JIANDAE KUOLEWA/KUOA !!!!

Kama wewe ni mwanamke jiandae KUMTII mume wako.Jiandae kwa kung`ang`ania mapambo yasio haribika,yaani roho ya upole na utulivu na iliyo thamani mbele za MUNGU.
Imeandikwa “Ninyi wake, watiini waume . . . .  .”- wakolosai 3:18

 Je wewe kama mwanamke unayetarajiwa kuolewa upo tayari  kuongozwa na mume wako?
Mume /Baba ndio kichwa cha familia hata kama hana hela au hajui lolote yeye bado anakuwa kichwa cha familia maana yake maamuzi mengi yanategemewa yatoke kwake au yapitishwe kwa ridhaa yake.

Imeandikwa “Ni afadhali kukaa katika pembe ya darini, Kuliko katika nyumba pana pamoja na mwanamke mgomvi.”-mithali 21:9

Je wewe kama mwanamke unayetarajia kuolewa upo tayari kumtii mumeo kwa ajili ya mambo ambayo hujayapenda ?.
Inawezekana hujazoea kutii mtu yeyote lakini kama unahitaji uwe na ndoa yenye kudumu basi anza kujiweka vyema kumtii mume wako.

Asilimia tisini (90%) ya ndoa ambazo zimevunjika chanzo chake ni wanawake kutotii waume zao.
Utii kwa mumeo  unaweza geuza moyo wa mumeo unaweza fanya hadi mumeo abadilike kama huwa anakuwa mkali anaanza kuwa mpole,utii unaweza fanya.

Inaanza kama utani tuu mwanamke anakuwa hamtii mume wake kwa mambo madogo madogo.
Kwa wanawake wengi kutokutii waume zao kumechangia wanaume kutegeka kirahisi na wanawake ambao wanaonekana wana utii na hata kufanya wanaume hao walio oa tayari kuanza mahusiano na wanawake walio n`nje ya ndoa kwa kuwa tu wanapendezwa na utii wao.

Ukiona ndoa zinavunjika ujue sababu kubwa sio hizo wanazozitaja bali chanzo chake mwanamke alikuwa hana utii,haheshimu mumewe na hakubali aongozwe!.
Wanaume kwa asili hawawezi kuwa na furaha kukaa na mwanamke ambaye hamtii.

Kama  ndoa yako ina matatizo matatizo kama mwanamke sasa badili nia sasa na kuanza kumfanya mume wako ajisikie yeye ni kiongozi yeye ni msemaji wa mwisho wa mambo,ajisikie yeye ni mtu anaongoza na kutegemewa.

Haina maana kila anachosema ni lazima utii hapo hapo hata kama kina madhara lakini unaruhusiwa kumpa ushauri kwa upole na akaupokea vizuri.
Lakini hata kaa akubali ushauri wako endapo kila anachokisema kwako kinakuwa kibaya na unakikataa kwa kumdharau au kuonyesha hali yeyote ya kutokumtii.

Mwanamume jiandae kumpa mke wako heshima

Imeandikwa Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.”-Mwanzo 2:18.

Unataka ndoa yako idumu na iwe nzuri yenye furaha na amani inabidi ukubali kuishi kama MUNGU alivyotaka kwa kuwa yeye MUNGU ndiye muanzilishi wa ndoa.

Imeandikwa “. . . . . kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe.”-1 petro 3:1-7

Kama wewe mwanaume unataka uwe na ndoa yenye amani na kudumu inabidi ujifunze na ujizoeshe kumheshimu mchumba wako/mkeo.

Kila kitu katika maisha kinahitaji maandalizi,na maandalizi yanaweza kutengeneza kitu kikawa kizuri au kibaya kwa hiyo basi maandalizi ni msingi wa kila kitu.Kama unataka kitu kiwe kizuri sana basi inatakiwa maandalizi yake yawe mazuri sana.

