Mkate


Mambo ya kufanya unapokabiliwa na vita

Kuna mambo ambayo mtu anatakiwa kuyafanya anapokabiliwa na vita au magumu katika maisha yake.Nayo hayo yatakuwa msaada katika kumaliza vita yake katika ushindi mkuu na vizuri zaidi.

Mambo yakufanya uanapokabiliwa na vita ni pamoja na:-

i.Kusamehe

Imeandikwa “Lakini kama ninyi hamsamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe niny i makosa yenu.” Marko 11:26.Mtu anapopitia vita, anapopitia mambo magumu mara nyingi watu wanaomkejeli na kumcheka ni watu wa karibu yaani watu wa nyumbani.

Unaweza kutendewa ubaya na watu wa karibu.Ukatendewa ubaya wa makusudi kabisa lakini unabidi uwasamehe.Jifunze kusamehe kwa kuwa wewe pia umepokea msamaha kutoka kwa Mungu kwa njia ya Yesukristo.

Yusufu aliwasamehe wale ndugu zake waliotaka kumuua wakamuuza.Yusufu alimsamehe hata mke wa mfalme aliyemsingizia kuwa amembaka “Yusufu akawakalisha babaye na nduguze, na kuwapa milki katika nchi ya Misri, katika mahali pazuri pa nchi, katika nchi ya Ramesesi, kama Farao alivyoamuru.” Mwanzo 47:11

Yusufu haku muhukumu wala kuacha kumsamehe mtumwa aliyekuwa amemsahau kumtaja taja kwa mfalme “Ila unikumbuke mimi, utakapopata mema, ukanifanyie fadhili, nakuomba, ukanitaje kwa Farao, na kunitoa katika nyumba hii”mwanzo 40:14.

“ Lakini huyo mkuu wa wanyweshaji hakumkumbuka Yusufu, alimsahau.” Mwanzo 40:23.Yusufu alimsamehe hata mnyweshaji kwa kuto kumkumbuka na kumsahau kumtaja taja kwa mfalme.

Leo kuna watu wengi wanalalamika kwamba mdogo wangu nilimsomesha mwenyewe lakini leo amenisahau, leo watu wanalalamika mimi mtu huyu tulianza nae maisha alikuwa hana hata kitanda tulianza chumba kimoja tukafanikiwa, tukanunua gari tukajenga kumbe vitu vyote alikuwa ananunua kwa jina lake leo sasa amenifukuza.

Wengine wanalalamika kwa kuniambia mchungaji huyu kaka nilimsomesha kabisa na wakati ule ulikuwa ni wakati mgumu sana kwangu, Ila nilivumilia yote nimsomeshe kwa kuwa aliniahidi atanioa, lakini baada yakumaliza masomao yake amenikimbia na kwenda kumuoa msichana mwingine.


Watu wanaweza kukutenda vibaya kipindi cha vita yako, wanaweza wakawa wanakuwazia mabaya hata wanaweza kukusema vibaya.Lakini unatakiwa uwasamehe haijalishi makosa yao au wanaukaribu na wewe kiasi gani, inabidi uwasamehe tuu.
Vita aliyokuwa anapambana nayo Daudi ukisoma katika biblia, “Sauli akajaribu kumpiga Daudi hata ukutani kwa mkuki wake, ila yeye akaponyoka kutoka mbele ya Sauli, nao huo mkuki akaupiga ukutani; naye Daudi akakimbia, akaokoka usiku ule” 1 Samweli 19:10
Ilifika kipindi ambacho daudi anajua kuwa anawindwa na sauli ili auwawe lakini daudi alimsamehe sauli hata pale ambapo alipata nafasi ya kumuua.

Imeandikwa “Nao watu wa Daudi wakamwambia, Tazama, hii ndiyo siku ile aliyokuambia Bwana, Angalia, nitamtia adui yako mikononi mwako, nawe utamtenda yo yote utakayoona kuwa mema.
Basi Daudi akainuka, akaukata upindo wa vazi lake Sauli kwa siri.Lakini halafu, moyo wake Daudi ukamchoma, kwa sababu amekata upindo wa vazi lake Sauli.
Akawaambia watu wake, Hasha! Nisimtendee bwana wangu, masihi wa BWANA, neno hili, kuunyosha mkono wangu juu yake,kwa maana yeye ni masihi wa BWANA.1 samweli 24:4-6

Daudi hakutaka kulipiza kumtenda vibaya Sauli ingawa Sauli aliazimia kumuua Daudi.ImeandikwaBwana atuamue, mimi na wewe, na Bwana anilipizie kisasi changu kwako; lakini mkono wangu hautakuwa juu yako.” 1samweli 24:12
Ili usiweze kutunza uchungu wa mambo mabaya ambayo yaliyokuwekea maumivu ni bora usamehe imeandikwa“hata kinyume cha hayo, ni afadhali mmsamehe na kumfariji, mtu kama huyo asije akamezwa katika huzuni yake ipitayo kiasi.” 2 Wakorintho 2:7
Marko 11:25 Nanyi, kila msimamapo na kusali, sameheni, mkiwa na neno juu ya mtu; ili na Baba yenu aliye mbinguni awasamehe na ninyi makosa yenu.

