayari kumpa maisha yako YESUKRISTO omba sala ifuatayo:
Unirehemu mimi, MUNGU kutokana na uzuri wa upendo wako; kutokana na neema zako ondoa maanguko yangu.Nioshe kutoka kwenye maovu yangu na unisafi dhambi zangu.Ninatambua makosa yangu na dhambi zangu,tazama nilizaliwa katika uovu na mama yangu alichukua ujauzito wangu dhambini.Tazama natamani kweli ndani yangu na maficho yangu yajue hekima yako.
Nifanye nisikie furaha na amani yako ;Mifupa iliyovunjika iingiwe furaha yako na urejesho wako.Ficha uso wangu kutoka kwenye dhambi, ondoa kila ovu langu na uniumbie moyo safi,Oh Bwana ; na uweke tena sawa roho yangu.
Usiniondoe kutoka kwenye uwepo wako na usimchukue Roho wako mtakatifu kutoka kwangu.Nirejeshe furaha ya wokovu na kuniinua nikiwa na uhuru wako rohoni mwangu.(Zaburi 51).Andika majina yangu kwenye kitabu cha Uzima.Na iwe furaha kuu Mbinguni juu ya wokovu wa roho yangu katika Jina la YESUKRISTO,Nimeomba.Amen !.
Tafadhali nakuomba SHARE kwa mwenzio; na kwa shuhuda nyingi zaidi tembelea; www.jasirimbarikiwa.blogspot.com .SHARE kwa wengine nao.

MAONO JUU YA SIKU ZA MWISHO, KANISA, UNYAKUO, MBINGU NA KUZIMU na Othusitse Mmusi.

Maono aliyoonyeshwa na Bwana, ndugu Othusitsie Mmusi kutoka Botswana kuhusiana na Siku za mwisho, Mateso ya majaribu, Dunia katika vita, Uchumi utavyoanguka, Malango ya kuzimu yamefunguliwa, Mashambulizi ya kiroho, Hali ya kanisa, utayari wa unyakuo, mbingu na kuzimu.Maonyo makuu kutoka kwa Bwana ili wote wenye masikio wasikie ili wajiandae wenyewe.

Jumapili ya mwezi wa 8,tarehe 30 mwaka 2015 mida ya saa 9 usiku.Nilikuwa kitandani mwangu na ghafla macho yangu ya kiroho yakafunguka Nikaona nje ya paa la nyumba wakati nipo ndani ya nyumba, nikaona nyota na anga.Ghafla nikawa nje ya mwili,nikasafiri katikakatika anga kwa mwendo mkubwa.Nikaona nyota na anga.

MATESO YA MAJARIBU KWA WAKRISTO
Bwana MUNGU akaanza kunionyesha mateso ya siku za mwisho kwa waKristo, Nikawaona waKristo wamekamatwa, wanapelekwa jela, Nikawaona wachungaji wamekamatwa, Nikaonyeshwa kwenye gazeti na majina ya wachungaji na makanisa waliofungwa.Nikaona watu wamekaa chini wakipanga nani anayefuta kufungwa.Haya yalikuwa yakionekana sehemu mbali mbali duniani,Hasa mashariki na kati.Nilionyeshwa wanawake, watoto na waume wakiuwawa kwa njia mbalimbali, wakikatwa, roli lililojaa watu waliotekwa,watu walikuwa wakilia na kuogopa wengine walikuwa wakikimbia kujaribu kujificha na hao watesi.ilikuwa inaumiza sana.Bwana akasema nami, “Hii ni ishara ya ujio WANGU u karibu”.
Mathayo 24:9-“Wakati huo watawasaliti ninyi mpate dhiki, nao watawaua; nanyi mtakuwa watu wa kuchukiwa na mataifa yote kwa ajili ya jina langu.
10 Ndipo wengi watakapojikwaa, nao watasalitiana, na kuchukiana.
 11 Na manabii wengi wa uongo watatokea, na kudanganya wengi.
 12 Na kwa sababu ya kuongezeka maasi, upendo wa wengi utapoa.
 13 Lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.”
Mathayo 24:33-“33 nanyi kadhalika, myaonapo hayo yote, tambueni ya kuwa yu karibu, milangoni.”