Ukiona ndoa ya watu fulani imedumu muda mrefu kwa amani na furaha ujue kila mmoja wao alijiandaa hasa katika moyo wake.
Upendo au hisia pekee hazifanyi ndoa kudumu bali maandalizi ya kitabia ndio yanafanya ndoa kuwa vizuri.

Jiulize hili na upate kujua kuwa kila mtu anapofunga ndoa hua anamapenzi ya dhati kwa mwenzi wake,huwa ana hisia kubwa sana kwa mwenzi wake lakini hushangai baada ya muda watu hao huachana!!!.

Kwa hiyo kosa sio kuwa hawapendani bali hawana tabia zinazoendana kuishi katika ndoa. Kwa hiyo tabia bora katika ndoa ni muhimu  kuliko mali/fedha,upendo ,hisia na vinginevyo.

Maandalizi yakiwa kidogo yatatoa matokeo kidogo,Maandalizi yakiwa makubwa yatatoa matokeo makubwa.
Vivyo hivyo watu wengi wanapenda kuwa na ndoa nzuri zenye furaha na amani lakini hawawi na maandalizi yanayoendana kuipata ndoa nzuri kiasi hicho.

Kwanza kabla ya kuwaza kuoa au kuolewa unatakiwa ujiandae binafsi kuwa mzuri kabla ya kuwaza unataka mtu mzuri kiasi gani.Ninaposema mzuri ninamaanisha uzuri wa moyo na sio wa sura ingawa si tatizo kama nao ukiwa nao.

Mwanzilishi wa ndoa ni MUNGU hivyo ukitaka kuishi maisha ya furaha na amani katika ndoa yako inabidi uangalie na ufuatishe kila maelekezo ya muanzilishi wa taasisi hiyo yaani ndoa.
Kujiandaa kuolewa ni kujitazama mwenyewe kwanza kama  wewe ni mke/mume mwema?

Watu wengi wanaposikia swala la kuolewa/kuoa hufikiria kujiandaa katika maswala ya kiuchumi tuu yaani awe na mali na fedha ndipo aoe au aolewe pasipo kujua kuwa ni muhimu zaidi kuwa na maandalizi katika fikra na tabia kuliko kifedha na mali.

Kwa kuwa kinachofanya ndoa nyingi zivunjike sio kukosa mali/fedha bali ni kukosa tabia njema kati ya wawili hao     
Kwa hiyo kujiandaa kitabia ni vizuri zaidi kuliko kujiandaa kifedha. Huu ndio mwenendo mzima wa kutenda,kufikiri na kusema.


Hekima zitakazokusaidia kuishi vyema katika ndoa !
Hekima ni maarifa kamiliyanayoweza kukusaidia katika mambo mbalimbali.
Sasa kuna hekima inayohitajika kujifunza na kuitumia ili kuwa na ndoa nzuri katika maisha yako yote bila kutengana,wala kuachana.Hizo hekima nazo ni pamoja na :-
                                                                                                                                         
1.Jua namna ya kuutumia ulimi wako.
ImeandikwaMpumbavu hudhihirisha hasira yake yote; Bali mwenye hekima huizuia na kuituliza.”-Mithali 29:11
Kuwa mwenye uwezo wa kuongea mambo ya maana na katika wakati unaofaa.Tena ni bora kunyamaza kuliko kuongea mambo yatayochochea hasira.

Imeandikwa Asiye na akili humdharau mwenziwe; Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.
 Mwenye kitango akisingizia hufunua siri; Bali mwenye roho ya uaminifu husitiri mambo”-Mithali 11:12-13.


2.ONGEA KWA UPOLE
Haina haja yeyote ya kuongea mwenzi wako kwa ukali na si vyema kuongea kwa ukali na mwenzi wako.
Imeandikwa “Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.”-mithali 15:1

Tuwe na uvumilivu kwa magumu ili kuweza kuongea kwa upole na heshima na hiyo ndio hekima kuu.