ii.Kumtegemea Mungu
Kumtegemea Mungu ni vyema kwa kuwa Yeye ndiye atupaye uwezo pale ambapo tumekwama.Imeandikwa “Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka;
bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia” isaya 40:30-31.
Kuna muda unafika ambapo mtu anaweza kupitia mabo magumu,vita kubwa na asiweze kupatikana hata mmoja wa kukutia moyo wala kukusaidia.Kama kuna watu ambao mtu anawategemea basi mtu huyo naye anaweza kufariki muda wowote na ukakosa msaada.
Kwa hiyo katika vita yako mtegemee Mungu naye atakuokoa katika wakati ambao haukuutarajia kabisa, Mungu anaweza kukupigania na kukuokoa kwa  kuwa tuu umemtumainia.

iii.Kukiri ushindi kabla ya kutokea
Unapofikwa na vita katika maisha yako, jizoeshe kukiri ushindi hata kama huoni njia ya kutokea.Unapopitia mambo magumu hata ndugu na jamaa wanakukatisha tamaa,wewe zidi tuu kukiri ushindi hata kama bado haujatokea.

Imeandikwa “Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake.” Mithali 18:21.Maana yake mtu akisema atashindwa na atashindwa kweli kwa kuwa kuna nguvu kubwa katika ndimi zetu.

Kiri ushindi jinenee mema hata kama hali halisi hairuhusu kukiri ushindi.Kiri ushindi hata kama bado hauuoni ushindi wenyewe,Hakuna neno lolote utakalolinena ambalo Mungu halijui.Imeandikwa “Maana hamna neno ulimini mwangu Usilolijua kabisa, Bwana.” Zaburi 139:4

Badala ya kusema “nitakufa” wewe sema “sitakufa ili niyasimulie matendo ya Bwana”,badala ya kusema “nitashindwa katika hii vita” wewe sema “vita ni vya Bwana hakika nauona ushindi mkuu”.
Kuna nguvu katika kukiri au kusema kuna nguvu kubwa sana katika ulimwengu wa roho.Daudi alikiri ushindi dhidi ya goliati hata kabla ya ushindi wenyewe kuonekana.ImeandikwaNdipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe kwa jina la Bwana wa majeshi, Mungu wa majeshi ya Israeli uliowatukana.  
Siku hii ya leo Bwana atakuua mkononi mwangu, nami nitakupiga, na kukuondolea kichwa chako, nami leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya majeshi ya Wafilisti, ili kwamba dunia nzima wajue ya kuwa yuko Mungu katika Israeli.” 1Samweli 17:45- 46
Shadraka, Meshaki na Abednego walikiri kuokolewa na Mungu dhidi ya moto hata kabla hawaja uona wokovu wenyewe.Imeandikwa Ndipo Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakajibu, wakamwambia mfalme, Ee Nebukadreza, hamna haja kukujibu katika neno hili.
Kama ni hivyo, Mungu wetu tunayemtumikia aweza kutuokoa na tanuru ile iwakayo moto; naye atatuokoa na mkono wako, Ee mfalme.Bali kama si hivyo, ujue, Ee mfalme, ya kuwa sisi hatukubali kuitumikia miungu yako, wala kuisujudia hiyo sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha” Daniel 3:16-18

Naye Mungu aliwaokoa Shadraka, Meshaki na Abednego kwa kuwa walikiri ushindi kwa kumtegemea Bwana,Naye Bwana akawaokoa.“Kisha Nebukadreza akaukaribia mdomo wa ile tanuru iliyokuwa inawaka moto. Akanena, akasema, Enyi Shadraka, na Meshaki, na Abednego, watumishi wa Mungu Aliye juu, tokeni, mje huku. Ndipo Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakatoka katika ule moto.

. . . . . . . . . . . . . . . . wakawaona watu hao, ya kuwa ule moto ulikuwa hauna nguvu juu ya miili yao, wala nywele za vichwa vyao hazikuteketea, wala suruali zao hazikubadilika, wala harufu ya moto haikuwapata hata kidogo.” Daniel 3:26-27

Kwa hiyo siku zote pendelea kukiri ushindi katika jambo lolote lile unalolipitia kwa kuwa utakula matunda ya ulimi wako.Kiri ushindi ukimtegemea Bwana kuwa ndiye atakayekupigania.
kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu.Luka 1:37

No comments :

Post a Comment

Andika maoni yako hapa !! ... You may comment here !!!

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...