VITABU VYA KIKRISTO, MAKANISA NA FACEBOOK PEJI
Bwana MUNGU akanionyesha stoo ya vitabu vya kiKristo Nikaangalia katika mashelfu na vitabu vingi na vilivyoandikwa na waKristo lakini vyote vinahusu “Furahia maisha”, “Mafanikio katika maisha”, “Funguo za utajiri”.Nikaangalia karibu vitabu vyote vilikuwa vina masomo hayo ya kufanana.Nikauliza tafadhali naweza  kupata kitabu kinachohusu Kuzimu ,Mbinguni au Unyakuo.Nikashangaa sana katika stoo kubwa yenye vitabu vingi sana vya kikristo nikaletewa kitabu pekee kimoja tuu nacho ni kidogo sana ndicho pekee kinachohusu mambo ya kuzimu na mbinguni.

Bwana MUNGU akanichukua na kunionyesha majina ya makanisa tofauti tofauti na waanzilishi wake.Katika hayo nikaonyeshwa ujumbe mkuu na unahubiriwa mara kwa mara katika hayo yote makanisa ni ujumbe unaohusu “Mafanikio katika maisha”.Nikaonyeshwa kanisa moja lilikuwa dogo sana ndilo lilikuwa linajali kuwa andaa watu wake kwa ajili ya ujio wake Bwana YESUKRISTO.
Uwiano wa makanisa yaliokuwa yanahubiri bibilia kikamilifu na kuweka msisitizo kuhusiana na mambo ya milele, ilikuwa ni kama 1:20 kama hesabu ya makanisa yote ya ile orodha.
Ndipo Bwana akafungua kioo, Nikaona Fesibuku peji(Facebook page) nyingi sana, Na nyingi zake zilikuwa zikijikita kufundisha watu kuishi vyema,kufurahia sasa maisha, kupokea baraka na fedha, Baada ya hayo nikaona peji (page) iliyojikita kufundisha watu nini kinachofuata baada ya haya maisha,kuzimu, unyakuo, mbinguni na utakatifu.

Nikaangalia watu walio (like) hiyo peji(page) niliona majina ya marafiki zangu wawili tu,na hao wengine nilikuwa siwa fahamu.Nilishangaa kwa nini peji(page) zenye ujumbe wa maana zina watu wachache ukilinganisha na zingine.Na kwanini wakristo wachache sana ninao wafahamu walio like peji hizo.

Bwana akaniambia “Mwanangu, Hii ni hali ya kanisa LANGU, Hii inakuonyesha watu wangu wengi wasivyokuwa tayari kwa ujio WANGU.Wengi wanasumbikia vitu vidogo badala ya kusumbukia kunipendza MIMI.Watu wangu wachache sana ndio wako tayari kwa unyakuo WANGU,Kama ndio ningekuja sasa ,wachache ndio wangenyakuliwa, Waonye sasa, Muda ni mfupi sana sana.”

2 Timotheo 4:1-4 “1 Nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu walio hai na waliokufa; kwa kufunuliwa kwake na kwa ufalme wake;
 2 lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho.
 3 Maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima; ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia waalimu makundi makundi, kwa kuwa wana masikio ya utafiti;”
 4 nao watajiepusha wasisikie yaliyo kweli, na kuzigeukia hadithi za uongo.”

YOHANA MBATIZAJI, UNYAKUO, MTAZAMO WA MBINGUNI NA KUZIMU.
Jumatatu, mwezi huo huo,31,2015.Asubuhi Bwana akafungua macho yangu ,Nilikuwa nimesafiri kwenye dunia ndipo likaja jangwa, Nikamuona mtu ambaye inaonekana kama anaishi hapo katika hiyo nchi.Alikuwa ana mavazi yaliyotengenezewa na ngozi ya mnyama na manyoya.Nywele zake zilikuwa ndefu,Naye alikuwa akipaza sauti katika jangwa kama vile akihubiri,Bwana akafanya nielewe kuwa alikuwa ni Yohana mbatizaji, Nikaona watu wengi wanamjia ili kusikia ujumbe wake.