Imeandikwa “Kwa uvumilivu mwingi mkuu husadikishwa; Na ulimi laini huvunja mfupa.”-mithali 25:15

3.Angalau Fikiri kabla hujaongea neno.

“Je! Umemwona mtu mwenye kuhamaki katika maneno? Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye”-Mithali 29:20
Kabla ya kutoa neno ni hekima sana ukiwa una fikiri kuliko kuongea mabaya juu ya jambo lolote kwa mwezi wako.Moyo wa mwenye haki hufikiri jinsi atakavyojibu; Bali kinywa cha wasio haki humwaga mabaya.”-mithali 15:28

Ongea kitu kwa namna ya kufundisha na namna ya kujenga nasio kulaumu au kukosoa ili eti uonekane uko mkamilifu sana.
“Moyo wake mwenye hekima hufundisha kinywa chake; Huzidisha elimu ya midomo yake.”-mithali 16:23


4.Angalau sikiliza kabla ya kuongea neno/usiwe mwepesi wa kuongea.
Imeandikwa Yeye ajibuye kabla hajasikia, Ni upumbavu na aibu kwake.”-mithali 18:13

Mabishano mengi katika mahusiano hutokea kwa kuwa tuu kuna mmoja kati yao ambaye hajamsikiliza mwenzie kwa kuongea pasipo kutaka kumsikiliza mwenzie.

 “Aliye na akili moyoni mwake atapokea agizo; Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka”-Mithali 10:8

5.Usiongeze chumvi
Imeandikwa “Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa; Wala asemaye uongo hataokoka”- mithali 19:5
Si sawa kuwa muongo yaani mtu wa kunena uongo ni bora uongee ukweli hata kama ukweli huo unaweza kuwa unaumiza sana lakini ni bora uuseme huo kuliko uongo.

Afadhali maskini aendaye katika unyofu wake, Kuliko mpotofu wa midomo aliye mpumbavu.”- mithali 19:1


6.Kuwa makini na utani/jinsi unavyotania.
Utani una asilimia 50% za kujenga na pia utani una asilimia 50 % za kubomoa.Kwa hiyo upomtania mpenzi wako kuwa sana makini na utani unaoufanya kwa kuwa unaweza utani huo ukamkwaza.

Imeandikwa “Kama mtu mwenye wazimu atupaye mienge, Na mishale, na mauti;
 Ndivyo alivyo amdanganyaye mwenzake, Na kusema, Je! Sikufanya mzaha tu?”-Mithali 26:18-19

7.Penda kutumia maneno yanayojenga katika maongezi yako
Ongea mambo yanayojenga kwa maneno ya kuvutia hata kama yeye huwa hafanyi hivyo.
Imeandikwa“Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga; Bali ulimi wa mwenye haki ni afya.”-mithali 12:18

Kuna mambo ambayo mtu akiambiwa moja kwa moja anakuwa na furaha na amani. Mfano neno:nakupenda,pole,asante,samahani,nisamehe na n.k
“Uzito katika moyo wa mtu huuinamisha; Bali neno jema huufurahisha.”-Mithali 12:25


Kuishi katika ndoa yenye amani na upendo si bahati nasibu si kamari bali ni kuamua na kupangilia kwa kujizoesha tabia njema.











KANSA ZINAZOSABABISHWA NA KUSIKILIZA MUZIKI WA BONGO FLEVA


Watu wengi hawafahamu kuwa muziki wa kidunia una nafasi kubwa ya kuwaletea hatari katika maisha yao ya kiroho.




Tambua kuwa mambo ambayo yanatokea katika ulimwengu wa kimwili yanakuwa yameanza katika ulimwengu wa kiroho ,kwa hiyo ukiweza kuudhibiti ulimwengu wa kiroho ndio umeweza kuumeudhibiti ulimwengu wa kimwili.




Kabla ya kuainisha kansa zitokanazo na muziki wa kidunia kwanza pata kujua athari zinazotokea kutokea kutokana na kusikiliza muziki wa kidunia.
HATARI YA MUZIKI WA KIDUNIA KATIKA MAISHA YA KIROHO
Kuna madhara mengi yanayotokea katika maisha ya kiroho pale mtu anaposikiliza muziki wa kidunia.Baadhi ya madhara hayo ni pamoja na:-

1.UKIRI MBOVU  


Nyimbo zinapoimbwa baadaeKinywa kinanguvu sana na maneno mengi katika muziki wa kidunia yanakiri madhaifu, mfano muziki unaimba unasema “sisi tu masikini sana” Sasa unapoimba nyimbo kama hiyo inakufanya ukiri vitu ambavyo sivyema katika ulimwengu wa kiroho na kimwili pia kwa kuwa imeandikwa “Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake.”-Mithali 18:21.


Kwa hiyo unapoimba “sisi tu masikini sana” unakuwa unautengeneza umasikini katika ulimwengu wa kiroho na si muda umasikini huo utakuja kujitokeza katika masha ya kimwili.
Mtu yeyote aliye hai kiroho hawezi kukiri au kusema sema hovyo hovyo kwa kuwa kwa kusema sema hovyo huko ndio kunapelekea hayo mambo kutokea katika maisha yake.

Mfano:Ukikiri “kushindwa”nawe utashindwa ,ukikiri “maisha magumu” na kweli kwako wewe yatakuwa maisha magumu hata kama yalitaka kuwa maraisi kwa kuwa shetani atashikilia uthibitisho wa neno lako ulilolisema.
Kwa hiyo kutokana na muziki wa dunia utajikuta kwenye hatari ya kujikuta ukiimba vitu visivyo na maana ukadhani inaishia hapo tuu,kumbe inakwenda kuathiri ulimwengu wako wa kiroho kwa kukiri vibaya baadhi ya mambo katika maisha yako tuu kwa sababu ya kufuatisha na kuziimba nyimbo za kidunia.

2.KUISHI KATIKA ULIMWENGU WA KUFIKIRIKA
Muziki wa kidunia unafanya watu wengi waishi katika ulimwenu wa kufikirika yaani ulimwenu usio halisi kwa kuwa nyimbo nyingi za kidunia huwa haziongelei maisha ya kawaida bali maisha ya kufikirika.
Kuazia anayeimba mpaka anaye kwenda kuusikiliza muziki wa dunia huwa wanajikuta wakiishi katika ulimwengu wa kufikirika yaani kuishi katika ulimwengu ambao si halisi.

3.KUPATANISHWA NA KUZIMU

Mara nyingi wasanii wanaoimba muziki wa kidunia huwa wanafanya mapatano na kuzimu ili wapewe nguvu katika kazi zao za muziki wa kidunia ili pindi zitokapo zifanikiwe sana kwa kusikika ,kupendwa na hata kukubalika. 

Kupitia muundo wa video za miziki ya kidunia kuna baadhi ya vitendo vyao katika mkanda(scene) vinakuunganisha na ushetani .mfano katika picha chini.


Hivyo kwa kusikiliza miziki ya kidunia unaweza jikuta ukipatanishwa na kuzimu kutokana na maagano husika juu ya miziki yao.
Pia mtu anaweza kuzidi kuungana nao hata kupitia style(maisha binafsi) mfano ni :-

        i.            Kupitia tattoo.

Imeandikwa “Msichanje chale yo yote katika nyama ya miili yenu kwa ajili ya wafu, wala msiandike alama miilini mwenu; mimi ndimi Bwana.” Mambo ya Walawi 19:28.


Unapokuta baadhi ya waimbaji wa muziki wa kidunia wana michoro katika miili yao maarufu kama tattoo ni wazi kuwa wana maagano ya moja kwa moja na nguvu za giza juu ya kazi zao za muziki .