Bwana akaniambia, Ninatuma wahubiri ambao watakuwa kama Yohana mbatizaji na wataandaa njia kwa ajili ya kuja kwake BWANA, Hao wahubiri wataohubiri TOBA na kufanya watu WANGU wawe tayari kwa ujio WANGU”.
Malaki 3:1 “1 Angalieni, namtuma mjumbe wangu, naye ataitengeneza njia mbele yangu; naye Bwana mnayemtafuta atalijilia hekalu lake ghafula; naam, yule mjumbe wa agano mnayemfurahia, angalieni, anakuja, asema Bwana wa majeshi.”
Mathayo 3:1-6 “1 Siku zile aliondokea Yohana Mbatizaji akihubiri katika nyika ya Uyahudi, na kusema,
 2 Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia.
 3 Kwa sababu huyo ndiye aliyenenwa na nabii Isaya, akisema, Sauti ya mtu aliaye nyikani, Itengenezeni njia ya Bwana, Yanyosheni mapito yake.
 4 Naye Yohana mwenyewe alikuwa na vazi lake la singa za ngamia, na mshipi wa ngozi kiunoni mwake; na chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu.
 5 Ndipo walipomwendea Yerusalemu, na Uyahudi wote, na nchi zote za kandokando ya Yordani;
 6 naye akawabatiza katika mto wa Yordani, huku wakiziungama dhambi zao.”

JE, UNYAKUO TAYARI ?
Bwana MUNGU akanichukua na kunionyesha siku hizi hizi duniani, nikiwa nimesimama na viumbe vya kimbingu na nilipo inua macho yangu juu ,Niliona jambo la ajabu nikaona upinde mkubwa , wingu linalong`aa na utukufu wa MUNGU ulikuwa unang`aa.Nikaona mianga myeupe inatembea  tembea kwenye mawingu na niliweza kusikia sauti kutoka huko,Nayo ilikuwa inakuwa kila sekunde ndipo nikajua hili ni wingu la kupokea ujio wa YESUKRISTO.Nikajua muda wowote tokea sasa unyakuo unaweza tokea hivyo vitu katika anga vikazidi kukua na kuongezeka hasa anga la mashariki.Nikaangalia duniani, nikaona watu wengi, wakristo, nao walikuwa hawaoni lolote walikuwa wakiendelea na shughuli zao wako bize kila siku na shughuli zao za siku kwa siku wako huru hata kutenda dhambi kama siku nyingine.Kwa wao ni siku kama siku zingine.Nilijua kuwa muda wowote unyakuo utatokea.

Bwana akaniambia “Mwanangu,angalia, hawakeshi wala kuomba,Sio wakeshaji kwa ajili ya ujio WANGU,Wako kwenye usingizi wa kiroho pamoja na dunia, Hawajui ishara hata ishara zangu za ujio Wangu,Hawajui si muda nachukua KANISA”
Mwili wangu ukawa mwepesi kwa uzito nikajisikia kama nimebadilishwa, Nikajiona mwepesi kwa uzito, mwili unaweza ukawa kwenye hewa na kuja chini, kama vile putolinalo nyanyuliwa na upepo  na kushushwa chini tena,Nilikuwa naenda juu na chini kama vile kuna kitu kinataka kutokea.
-Luka 21:36 “Basi, kesheni ninyi kila wakati, mkiomba, ili mpate kuokoka katika haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
-Ufunuo 22:7 “Na tazama, naja upesi; heri yeye ayashikaye maneno ya unabii wa kitabu hiki.”
MBINGU
Mara nikapelekwa mbinguni, Kitu cha kwanza nilichokiona kilikuwa ni paradise hali ya hewa ya mule ilikuwa nzuri sana yenye amani kutoelezeka.Kulikuwa na mianga kila kona,niliona maeneo makubwa na mashamba yanayoonyesha ni vigumu kuona mwisho wake.Niliziona bustani nzuri na zenye kupambwa kwa maua na chemi chem za maji, Nikaona mwanga wa dhahabu unaongaa kwenye bustani, niliona miti ya mapori iko sawa sawa.Nikaona wanyama wenye nguvu na afya, Nikaona ndege wa kila aina ,vitu vya mbinguni vya shangaza kupita kawaida nilibaki kujisemea “wow”, “vizuri sana” “utukufu”.nikasikia furaha na amani isiyo ya kawaida katika roho yangu.

Nikaja kwenye mji wa Mbinguni , Nikaona mitaa ya dhahabu ,nikaona majumba,jumba la kwanza nililoliona lilikuwa kubwa sana na zuri mno lililochukua eneo kubwa ,nilijua kwa ufunuo litakuwa na vyumba vya kulala mia, vifaavilivyotumiwa kujengea nyumba hiyo havijawahi onekana hapa duniani. Lilikuwa likiwaka waka,lenye rangi mbali mbali na refu , Nyumba ingine ilikuwa kubwa kuliko ya kwanza niliyoiona, na yatatu niliyoiona ilikuwa kubwa kuliko ya pili.Zote zilitengenezwa kwa malighafi za mbinguni.Bwana akaniambia: “Hao ni watumishi Wangu walionitumikia kwa uaminifu duniani,Pia kuna majengo makubwa zaidi ya hayo”.
Bwana akaniambia; “Nitakuchukua wewe muda mwingine na kukuonyesha jumba la Ibrahim na Paulo”.Nikajua majengo yao yatakuwa makubwa sana kulingana na vile Bwana alivyo nieleza na kutokana na uaminifu wao na kazi kubwa walioifanya kwa MUNGU imewapa majumba makubwa mbinguni.
Bwana akaniambia “Kuwa mtii na mwaminifu katika kufanya kile nilichokuitia kukifanya”
-Yohana 14:1-3 “1 Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi.
 2 Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali.
 3 Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo.”
-1 Wakorintho 4:1-2 “1 Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu.
 2 Hapo tena inayohitajiwa katika mawakili, ndiyo mtu aonekane kuwa mwaminifu.”
Niliona sehemu, ambako kila kitu kilikuwa kinang`aa dhahabu, Mwanga wa dhahabu wa uwepo wa udhihirisho Wake, Maua pia yalionekana ya dhahabu.Sikutumia muda mwingi hapo.
Mji wote wa mbinguni ulikuwa unamwanga,rangi nzuri,uzuri na uhai.Nilikuwa nikipiga kwa sauti msifu MUNGU!,msifu MUNGU !,Pia vitu vingi vilijitokeza kipindi ambacho nilichokuwa naenda kwa spidi ya mawazo,Nakuwa mara moja katika sehemu MUNGU aliyotaka mimi niwe.
MTAZAMO WA KUZIMU
Mara nikajikuta nje ya mbingu ,nkapelekwa sehemu za chini za dunia ,nikaona Kuzimu, kulikuwa na giza la kutisha lililo samba,mapepo wa kila aina, watu walikuwa wakiteseka na moto na wakilia na kupiga kelele kwa uchungu , “awf !, awf !” na kuomboleza kwa roho zao kupotea.
VIPAO MBELE VYA MILELE
Mara nikatolewa nikawa ninakuja.Nilikuwa nina paa kwa spidi isiyo ya kawaida dunia nzima ,nikiona mataifa mbali mbali, wakila tamaduni,watu wa rangi zote.Nikasikia sauti kutoka kwa MUNGU mbinguni ikisema “Nenda na uwaambie watu wadunia kuwa umeiona mbingu na kuzimu.Nenda na uwaambie hao,kuwa umeona viumbe mbinguni na umeona mapepo ya kutisha Kuzimu pia,Nenda na uwaambie wanatakiwa wajiandae kwa ujio WANGU,Waambie nimetuma ujumbe huu,Waambie nitathibitisha pindi mtumishi WANGU atapohubiri ujumbe huu,Waambie saa hii, nnaweka thamani zaidi kuhubiri kuhusu utakatifu na ujio wangu kuliko mafanikio”.
- Zaburi 9:17 “Wadhalimu watarejea kuzimu, Naam, mataifa yote wanaomsahau Mungu.”
- 1 Petro 1:13-16“Kwa hiyo vifungeni viuno vya nia zenu, na kuwa na kiasi; mkiitumainia kwa utimilifu ile neema mtakayoletewa katika ufunuo wake Yesu Kristo. 14 Kama watoto wa kutii msijifananishe na tamaa zenu za kwanza za ujinga wenu;
 15 bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;
 16 kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.”
- 1 Timotheo 6:10 “Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi.”
Ghafla nikaoka katika maono.Nilishangazwa na kuanza kuongozwa kwa kile nilichokiona na kupitia.