Sasa pale mtu mwingine anapoiga ile tattoo aliyekuwa nayo muimbaji flani wa muziki wa kidunia inamfanya naye aingie kwenye maagano ya kishetani pasipo kujijua.

      ii.            Kupitia ishara za vidole.

Kwa kusikiliza  muziki wa kidunia waweza jikuta unakutwa na hatari ya kuunganishwa  na kuzimu kw sababu ya kuiga au kufuatisha wanavyofanya waimbani wa muziki wa kidunia.

Ishara nyingi za vidole zinazotumiwa na waimbaji wengi wa muziki wa kidunia ni za kishetani na baadhi yao waimbaji hao wanajua moja kwa moja wanachokifanya.

 Imeandikwa "Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili, na aihesabu hesabu ya mnyama huyo; maana ni hesabu ya kibinadamu. Na hesabu yake ni mia sita, sitini na sita (666)."-  --   Ufunuo wa Yohana 13:18

mfano wa chapa hii ya mnyama (damien/shetani) ni alama ya 666 ambyo inatumiwa kama ishara kwa njia ya vidole.

Ishara zingine wanazozionyesha waimbaji wengi wa kidunia ni kama mapozi bali si mapozi kwa kuwa zingine zina maana ya kumtukuza shetani.
Ishara zingine zinakuwa ni za kumsifu shetani kwa kuwapa mashabiki wengi ,kukubalika kwa muziki wa kidunia wanayoimba.

    iii.            Maneno.
“Kwa hiyo nawaarifu, ya kwamba hakuna mtu anenaye katika Roho wa Mungu. . . . . . . . . . . . .. . . ..”1 Wakorintho 12:3
Nataka nikuonyeshe tuu kuwa mtu yeyote anaponena anaweza kunena jambo kutokana na kuhamasika au kuamshwa na roho ,yaweza kuwa ni roho wa MUNGU au ni roho wa shetani.
Kama mtumishi wa MUNGU huwa kuna roho ya MUNGU husema kupitia mumishi huyo.

Je mtu tuu ambaye ni muimbaji wa muziki wa kidunia tuu anaimba baadhi ya nyimbo kupitia roho ya shetani,Yaani kupata awazo ya kishetani juu ya muziki wake naye kuyatimiza ili kuweza kufanikiwa.

4.KUWAKA TAMAA
Imeandikwa “Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu;” -Wakolosai 3:5



Video nyingi za muziki wa kidunia huwa na namna ambayo huamsha watu wanao zitazama hali ya kutamani wanawake,pombe na ngono.
Video hizo ambazo wasanii huvaa nusu uchi na kucheza kwa kuonyesha maungo yao ili tuu kutamanisha.


Mungu hapendi sisi kama wanawe tuwake tamaa zozote bali hupenda tuzishike sheria zae na tuzifuate. “Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi.” 2 Timotheo 2:22
Hivyo basi kwa kuziangalia video za muziki wa kidunia mara nyingi unaweza kujikuta ukiwaka tamaa na kwa hiyo tamaa unakuwa umemkosea MUNGU na unapokuwa umemkosea MUNGU hapo ndipo ulinzi wa Mungu unaondoka maishani mwako na shetani kupata nafasi katika maisha yako.

Kwa hiyo ni bora kujiepusha kusikliza na kufuatilia muzki wa kidunia kwa kuwa unakufanya uwake tamaa ambazo mwishowe utaangamia kwa kuwa imeandikwa.Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele.- 1 Yohana 2:17

5.KUMSIFU SHETANI PASIPO KUJIJUA
Unaweza kujikuta unamsifu shetani bila ya wewe mwenyewe kujijua kama unasikiliza na kufuatilia sana muziki wa kidunia.

Nyimbo nyingi za kidunia huonyesha majivuno,kusifu wanawake,pombe ,ngono na vinginevyo ambavyo vyote hivyo ni kazi ya shetani.


Nyimbo huhamasisha watu kwenda kinyume na maagizo ya MUNGU hivyo kufanya watu wengi wajikute wakimuabudu shetani pasipo wao wenyewe kujijua na mwishowe kuangamia.

KANSA TATU (3) ZINAZOTOKANA NA KUSIKILIZA SANA MUZIKI WA KIDUNIA
Kuna magonjwa matatu ya kiroho yanayotokana na mtu kusikiliza sana muziki wa kidunia.
kwa kuwa mtu asikilizapo huu muziki wa kidunia hujikuta akishindwa kwenda kanisani mara kwa mara akishindwa kusoma bibilia mara kwa mara ,atajikuta hata akishindwa kufanya maombi yake binafsi mara kwa mara.
Magonjwa makubwa ni :-

1.Kuwa na mahudhurio makubwa ya disco,matamasha na nighty club  kuliko kanisani.
Ugonjwa wa kwanza wa kiroho ni kujikuta una mahudhurio makubwa ya kwenda kwenye matamasha ,kujirusha ya muziki wa kidunia kuliko mikesha kanisani au maombi.

Utajikuta unapenda kwenda kwenye matamasha, kutokana na

 i.Mavazi
Kwa kuwa mtu huyu alikuwa akisikiliza sana muziki wa kidunia ataanza kuiga mavazi yake hivyo basi inapofika muda wa kwenda kanisani anajikuta hana vazi lolote linaloendana na kanisani hivyo kujikuta kuendelea kubakia kwenye utumwa wa kwenda disko na matamasha ya muziki wa kidunia.


ii.Styles
Maisha binafsi na muongozo wake unakuwa umebadilika na kuwa anawaza miziki yenye kuharibu maisha yake.Kwa mfano style ya nywele ya kunyoa kiduku au kama ni mwanaume ajikute amesuka,itamfanya azidi kupata sababu ya kutokwenda kanisani kutokana na style ya nywele zake haziendani na za wengine kanisani.

2.Kuvutiwa kusoma habari za udaku kuliko Bibilia(Neno la MUNGU).
Tatizo lingine linalotokana na kusikiliza sana muziki wa kidunia ni kujikuta ukifuatilia sana habari za wasanii ,yaani udaku kuliko kusoma Neno la MUNGU.

Kwa kuwa umeshazoea kuzisikiliza sana nyimbo za kidunia na majina yao una wajua hivyo itakufanya uwe makini kufuatilia mambo yoyote ya maisha yao yawe mabaya au mazuri lazima uwe unayafuatilia na kukufanya kusahau kabisa kusoma neno la MUNGU.

3.Kuweka hazina sana kwenye ngono,wanaume,wanawake kuliko MUNGU.
Imeandikwa “kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako.”- Mathayo 6:21
Badala ya kuweka hazina katika kujitoa katika kazi za MUNGU kwa fedha au hata nguvu basi kwa wanaosikiliza sana muziki wa kidunia hujikuta wakiweka hazina zao kwa wanawake,ngono mdawa ya kulevya.
Hili ni gonjwa la kiroho linalotokana na kusikiliza muziki wa kidunia.

Muziki wa kidunia una athari nyingi nazo hutengenezwa kidogo kidogo kama vile ulikuwa hujui kunywa pombe unaanza kunywa kidogo kidogo,
ulikuwa huna tamaa za wanawake sasa waweza jikuta kutokana na video za muziki wa kidunia unaanza hamasika na kuwa na tamaa na wanawake.

Jiulize wewe mwenyewe kama mkristo unazo nyimbo ngapi za kidunia ,na unazo ngapi za kumsifu MUNGU ?.

Kama una nyimbo  nyingi za kidunia na chache za kumsifu MUNGU basi wewe tambua maisha yako ya kiroho yako kwenye hatari.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...