MALANGO YA KUZIMU, roho ZA GIZA, SAUTI YA BWANA YESUKRISTO.
Jumamosi,Mwezi wa 9, tarehe 19,2015 saa kumi na moja(11) asubuhi.Macho yangu ya rohoni yalifunguliwa kwa uwazi ,Na kuangalia chini  nikaona malango ya kuzimu, Mara nikaona kundi la roho za giza zilikuwa zikitoka kwa kasi ,nilipoangalia kwa karibu ,nikagundua mapepo ya kila aina wengine wapo kama viumbe warukao na mbwa.Nao walikuwa wakipanda kuja duniani.
Ndipo nikasikia kwa sauti ya YESUKRISTO ikiongea wazi wazi kutoka mbinguni ikiongea kwa sauti kubwa setensi hiz tano.
1.    “MALANGO YA KUZIMU YAKO WAZI,
2.    LAKINI HAWATAWEZA KUSHINDA,
3.    WATU WENGI WATAANGUKA
4.    NA WATU WENGI WENGINE WATAINUKA
5.    LAKINI ATAKAYEVUMILIA MPAKA MWISHO ATAOKOLEWA”
Ghafla nilipokuwa nikaona kitu kilichonishtua nikaona wachungaji wengi wakubwa na maarufu, baadhi wakianguka katika dhambi , na hawakutubu na hakuna anayejua na wengi kushindwa kuingia mbinguni.
Ilikuwa ni mchanganyiko ,wa mbio tofauti tofauti, niliweza kerejesha kwa kiasi tu kumbukumbu yake.Zile roho zilizokuwa zinatoka kuzimu , nyingi zake zilikuwa ni roho zinazoleta kuhamasisha dhambi za uasherati,uzinzi na kila aina ya matamanio, ndiyo maana watu wengi walianguka.Nilikuwa nikiruka karibia na mwisho, kulikuwa na kila aina ya mapepo duniani,kwa kutongoza, na kufanya kila aina ya uovu.
Nakumbuka nililia nikisema “Bwana YESU, niokoe niokoe mimi kutoka kwenye huu mtego wa shetani, tafadhali, tafadhali  nisaidie kuwa mwaminifumpaka mwisho”.Nilikuwa katika machozi nikiomba,kuona jinsi gani shetani anawaharibu watu.Niliangalia maisha yangu kama nacheza na movi,sasa mpaka karibia mwisho, kutembea na Bwana,Na ilipofika mwisho ,maono yalinyanyuliwa juu kwa haraka.Nilitetemeka kutokana na kilichoko duniani na kuhusu wakristo wengi ambao wanaanguka na kushindwa kuingia mbinguni ,hata wale wachungaji wakubwa na maarufu sana.
Niliwahi rudi nyuma na kuacha wokovu kipindi nilipokuwa kijana,Bwana alinionyesha sehemu na kunipa nafasi ingine.
Katika hizi siku za mwisho tunatakiwa kila siku kuwa na ushirika mkubwa na MUNGU,Tunatakiwa kusoma neno la MUNGU,kufunga na kuomba, Tunatakiwa tuwe na marafiki/makundi mazuri, hatutakiwi kukosa kusanyiko la wapendwa (Kanisa na Ushirika).
“21 Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
 22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?
 23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.”-Mathayo 7:21-23
- “8 Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.” 1 Petro 5:8

VITA YA TATU(III) YA DUNIA, GIZA NA KUANGUKA KWA UCHUMI
Jumatatu ya mwezi septemba,21,2015.Asubuhi mishale ya saa mbili.Nilionyeshwa kuna wanajeshi wengi sana wakiwa kutoka nchi mbali mbali wakiwa na gwanda tofauti tofauti kulingana na mpangilio wa nchi zao.Wakiwa tayari kwa vita,Marekani na walioungana nao,China na walioungana nao,Kulikuwa na bunduki nyingi sana, wanajeshi wa miguu,Silaha za kila aina.Inaonekana vita ya dunia ya tatu(3) ikiwekwa tayari kuanza.
Niliona giza la ajabu lililofunika ardhi,anga,na umemeulikuwa haupo kwa baadhi ya maeneo,Watu wengi wakaenda kujificha katika makanisa ili wapate ulinzi.Niliona Nikaona sehemu watu wakiwa maelfu ya watu, vijana, watotot na wakubwa ,wako wakiwa wakimbizi katika nchi zao wenyewe.

Niliona uchumi ulioshuka , kuwa mbaya na watu wakishindwa kutoa fedha kwenye ATM.Katika maono hayo hali iliyo karibu sana na kujua mapema mapema tarumbeta italia, kanisa litanyakuliwa na dunia ikaachwa katika dhiki kuu.Ghafla nikatoka katika maono hayo.

-“ 25 Tena, kutakuwa na ishara katika jua, na mwezi, na nyota; na katika nchi dhiki ya mataifa wakishangaa kwa uvumi wa bahari na msukosuko wake;
26 watu wakivunjika mioyo kwa hofu, na kwa kutazamia mambo yatakayoupata ulimwengu. Kwa kuwa nguvu za mbinguni zitatikisika.
27 Hapo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika wingu pamoja na nguvu na utukufu mwingi.
28 Basi mambo hayo yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia.”-Luka 25-28
SHARE KWA WENGINE 
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...